Bwana harusi amuua baba yake kwa risasi

Bwana harusi amuua baba yake kwa risasi

kirikuu1

Member
Joined
May 11, 2012
Posts
71
Reaction score
19
Mtu mmoja wa miaka 47 aliyejulikana kwa jina la Shirima mkazi wa Kibaha, amemuua baba yake mzazi anayekadiriwa kuwa na miaka 70 kwa kumpigarisasi iliyotoka kwenye SMG yake.

Inasemekana baba huyo alikua amelala nyumbani kwa mwanae na alitokea Moshi kwa mualiko wa harusi ya bwana Shirima ambayo ilikwisha fanyikana hapo bwana Shirima na mkewe walikua honeymoon hapo nyumbani kwao.

usiku wa jana baba yake alipatwa na haja ndogo akaenda chooni wakati anarudi akakosea mlango wa chumba chake na kuingia chumbani kwa mwanae ndipo mke wa Shirima aliposikia mlango unafunguliwa na mtu yupo ndani - akapiga kelele za mwizi hapo ndo mumewe akachukua short gun yake na kumlenga babake na kumuua akidhani ni mwizi.

Inasemekana makazi ya bwana Shirima mtaani kwao nyumba zipo mbalimbali ndo mana akachukua uamuzi wa kumimina risasa bila kuuliza hata swali moja kwa mvamizi huyo wa chumbani kwake.

Imenisikitisha sana habari hii, yamkini tuwe waangalifu kabla ya kuchukua uamuziwowote.

SOURCE WAPO RADIO ASUBUHI HII
 
Hivi kweli kuna uhusiano wa kwenda honeymoon mbali na hili tukio?

sasa kama wangekuwa mbali.....baba angekosea mlango....ingekuwa issue nyingine......we huoni jamaa alikuwa anahami sukari yake mpya...........
 
mfanyabiashara maarufu mkazi wa mlandizi, mkoa wa pwani ndugu BON KAVISHE,amemuua babake mdogo kwa risasi majira ya saa 10 usiku nyumbani kwake mlandizi. tukio hilo limetokea siku ya jumamosi kuamkia jumapili ya tarehe 12.05.2013 baada ya kukamilika sherehe ya harusi ya mdogo wake.taarifa zinadai kuwa baada ya sherehe hiyo ndugu jamaa na marafik wakaenda kujipumzisha.ndipo ndugu KAVISHE ambaye ni mmiliki wa bar maarufu hapa mlandizi ya zimbabwe bar alipoenda kujipumzisha nyumbani yeye na babake mdogo, lakin wakati wa usiku babake mdogo akataka aende choon ndipo katka harakati akajikuta ameingia chumbani kwa mwanae na ndipo mke wa kavishe akapiga kelele akidhani ni mwizi na ndugu kavishe kumpiga risasi na kufariki papo hapo.mpaka sasa ndugu kavishe anashikiliwa na jeshi la polisi kwa mahojiano zaidi.
 
poleni sana wafiwa.
menikumbusha kesi moja bwana mmoja alikuwa anafanya ngono kichakani katika shamba
mwenye shamba akidhani ni nguruwe mwitu waharibifu bila kuuliza akalenga shabaha na kumuua mmoja.
hakuita kujua kama ni mtu yeye alilenga shabaha.
kwa huyu bwana alikuwa na haki hiyo kama eneo hilo kuna wizi nk
jambazi haitwi unalenga shabaha mara moja kama defence yake
akienda mahakamani ataplead manslaugher ataungwa miaka miwili au mitatu au kuachiwa.
ofkoz kuna negligent hapa.
 
Maskini rip baba shirima, chonde chonde tufikiri kabla ya kutenda.
 
Pole kwa wafiwa, kifo cha bahati mbaya ila sheria ifanye kazi haraka siyo mhusika kuwekwa ndani miaka 3 kutafuta ushahidi.
 
Dah hii nimeisikia kwa mtu lakini alinipa juu-juu yeye ana undugu na huyo mtenda kosa,bad luck,anyways tuachie sheria itatenda haki hapo.
 
Nimecheka sana!

Me too!Hivi unawezaje kuhusisha tukio hili na kwenda honeymoon?!!Kwahiyo watu wanaenda honeymoon kuepuka kupiga watu wengine risasi,au kuepuka ajali zinazofanan na hizi?hahaaaaa!!

Sent from my BlackBerry 8520 using JamiiForums
 
Back
Top Bottom