Bungeni pawaka: KURA YA SIRI vs KURA YA WAZI

Upigaji wa kura wa siri ndio suluhisho pekee litakalowapa uhuru wajumbe kufanya maamuzi bila ya shinikizo au vitisho. Khofu hasa ya nini kushinikiza watu kupiga kura kwa uwazi huku tayari mushaweka vitisho vya kuwafukuza, na kuwa brand wasaliti? Hivi tumeamua kubadili katiba ili kunyosheana vidole baada ya mabadiliko au kufuta uhasama na kuanza chapter mpya ya maendeleo?

Kama kawaida hoja ziszo na mashiko kulifananisha bunge la marekani na la Tanzania maana sijawahi kuona kura za kumchagua house speaker wa marekani kuzidi wajumbe wenyewe. Tusijitie upofu tukasahau kwamba uoza wa rushwa, vitisho na lack of ethics ndio hasa chanzo cha bunge letu likawa bovu lenye kubeba wingi wa maslahi binafsi ya posho badala ya agenda ya mabadiliko ya kweli yenye asasi ya wananchi na maendeleo yao.

Tatizo letu ni kuzowea fitna, kunyosheana vidole na kuziba demokrasia ya uhuru wa mtu kuwa na kauli yake bila ya shinikizo. Hivi umeona wapi katika mazingira magumu kama ya sasa halafu tukaweka wazi kura ambazo zinakila ya dalili ya kuwa patronise na intimidate wajumbe kukubali wasioyaamini. Napolean naye pia aliwahasisha wafaransa kukubali mfumo wa kupiga kura kwa uwazi lakini wananchi waligoma kwa sababu bias ya kura za kuonekana hazitakuwa na uzito wa legitimacy ya kweli kwa wapigaji. Hivi hasa munakusudia kuwafanya nini wale ambao watakwenda kinyume na itikadi zenu hata mushadidie kura za uwazi?

sasa kuna wimbi la uhalifu mkubwa wa wanaomwagiwa acid n.k kwa vile tu wanamitazamo tafauti sasa munachokitaka kukifanya hamuoni kwamba munawaweka wajumbe katika hali ya hatari pale bunge linapomalizika na wenye visasi kuwasubiri kwa kuwahujumu? hamuoni kwamba uwazi wa aina hii unaweza kuzua balaa katika jamii na hata kuondosha hali ya utulivu tulionayo? Hivi uwazi wa kura unafaida gani kubwa zaidi ya kuwafitinisha watu kwa sababu ya mitazamo tafauti?

Lengo la kura yoyote ni uhuru wa kuamua ulitakalo bila ya intimidation, threat na bias. faida ya kura ya siri ni kwamba hasa katika kura ya kubwa ya katiba ni kuhakikisha beyond any reasonable doubt wajumbe wanafanya maamuzi yalio moyoni mwao na kama rais alivyosema hakuna haja ya vitisho, ngumi na kunyosheana vidole, kikubwa ni hoja. Kwa nini hasa watu wasijikite katika hoja badala ya hii hamkani ya demokrasia ya punishment ya kura za wazi au masuala ya kusomeana halbadiri?

Bunge lisiendeshwe kienyeji enyeji, hivi tuseme kura za wazi tutaziita ni uhuru wa kweli? Tunahofu nini hasa hata tukashindwa kutumia common sense katika suala kubwa na zito kwa taifa? Hoja ya kwamba suala hili ni la kitaifa na ni vyema watu wakawa mashujaa na kuwa wawazi katika kura ni hoja dhaifu, maana hakuna nafasi kubwa katika nchi kuliko hio katiba kama nafasi ya Rais na madaraka makubwa aliopewa nayo including kulivunja bunge na kuunda bunge jengine bias litakalofuta katiba na kumpa inayomfavour, lakini hatupigi kura ya uwazi bali ya siri. hata hao wajumbe wa hilo bunge nao pia hupigiwa kura ya siri na ndio sasa wanamamlaka ya kubadili katiba sasa kwa nini tusingewapigia kwa uwazi.

Misingi ya demokrasia iko wapi? tumekuwa na kangaroo courts zisizojali maadili, bunge dhaifu la wapenda posho, nahata hili la kura nalo litiwe dosari kwa kuhalalisha kisichotakiwa na wananchi? wengi tulitarajia lengo la katiba mpya ni kuanza chapter mpya ya maendeleo na kusahau yaliopita, hivi hii nia tunayo kweli wakati dalili za makusudi za kuwekeana visasi zinatunzwa ati kwa misingi ya national interests, hivi jamani tumekusudia kuipeleka wapi hii nchi. Wapeni haki na dhamana tuliowapa kwa kuwaachia kila mjumbe uhuru wake wa kura ya siri ili tuweze kupata katiba ilio bora na yetu sote.

