Bungeni: Lowassa atangazwa Mtoro

Bungeni: Lowassa atangazwa Mtoro

Mwanakili90

JF-Expert Member
Joined
Nov 24, 2010
Posts
1,568
Reaction score
246
Katika zoezi linaloendelea hivi sasa,la kupiga kura ya kupitisha Bajeti,Mh.Edward Lowasa ameitwa mtoro na wabunge wenzake baada ya jina lake kuitwa na kuwa kimya,kuna mbunge akaitikia mtoro.
 
Mafisadi wote hawapo,sema kwa lowasa wameropoka tu mtoro
 
Ajabu ya UTORO ni nini? Unless kuna UDHURU, usipokuwepo mahali bila taarifa ni utoro tu au kuna neno laini zaidi?
 
Hawana jeuri ya kumsema akiwepo hao...Walikuwa well sure kwamba hayupo ndio wakasema hilo!
 
Sasa Lowasa aache kufanya mambo yake ya maana aje kwenye bunge ambalo wabunge wa ccm kazi yao ni kusema ndio!,........... Lowasa ni mjanja sana ataki kuwa sehemu ya lawama kwa kupitisha bajeti ya hovyo kama hii. Ongera sana Lowasa.
 
Wametoka ili kuja kutengeneza michongo na namna ya kuihujumu serikali!
 
huku kwetu TAA ZIMA wamezima umeme wao tokea jioni hii
 
hata angekuwepo hataki bughudha. Eti akabishane na watoto wa jana kwenye siasa kama kina Lema wanaotangaza siasa mbele ya majeneza kanisani huku akisimama madhabahuni? Lowassa anafaa awakwepe wahuni kama kina Lema
 
Hawana jeuri ya kumsema akiwepo hao...Walikuwa well sure kwamba hayupo ndio wakasema hilo!

Kwani EL haangaliagi hata luninga? Maana anaweza kua hayupo bungeni lakini akawa anacheki kupitia luninga. So if that is the case, then jamaa walioropoka "mtoro" wana libalaa likubwa!!!
 
kwani huyo lowasa ni nani hadi awape watu kimuhe muhe??????????????
 
Back
Top Bottom