Elections 2010 BUNGENI: Upinzani upo ndani ya kambi ya upinzani?

Na wale tisa (9) ambao kura zao waliziharibu hao umewaweka wapi? kwamba ni popo hawajulikani wako upande upi?
 
Hakuna kukaa.nasema mawazo haya ni potofu.cuf wana ndoa na ccm,nccr kadhalika,tlp ndo usiseme.udp mnajua.chadema nenda mwenyewe.jenga upinzani hadi kieleweke.nafurahi wapinzani feki wameonekana mapema.chadema mwendo mdundo.
Wewe umesema. Nitfute baadaye nikupe pipi.
 
Kwa mtazamo wangu nimeyapokea matokeo ya uspika ( makinda kura 265 na marando kura 53) kama kuna upizani ndani ya kambi ya upinzani ambao ulianza wakati wanachagua kiongozi wa kambi ya upinzani bungeni, nimesikia cuf nao watachagua kiongozi wao licha ya chadema kumchagua mbowe kutokana na kutimiza masharti kwa kanuni za bunge, huu ni mpasuko ndani ya kambi ya upizani na haswa huletwa na cuf, niwaombe wabunge wa upinzani kukaa ili waweze kutoa hizi tofauti zao, maana kama wanataka kuibomoa ccm lazima wawe kitu kimoja.

Si sahihi kuiweka CUF katika kambi ya upinzani kwa kuwa wameishafunga ndoa na CCM kule zenji ktk serikali ya mseto, that means CUF ni ndugu zaidi na CCM kuliko vyama vingine, na kwakuwa CUF ndo walioolewa hawatakuwa tayari kwenda kinyume na matakwa ya bwana wao CCM. Navionea huruma vyama vingine vilivyoingia ktk mkumbo wa CUF vitaishia kuonekana kama ni mamluki wa CCM na vikajifia kifo cha mande. NCCR ina wabunge vijana makini sana, haikutakiwa kuwapeleka vijana wale ambao wanatakiwa kukijenga chama chao kumezwa na CUF ambayo miaka yote msimamo wake hautabiriki na imeundwa na wabunge wengi wanaotetea maslahi ya Pemba ambayo hayatawavutia wapigakura wa huku bara hapo 2015.
 
Lengo ni kufanya kazi uliyotumwa na watu wako nasi kukaa unawalazimisha chadema waungane nawewe, au subiri mpaka wakati wa uchaguzi.
 
Mhhhhh!!!!! NILIJUA TU UROHO UROHO , UROHO WA MADARAKA. HII INAONYESHA HATA MKIIONDOA CCM MAFISISADI MTAKUWA WENYEWE!!!! AIBU GANI HII JAMANI?!!!!!!
 
Yaliyotokea ni haya hapa:

Kutoka ndani ya uvungu wao...
Walikaa Chadema na CUF ili waone wataingiaje Bungeni. Kabla ya Uchaguzi wa Spika, Hamad Rashid alitaka kugombea Uspika, Chadema wakamwambia hapana wacha Agombee huyu Mwanasheria, wewe utarudi katika kambi ya upinzani kwa cheo chako kile cha awali, na kwa kufanya hivyo tutagawana madaraka. Hamad akawakubalia na kuondoa azma yake ya kugombea U-Spika alipofanya hivyo, Zito akaibuka na kusema Wataunda kambi Chadema peke yake bila kushirikisha vyama vingine. hilo nalo. Hapo ndipo Marando alipozikosa kura ambazo zingemvusha kwenye Uspika. Na hii imefanyika kutokana na ufinyu wa fikra (kama sio viongozi waandamizi wa Chadema kupewa chochote toka CCM) wakidhani kwamba umaarufu unatokana na kuongoza kambi ya upinzani bungeni bila kuwa na ushirikiano kutoka vyama vingine. Walichokisahau Chadema ni kuwa CUF walijaribu kutoshirikisha vyama vingine awali na kisha wakajirekebisha, na hapo wasiomjua Slaa ndipo walipomtambua. Ila kwa kwa hili la ubinafsi wa CHADEMA wameumaliza UPINZANI Tanzania. Tutafute kaburi tuuzike...

Tusubiri kuundwa kwa chama kipya kisicho na damu ya U-CCM-CCM.:sad:

Nawasilisha.
Source!? Ondoa spin zako hapa we mjinga. Nenda kule ccm ukawambie ujinga wako huu.
 
mh kwa mbinu za sisem watahakikisha wanaisambalatisha chadema vibaya mno. sasa nijukumu ya wabunge wa chadema na wanachama kuwa na msimamo sana kutokudanganyika!
 
Jamani kumbukeni kwamba hata Zanzibar CUF waliingia kwenye makubaliano baina yao na CCM. Na hawakushirikisha chama chochote kingine.