Kama kuna umuhimu wa kura za uwazi, mungelianza basi kati chaguzi za vyama vyenu kuanzia nafasi ya Mwenyekiti na kuendelea. Kwani kisa cha kura za maruhani zilianza vipi? Hebu kuweni sensible na muwache huu utoto sasa.

 
Ccm kwenye hili wako sawa tunaangalia katiba kwa ajili ya wananchi kama kuna mtu anaogopa kufukuzwa huyo hafai kuwa kiongozi ester bulaya amesema yy ni muumini wa kura ya siri tuone hata afukuzwe
Hii ya 77 ilipigiwa kura ya aina gani?66666!
 
Jamani wanazuoni, haingii akilini kumuona mjumbe anasimama kwa guts zote ..naunga mkono kura ya wazi. Je hawa wanafaham kuwa watapigiwa kura 2015 hawa wale wabunge au ndo kujiripua. Tuelemishe jamii iwaogope hawa kama ukoma. Tuwe wa kweli jamani na,sio ushabiki wa vyama. Mimi naunga mkono kura ya siri hata mke wangu sitamwambia kwani ndo demokrasia ya kweli.
 
JANA NILIMUONA MBUNGE KAPUYA AKICHANGIA KANUNI ZA BUNGE KUHUSU KURA IWE YA SIRI AU YA WAZI AMENIFURAHISHA SANA ALIVYOWEZA KUTOA YA MOYONI MWAKE BILA KUJALI MSIMAMO WA CHAMA CHAKE NIMEFURAHI PALE ALIPOPENDEKEZA KURA YA SIRI WAKATI MSIMAMO WA CCM NI KURA YA WAZI KWAKWELI AMENIFURAAISHA SANA AMEONYESHA KWELI YEYE NI PROFESA NA PROFESA HAWEZI KULISHWA MANENO NA WATU WENYE UDOCTORWA KUPEWA BILA KWENDA SHULE NA WENGINE KAMA AKINA NAPE. NAPENDA KUWATAHADHARISHAWANA CCM WENYE AKILI ZAO MSIKUBALI KUSHIKIWA AKILI NA WATU WENGINE HATA SHULE HAWAJASOMA VIZURI LAKINI KWAVILE NI KIONGOZI WA CCM ANAWAENDESHA TU. MNAOGOPESHWA MTAWAJIBISHWA KAMA MKIENDA KINYUME KWANI HAO KINA NAPE NDO HAO WANANCHI WA JIMBO LAKO WALIOKUPA KURA?? NYIE SIMAMIENI HAKI WAKUWAFUKUZA CHAMA KUNA VYANA KIBAO VYA KUJIUNGA NAVYO ILIMRADI TU ULISIMAMIA HAKI YA WANANCHI UTACHAGULIWA TU.:flypig:
 
mimi naona lengo la ccm ni kukwamisha upatikanaji wa katiba mpya ili katiba hii mbovu iendelee kutumika,kwa sababu haiingii akilini toka lini ccm wanapenda uwazi, maana kama wanapenda uwazi wangeanzia kwenye mikataba mibovu, waliohusika na kashifa ya EPA na kufichwa kwa gavana balali, richmond, wizi wa fedha za umma n.k., hapa wanachokifanya ccm ni kucheza sarakasi, lakini wananchi tunaona na muda ukifika watakiona cha mtema kuni.
 
Huyu Mjumbe anaetaka kura za wazi ni MPUUZI wa hali ya juu na hajui kilichompeleka huko. Anatakiwa kujua kuwa katiba hii ni kwa ajili ya watoto na wajuu wake zaidi! aache kufikiria TUMBO lake analochumia kwa vijisenti vya kuhongwa na wasioitakia mema NCHI yetu! MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
Yaani wee ukizeeka utakuwa mchawi kabisa umeona watu hawachangii hii thread yako kwanini? Umekaa kuiumbea mbea tu!

Next time tumia kichwa kufikiri na siyo kunyoa KIDUKU!
 
Ni kama vile ccm wanataka kura ya wazi ili kuweza kuwajua wajumbe wao ambao ambao wataowasaliti.
Wakati wapinzani wengi na baadhi ya wabunge wa ccm wanataka kura siri.
Mimi nataka kura ya siri.
Wewe jeeee?
 
