BVR imethibitisha kuna watu ni mapepo

BVR imethibitisha kuna watu ni mapepo

Kaka inategemea na fani za watu. Kuna mafundi ambao kwenye kazi zao hutumia material tofautitofauti ambazo ni vichubuzi kama mafundi uashi (Masons) ambao hutumia saruji bila kuvaa gloves hivyo kuharibu alama za vidole na ndio matatizo kama haya hutokea. Sio kwamba ni vigagula.

Na Gundu Pia Linachangia
 
Sayansi Na Ulimwengu Wa Roho Au Mapepo Wapi Na Wapi?

Vinashabihiana sana....! Labda nikuulize swali rahisi sana ninini kinafanya gari litembee? Au mashine ifanye kazi? Mujibu vyovyote unavyojua
 
Mkuu MSHANA JR mimi pia bvr iligoma mara 2 yatatu ikakubali nisaidie taf. kujua kama nina pepo au ni mtu niliekuwa jirani nae???


The the acha uoga mkuu hauna pepo ila wwe ndio pepo
 
Hii haina tofauti sana na kile walichofanyiwa wale walimu wa mwibara
- unapika chakula kizuri wali nyama ukianza tu kula kinageuka ugali maharagwe
- unalala chumbani na milango unafunga yote lakini kukicha unajikuta umelala nje
- unavaa nguo zako nzuri za gharama ukitoka nje unajikuta umevaa magunia
- unashikwa na kiu unachota Maji unywe ukianza tu yanageuka rangi

Ndugu yangu wewe unaishi enzi za giza na inaonekana unafikiri watu wote wako kama wewe! Mashine ikishindwa kusoma alama za vidole vya mtu basi huyo mtu ni pepo? Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha. 1. Inaweza ikawa mashine hazina ubora (kumbuka kila kitu cha bongo ni under-viwango) 2. Ma-operator ni magumashi (kumbuka ''wataalam'' wengi wa bongo ni magumashi) 3. Waandikishwaji wenyewe eg. magonjwa na baadhi ya dawa zinaweza kufuta alama za vidole.

Influence of Skin Diseases on Fingerprint Recognition: Influence of Skin Diseases on Fingerprint Recognition
 
Fatilia kwa undani hao waliokuwa wanaambiwa vidole havisomi. Ni wale wazee wanaonekana wataipigia ccm. Well done
 
Ndugu yangu wewe unaishi enzi za giza na inaonekana unafikiri watu wote wako kama wewe! Mashine ikishindwa kusoma alama za vidole vya mtu basi huyo mtu ni pepo? Kuna sababu nyingi zinazoweza kusababisha. 1. Inaweza ikawa mashine hazina ubora (kumbuka kila kitu cha bongo ni under-viwango) 2. Ma-operator ni magumashi (kumbuka ''wataalam'' wengi wa bongo ni magumashi) 3. Waandikishwaji wenyewe eg. magonjwa na baadhi ya dawa zinaweza kufuta alama za vidole.

Influence of Skin Diseases on Fingerprint Recognition: Influence of Skin Diseases on Fingerprint Recognition

Na hayo ndio mapepo yenyewe
 
sasa mapepo yanajiandikisha ili iweje yani... wapoteze mda kwenye foleni kisa kitambulisho au kupiga kura wakati wao ni mapepo..... siamini
 
Hazina ubora umethibitisha ama hisia tu

Kama hazina ubora hii itakuwa ni kashfa na aibu kubwa kwa nchi na mamlaka husika kwa kuleta mashine zisizo bora kwenye ishu nyeti kama hii
 
sasa mapepo yanajiandikisha ili iweje yani... wapoteze mda kwenye foleni kisa kitambulisho au kupiga kura wakati wao ni mapepo..... siamini
ISLETS mapepo ni roho zinazotangatanga duniani, zilikuwa kwenye miili iliyokufa, yani miili hiyo ilikuwa ni binadamu kamili wa kada mbalimbali katika maisha, wezi watukutu, maofisa, wataalam wa fani mbalimbali, malaya, matapeli nk nk

Mwili uharibikao unapofikia tamati(kifo), roho huondoka na background ya mhusika, unaweza kutumia neno memory card au database..... Na kutafuta mwili wa kukaa kwa muda na kufanya chochote kile, kiwe kibaya au kizuri au vyovyote vile
Ni kipindi hiki ndio watu hubehave kwa namna ya ajabu kabisa

Ni wazi ushawahi kusikia watu wakisema hivi huyu leo sijui yukoje? Au mwacheni huyo leo kavurugwa au ana stress zake au hivi fulani mbona siku mbili hizi simuelewielewi? Nk nk
 