Nawashangaa ambao mnaamini kuwa CUF wanaweza kuwa na ushirikiano na Chadema ktk bunge la JMT wakati huo huo kuwa na ushirikiano na CCM katika baraza la wawakilishi Zanzibar! Only a foul will buy this idea. Kumbukeni CCM ni ile ile ya Zanzibar na Bara na vile vile kwa CUF.

Kama mlifuatilia kwa makini mwenendo wa Prof. Lipumba wakati wa kampeni, kutangazwa matokeo na kisha kuapishwa kwa Rais wa JMT ni wazi alikuwa against Chadema zaidi kuliko ambavyo alikuwa against CCM. Kifupi alikuwa akimpigia kampeni JK. Na hii yote ilitokana na kutotaka kuharibu ndoa yao (ulaji wao) na CCM kule Zanzibar.

In short, hizo ndo hulka za viongozi wa bara la Afrika. Wamejaa ubinafsi na uzandiki.

Maalim Seif ameshasahau watu waliomwaga damu na maelfu kukimbilia nchi zingine kama wakimbizi!!

Mkuu umesema ukweli kabisa. Thanks.
 
Baada ya CUF kuungana na CCM kuunda serikali ya mseto, ni vizuri watanzania wote waelemishwe kuwa chama pekee cha upinzania kilichobaki Tanzania ni Chadema. Kulikuwa na nafasi ya vyama vingine kama TLP, NCCR navyo kuwa vyama vya upinzani. Lakini baada ya TLP, NCCR na vyama vingine kuungana na CUF bungeni inamaanisha kuwa CUF, TLP, NCCR vyote vimeungana na CCM. Hivyo, kama ambavyo tumeendelea kutoa elimu ya uraia kwa watanzania, tuendelee kuwafahamisha na waelewe kuwa chama cha upinzani na ambacho kinatetea masilahi ya Watanzania nchini kwetu ni Chadema pekee. Ujumbe huu na uenee nchi nzima sasa.


Hii ni muhimu na ya haraka sana....
 
Kaka Chadema magugu mengi, na magugu huwa yakiota mimea mizuri inakuwa hatarini. Zitto, wenje, .........
 
Ni kweli maneno yako maana ndio maana hawakuwashirikisha wenzao kuunda kambi ya upinzani bungeni kwa kujiona wao ndio wapinzani peke yao, hawakuwashirikisha kwa kuwapa japo umakamu.
 
ukweli ni kwamba Marando hakuwa ktk nafas ya kushinda hata kama cuf wote wangempigia kura lkn leo nimeamini kuwa cuf ni ccm na chadema wanalijua hilo ndo maaana sometimes wanakua na msimamo wao binafsi hawataki unafiki. chama cha upinzan pekee ni chadema.
 
Yaliyotokea ni haya hapa:

Kutoka ndani ya uvungu wao...
Walikaa Chadema na CUF ili waone wataingiaje Bungeni. Kabla ya Uchaguzi wa Spika, Hamad Rashid alitaka kugombea Uspika, Chadema wakamwambia hapana wacha Agombee huyu Mwanasheria, wewe utarudi katika kambi ya upinzani kwa cheo chako kile cha awali, na kwa kufanya hivyo tutagawana madaraka. Hamad akawakubalia na kuondoa azma yake ya kugombea U-Spika alipofanya hivyo, Zito akaibuka na kusema Wataunda kambi Chadema peke yake bila kushirikisha vyama vingine. hilo nalo. Hapo ndipo Marando alipozikosa kura ambazo zingemvusha kwenye Uspika. Na hii imefanyika kutokana na ufinyu wa fikra (kama sio viongozi waandamizi wa Chadema kupewa chochote toka CCM) wakidhani kwamba umaarufu unatokana na kuongoza kambi ya upinzani bungeni bila kuwa na ushirikiano kutoka vyama vingine. Walichokisahau Chadema ni kuwa CUF walijaribu kutoshirikisha vyama vingine awali na kisha wakajirekebisha, na hapo wasiomjua Slaa ndipo walipomtambua. Ila kwa kwa hili la ubinafsi wa CHADEMA wameumaliza UPINZANI Tanzania. Tutafute kaburi tuuzike...

Tusubiri kuundwa kwa chama kipya kisicho na damu ya U-CCM-CCM.:sad:

Nawasilisha.

kama hiyo avatar ni picha yako basi mtu mzima ovyooo,
what is your source au umetoka kulala saivi?
 
Tukipata serikali 3 kiburi cha cuf kitakoma kwani watakuwa na mbunge mmoja au wawili au hakuna kabisa. Wabunge wa CUF znz ndio wanaoitoa cuf tanzania bara. Sasa cuf wamefunga ndoa ya mkeka Znz halafu wanataka tena na Bara kufunga ndoa na wapinzani, huu ni umafia wa ccm ktk kuua upinzani. Bora kuishi bila kuoa (chadema) kuliko kuoa mke cuf.
 
Back
Top Bottom