Wajumbe wanaopendekeza kura ya"siri" ni kutoka makundi yote,,wa kura ya Uwazi....!?
Bunge la katiba linaloendelea tangia juzi kuhusu ni aina gani ya kura iwe inapigwa wakati wa maamuzi ya jambo au kifungu kitakacho kua na ubishi,limeendelea kuonyesha mgawanyiko mkubwa sana kati ya wajumbe wa Bunge maalum la Katiba.

Katika mapendekezo ya tume ya bunge yaliyoletwa kwa wajumbe wa bunge maalum la katiba juu ya Kanuni za kuendesha bunge hilo la katiba,tume hiyo imependekeza kura iwe ya siri au ya wazi.

Baada ya mjadala huo kupamba moto tangia juzi,baadhi ya Wajumbe wa katiba waliopata nafasi ya kuchangia au kutoa mapendekezo yao juu ya kura ya Uwazi na Usiri,,wajumbe kutoka vyama vya Cdm,Cuf,Nccr,vyama mbalimbali na taasisi zote isipokua Ccm pekee,walipendekeza kura za siri.

Pamoja na kua msimamo wa Ccm kwa maelekezo ya Waziri Mkuu mh,Pinda(kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima) ni kura ya siri,bado wabunge wake wawili Ester Bulaya na mwenzake waliunga mkono hoja ya kura ya "siri".

Hadi sasa ukijaribu kuangalia ni kwamba wajumbe wengi kutoka vyama vyote na taasisi mbalimbali wanapendekeza kura ya Siri ndio itumike kuamaua mambo mbalimbali yatakayo kua na ubishi au utata.

Wajumbe wa kutoka chama kimoja(Ccm) pekee ndio wanaopendekeza kura ya Uwazi.

Nauliza je Demokrasia ni kuwapa wa upande mmoja (Ccm pekee) au kuwapa walio wengi (nikimaanisha mchanganyiko wa Cdm,Ccm,Cuf na taasisi mbalimbali?)

Kiuhalisia hadi sasa hoja za Ccm hazina mshiko kwa kuwa ni wao pekee ndio wanaopendekeza kura iwe ya siri huku vyama vingine na taasisi mbalimbali wakipendekeza kura ya Siri,kwa maana hiyo ukweli utabaki tu kua ukweli kwamba Ccm tayari imeshindwa!
 
Ili kupata muafaka wa kura gani itumike itabidi papigwe kura. Je, itakuwa kura ya wazi au ya siri???
 
CCM hawawezi kukubali kura ya siri kwa kuwa ile "NEC ya tume" haipo bungeni na uchakachuaji hautawezekana. Kura ya wazi (dhahir) itawasaidia kuweka msimamo wa pamoja kwa kuwa atakayepiga kura tofautiataonekana sio mwenzao! Ila wakichaguana wenyewa .........ah kura ya siri bana!

22.jpg


IMG_3038.jpg
 
Nimeona Jana wakikazia Kira wazi. wazandiki hao. never! qanat aka wawabame wana mageuzi ndani ya ccm. Waco wengi.
 
Wajumbe wanaopendekeza kura ya"siri" ni kutoka makundi yote,,wa kura ya Uwazi....!? Bunge la katiba linaloendelea tangia juzi kuhusu ni aina gani ya kura iwe inapigwa wakati wa maamuzi ya jambo au kifungu kitakacho kua na ubishi,limeendelea kuonyesha mgawanyiko mkubwa sana kati ya wajumbe wa Bunge maalum la Katiba. Katika mapendekezo ya tume ya bunge yaliyoletwa kwa wajumbe wa bunge maalum la katiba juu ya Kanuni za kuendesha bunge hilo la katiba,tume hiyo imependekeza kura iwe ya siri au ya wazi. Baada ya mjadala huo kupamba moto tangia juzi,baadhi ya Wajumbe wa katiba waliopata nafasi ya kuchangia au kutoa mapendekezo yao juu ya kura ya Uwazi na Usiri,,wajumbe kutoka vyama vya Cdm,Cuf,Nccr,vyama mbalimbali na taasisi zote isipokua Ccm pekee,walipendekeza kura za siri. Pamoja na kua msimamo wa Ccm kwa maelekezo ya Waziri Mkuu mh,Pinda(kwa mujibu wa gazeti la Tanzania Daima) ni kura ya siri,bado wabunge wake wawili Ester Bulaya na mwenzake waliunga mkono hoja ya



mkuu hebu pitia tena hii habari yako na urekebishe makosa kidogo ya uchapaji yaliyomo
 
CCM watuambie kuna nini hata wang'ang'anie kura ya wazi inayohatarisha usalama wa wajumbe? Kura ya siri ina madhara gani hata waipinge hivyo? Watanzania tutafakari sana nyuma ya pazia kuna nini?
 
Back
Top Bottom