Bunge limetukanwa - Hakuna anayepiga kelele?!

Bunge limetukanwa - Hakuna anayepiga kelele?!

pasco kijana wangu, kitaaluma umefafanua vizuri.

Lakini hata katika taaluma kuna kukosea kutafsiri. Mikataba ni siri kwa mujibu wa law of contract kama parties wa mkataba wamekubaliana hivyo. Tuchukulie kuwa katika KADCO parties walikubaliana iwe siri. Parties ni nani na nani? Mamlaka ya Viwanja vya ndege na KADCO. Mamlaka ya viwanja vya ndege inamilikiwa na Serikali na kwa kupitia Wizara husika, mkataba huu ulitakiwa kupelekwa kama taarifa kwa kamati ya bunge husika. sijui kamati gani.
Suala la kodi ya dola 1000 kwa mwaka sio suala la siri maana si lazima mamlaka zinazohusika na kodi za mapato zijue?
Mkataba huu unaweza kuwa halili lakini mbovu (legal but bad contract) kwani mwenye mali analipwa kidogo na mkodishaji.

KADCO ni pamoja na Mzee Kilewo kama mmoja wa wanahisa.
 
Tanzania hakuna wabunge ila waheshimiwa wanaopokea allowance (double) kwa kutumia jina la uwakilishi wa wananchi in fact wanawakilisha matumbo yao..lol
 
Kwa mtizamo wangu mfupi mimi naona kuna haja ya kushughulika na mtu personaly anaeingia mkataba kwa niaba ya serikali na kuachana na kivuli wanachojifichia cha serikali. Mfano waziri anapokuja na sentesi kama hii ya KIA basi tushughulike nae parsonaly kuwa ndie kaingia mkataba wa kijinga na kumuwajibisha. Hii janja ya sisi kudanganyika kwa kuimba serikali, serikali wakati ni mtu au kundi kwa njaa zao wanafanya madudu itatupotezea mda mwingi na watoto wetu watakosa urithi. Ajulikane nani kahujumu na anakaa wapi na genge linalomuunga mkono ni kina nani basi kama serikali itashindwa kuchukua hatua husika, umma utazichukua!! WE ARE VERY MUCH AWARE THAT PRIVATIZATION AND FREE MARKET IS NOT ABOUT STEALING!!
 
Ni bahati mbaya kwamba, kila siku kuna taarifa za ufisadi mpya lakini hatuoni hatua.Inaumiza kila siku kupata data za mabilioni ya fedha za umma kutafunwa but things are the same always.Ni nani hasa atatangaza mwisho wa upuuzi huu?Watu wako comfortabe kabisa,Waliosanini mikataba hiyo ya ubakaji wanaendelea kula kiyoyozi bila wasiwasi wowote.Twafa.
 
Ni bahati mbaya kwamba, kila siku kuna taarifa za ufisadi mpya lakini hatuoni hatua.Inaumiza kila siku kupata data za mabilioni ya fedha za umma kutafunwa but things are the same always.Ni nani hasa atatangaza mwisho wa upuuzi huu?Watu wako comfortabe kabisa,Waliosanini mikataba hiyo ya ubakaji wanaendelea kula kiyoyozi bila wasiwasi wowote.Twafa.

Ufisadi ulikuwepo siku nyingi lakini hatukustuka kwa vile ulifanya kiaina. Sasa mafisadi wamejisahau na wanakula mchana bila hata kunawa na wanategemea hatuwaoni. Hakika sikio la kufa........!!!!!!!!!! Sasa ni sisi wananchi wenyewe wenye uwezo wa kuwafundisha adabu badala ya kumsubiri rais mchumi ambaye hata hajui kwa nini TZ inakuwa maskini atusaidie.
 
Duh, kweli siku moja nchi itawaka moto na hakuna kwa kukimbilia, bado TTCL vs Airtel pia serikali inasemaje kuhusu share zake? Zipo kweli? Any results from Due Dilligence reviews? ni sawasawa na mtu aliyemwagiwa upupu, anajikuna mwili mzima; ndo TZ ilivyo kila ugusapo ni Ufisadi tu!
 
Juzi Mbowe kaomba ajulishwe makampuni yaliyokwapua hiyo stimulus package ya Kikwete, jibu alilopewa na naibu waziri wa fedha ni kuwa sheria na kanuni za benki zinazuia kuyataja makampuni hayo, Kweli?
 
Mzee wa Busara, wote hatuwezi kukata tamaa. Nilisema huko nyuma kuwa "Taifa la watu Duni linajengwaje" Maana yangu hasa ilikuwa ni vigumu (kama siyo haiwezekani kabisa) kujenga Taifa la watu walioakata tamaa!! Ni kwa sababu hiyo nilishaapa huko nyuma kwa mizimu ya kikwetu kuwa sitakaa kimya na nitaendelea kupaza sauti yangu kama Yohana Mbatizaji kuwatangazia watu kuwa wakati wa "toba" ni sasa kwani "shoka limeshainuliwa dhidi ya shina!"

Mie napita tu humu wakuu...................
 
Back
Top Bottom