Last edited by a moderator:
Siyo kwamba mashine zinashindwa kuscan alama za vidole, ni kitu kingine tu waeleze vizuri, sanasana ni tatizo la kiufundi. As kwa huko Malaysia kilichotokea nadhani ni kwamba scanner inascan, inapojaribu kutafuta taarifa za mtu huyo kwenye database inakosa. Sijuwi hao watu walikuwa na passport za wapi, nchi nyingine passport zao zina chip inayohifadhi taarifa. Scanner haishindwi kuscan hata uweke tak.o, labda iwe na tatizo tu. Lakini wabongo watakimbilia uchawi, uchawi hauna nafasi kabisa kwenye teknolojia.

Kati ya watu wenye uelewa mdogo wewe unaongoza,kwa hiyo unapinga kuwa hakuna uchawi? Umeambiwa kuwa hayo mambo hutokea ktk ulimwengu wa roho,(the spiritual world) ambayo huwezi kuyaona ktk macho ya kawaida,si kila jambo ukimbilie teknolojia tu,uchawi upo,mapepo yapo na tunaishi nayo,mwaka 2006 nikiwa Newyork kwenye kitongoji cha brooklyn tulimbeba dada mmoja usiku aliyekuwa kaomba lift ile kufika ktk cemetery area akaomba kushuka na hapakuwa na nyumba,alitoweka ghafla.
 
nilibahatika kufanya kazi ya bvr, kwa muda wa wiki nne niliofanya kazi hiyo nilizalisha vitambulisho 1700 na ushee hivi. Kituko pekee nilichokutana nacho ni hiki, alikuja mama mmoja kipofu alivaa kaniki huku amejifunga kamba nyekundu kiunoni, kichwani na mikononi, wanaovaa hivyo huwa wanasema wana majini. Ilipofika zamu yake kazi ikaanza ya vidole kukataa kusoma, nilijaribu mara tano pamoja na kufuta vidole vyake kwa kitambaa ilishindikana. Mama mmoja kati ya wawili waliomsindikiza akamwambia yule mama kipofu kwani wewe si unamajini waombe wakuruhusu. Basi yule mama kipofu aliomba sekunde kadhaa kwa kilugha ya kabila lake alichanganya na kiswahili, nachokumbuka alisema hicho anachotaka kufanya ni kwa ajili ya kupata kitambulisho cha kupigia kura hakina madhara na wao majini. Baada maombi yake hayo nikaanza tena kuchukua alama za vidole vilikubali na watu wengine waliokuwepo wakisubiri zamu yao tukaishia kucheka tu na yule Mama alipata kitambulisho chake.
 
nilibahatika kufanya kazi ya bvr, kwa muda wa wiki nne niliofanya kazi hiyo nilizalisha vitambulisho 1700 na ushee hivi. Kituko pekee nilichokutana nacho ni hiki, alikuja mama mmoja kipofu alivaa kaniki huku amejifunga kamba nyekundu kiunoni, kichwani na mikononi, wanaovaa hivyo huwa wanasema wana majini. Ilipofika zamu yake kazi ikaanza ya vidole kukataa kusoma, nilijaribu mara tano pamoja na kufuta vidole vyake kwa kitambaa ilishindikana. Mama mmoja kati ya wawili waliomsindikiza akamwambia yule mama kipofu kwani wewe si unamajini waombe wakuruhusu. Basi yule mama kipofu aliomba sekunde kadhaa kwa kilugha ya kabila lake alichanganya na kiswahili, nachokumbuka alisema hicho anachotaka kufanya ni kwa ajili ya kupata kitambulisho cha kupigia kura hakina madhara na wao majini. Baada maombi yake hayo nikaanza tena kuchukua alama za vidole vilikubali na watu wengine waliokuwepo wakisubiri zamu yao tukaishia kucheka tu na yule Mama alipata kitambulisho chake.

cc: macho_mdiliko na wale wote waliokuwa wakipinga nilichoandika, asante saana Kusai kwa ushuhuda huu, mjadala unaweza kwenda vema sasa
 
Last edited by a moderator:
Ni michezo tu ili mpate muda wa kufikirisha bongo....viganja vinakuwa kama miti japo kwa macho ya kawaida unaona ni viganja kamili
Umeona ile video ya ifakara yule jamaa anayeshindwa kuangalia kabisa camera ili apigwe picha? Mwenye kuitaka aniambie nimtumie

Tafadhali nitumie Jr mshana
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom