Bunge limetukanwa - Hakuna anayepiga kelele?!

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,987
Na. M. M. Mwanakijiji
KLH News
Daima Macho – Hatulali mpaka kijulikane!


16New.JPG

Jengo jipya la Bunge Dodoma!

Bunge letu limetukanwa hadharani. Nilisubiri kwa hamu kuona kama kuna mwandishi, mbunge au kiongozi yeyote wa Tanzania ambaye atapaza sauti yake na kupiga kelele kufuatia taarifa kuwa kuna mikataba iliyotiwa saini na vyombo vya Tanzania ambayo inakataza Bunge (wawakilishi wa watu) kuihoji, kuingalia au hata kuipitia mikataba hiyo.

Hivi karibuni Mbunge wa Jimbo la Kigoma Kaskazini Bw. Zitto Kabwe (CHADEMA) alitaka serikali iulete Mkataba wa uendeshaji wa Uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro ulioipa kampuni ya KADCO kazi hiyo kwa malipo ya Dola 1000 (ndiyo, elfu moja) kwa mwaka wakati kampuni hiyo inapata karibu Dola 5000 kwa siku toka KLM. Bw. Kabwe alitaka wabunge wapewe nafasi ili waweze kuusoma na kuelewa ni kitu gani kilichokubaliwa ndani ya mkataba huo. Hata hivyo Naibu Waziri wa Miundo Mbinu Dr. Maua Daftari alisema kuwa kipengele cha 30.4 cha mkataba huo “kinaifunga serikali na mbia wake, Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO), kutoa habari kwa mtu yeyote ambaye si mhusika wa moja kwa moja kwenye utekelezaji wa mkataba huo.” Kwa mujibu wa Dr. Daftari na ilivyonukuliwa na gazeti mojawapo nchini “wabunge si wahusika wa moja kwa moja na mkataba huo, badala yake serikali itaendelea kuwawakilisha.”

Hapo sasa ndipo naona ya kuwa Bunge letu limetukanwa hadharani. Kinachoudhi na kukera ni kuwa Wabunge wa CCM na wale wa Upinzani wamekubali maelezo ya Dr. Daftari bila upinzani wa kina wa hoja ya kuwa wao hawana haki ya kupewa maelezo na ikibidi kupitia mikataba hiyo wao wenyewe. Ni sawa na mtu kuambia umedondosha kitu na unapobongoa anakupiga teke na wewe unageuka na unapotaka kulalama anasema hauna haki ya kulalama! Serikali si wawakilishi wa wananchi kwa kuchaguliwa!! Na Serikali siyo wawakilishi wa Bunge! Bunge ni wawakilishi wa watu na ni Bunge linalotunga sheria ambazo serikali inafuata!! Ni Bunge pekee lenye uwezo wa kumuita mtu yeyote binafsi au kama kampuni na kutaka wapewe maelezo yoyote ambayo ni kwa maslahi ya Taifa.

Kama ni kweli Bunge letu halina uwezo wa kuhoji mikataba ya serikali na kuiitaka mikataba hiyo iletwe na itazamwe na Wabunge wenyewe basi Bunge letu lina udhaifu mkubwa wa kisheria na kiutendaji. Hebu fikiri kwa dakika chache kuwa kitengo, au wakala fulani wa serikali anaingia mkataba na kampuni fulani kufanya jambo fulani, mkataba huo kwa sababu fulani unazua utata, basi Kamati ya Bunge (kwa niaba ya Bunge) wanataka kuona na kuusoma mkataba huo halafu kiongozi wa serikali anawaambia “It is none of your business!” – Haikuhusu! Ndugu zangu, kama hilo si tusi la rejareja basi ni tusi la nguoni!!

Ninachosema ni hivi:

a. Bunge kwa kutumia huu mfano huu wa KADCO lidai nafasi yake ya kisheria kwa kulazimisha mkataba huo uletwe kwa Wabunge na uangaliwe! Vinginevyo wakikubali kipengele hicho kisimame kama alivyodai Dr. Daftati basi watarajie mikataba mingi itawekwa kipengele kama hicho ili kuzuia vyombo vya serikali kupata nafasi ya kuangalia mikataba hiyo. Sijali hasa kama watu binafsi wakikatazwa kuangalia lakini ikifikia kuwa hata Wawakilishi wa wananchi wananyimwa fursa ya kuangalia mikataba na hivyo kulinda maslahi ya wananchi basi Bunge letu ni butu na lililobweteka!

b. Kama hakuna sheria inayoipa nguvu Bunge kuangalia mkataba wowote unaoingiwa na mtu, chombo, idara, wakala n.k chochote cha Kitanzania iwe ya serikali, au binafsi basi sheria hiyo itungwe mara moja ili kulinda maslahi ya Taifa, mali za Taifa na haki za wananchi! Katika sheria hiyo (kama haipo) ni lazima iwekwe wazi kuwa hakuna mkataba wowote utakoingiwa chombo chochote cha kitanzania (vya umma au binafsi) katika ardhi ya Tanzania au utakavyohusisha vyombo tanzu vyake ndani au nje ya Tanzania vitakavyokataza moja kwa moja au kwa kuashiria (directly or implicitly) kuwa Bunge halina uwezo wa kuiangalia mikataba hiyo kwa sehemu au yote (partially or totally). Mkataba wowote utakaokuwa na kipengele hicho mkataba huo utakuwa umepotoka na umetenguka (null and void).

c. Bunge lipewe nguvu ya kuwaita wale wote wanaoiingiza serikali katika mikataba wakati wa majadiliano na kuwahoji kwanini walikubali vipengele fulani viingizwe kwenye mikataba hiyo. Watu wanaoshiriki katika majadiliano ya mikataba kwa upande wa serikali wawe wanaweza kuitwa kutoa maelezo chini ya kiapo ya kwanini waliingia mikataba fulani. Na kama watu hao wataonekana kufanya hivyo kwa kujinufaisha au kuidhulumu serikali, basi Mwanasheria Mkuu apewe mamlaka ya kuwafungulia mashtaka ya kuihujumu serikali. Lengo liwe ni kuhakikisha kuwa wale wote wanaoaminiwa na serikali kufanya majadiliano basi wanafanya hivyo wakiwa na lengo moja na moja tu nalo ni kuhakikisha kuwa Mikataba inanufaisha kwa kiwango cha juu zaidi (maximum level) serikali au kitengo husika bila kunyima kwa haki faida kwa upande wa pili wa mkataba kwa kiwango cha juu wanachoweza kupata.

Hivyo basi, wabunge wetu walirudie jambo hili (la KADCO na KIA) na kulazimisha makampuni na wizara kuuleta mkataba huo kwao ama sivyo wanaanza kujenga mazoea mabaya (bad precedent). Wabunge wetu licha ya vyama vyao wasikubali kuburuzwa na serikali kwa kupewa maelezo dhaifu yasiyo na kichwa wala mguu yanayotolewa na mawaziri au manaibu waziri wanapojibu maswali Bungeni!!! Ama sivyo, iko siku badala ya kupigwa bong’oa tutajikuta tumepigwa dafrau!!!
 
Mimi sikutegemea mambo mapya baada ya BMW kwa JK .Leo hii majibu wakati yanatolewa rafiki yake mkubwa JK ni mwanasheria Mkuu ambaye anaingia Bungeni alikuwepo na hata hakuweza kufungua mdomo wake kusa hihisha anaogopa tonge lake ambalo kapewa majuzi .Iko safari ndefu sana .Kama Zitto kafungua kinywa kaitwa muongo na kutishwa leo hii Serikali ya JK ambaye ina magazeti yote na hata waandishi wanashindwa kuandika mambo ya maana ila ushabiki wanaweza kusimamia swala zito kama hili ??
Iko kazi sana na yangu Macho .Sikutegemea waziri wa JK aseme hayo wakati Rais anasema mikataba itaangaliwa upya na kwa uwazi na hili inakuwaje ???
 
Mwanakijiji:
Najua una uchungu sana na nchi yako. Hata hivyo nakupa pole maana Tanzania haiwezi kuendelea hata siku moja. Maisha ya neema yatakuwa kwenu wachache ambao mko nje ya nchi, viongozi na matajiri wa kigeni. Sisi wakulima wa vijijini haiwezekani kuendelea hata kidogo. Hotuba ya mheshimiwa huyo ina changamoto nyingi ambazo kwa vichwa vinavyofikiri vingeyafanyia kazi lakini kwa ninavyoelewa haiwezekani. Tule ugali na kusubiri kufa tu. Magazeti ya kitanzania kwa kulinda mkate wao, wamechukua kipengele kimoja tu na kukipa kichwa cha udhaifu.

Mtu wa kupiga kelele Tanzania hakuna, upinzani ni hoi na magazeti yote hakuna yanayoona mbele zaidi ya mkate wao wa kila siku. Mchungaji Mtikila anjitahidi sana kutoa hoja ila naye yuko pekee. Kama wapinzani wangejua wangewekeza nguvu kubwa zaidi kupata wabunge wengi ili bunge liwe moto moto kama mabunge ya nchi zingine. Washauri wapinzani wakazanie zaidi kwenye bunge maana huko ndiko kwenye nafasi ya kuibana na kuiuliza serikali. Unaonaje kama bunge lingekuwa na watu kama Mtikila, Mbowe na Mrema????.

Kama kweli wewe una uchungu na siasa za nyumbani rudi uanzishe redio yako, gazeti na pia gombea ubunge ili uwe na nafasi ya kusema kwa sauti kubwa zaidi. Ingawa hata wewe baada ya kupewa shangingi la million 40 sidhani kama kelele ulizo nazo zinaweza kuwa kubwa kama unavyopiga sasa. Hilo ndio tatizo kubwa. Kila mmoja anataka kula tu.
Ndio maana nasema Tanzania na nchi zote za Africa haiwezekani hata kidogo kuendelea - HAIWEZEKANI.
 
Mzee wa Busara, wote hatuwezi kukata tamaa. Nilisema huko nyuma kuwa "Taifa la watu Duni linajengwaje" Maana yangu hasa ilikuwa ni vigumu (kama siyo haiwezekani kabisa) kujenga Taifa la watu walioakata tamaa!! Ni kwa sababu hiyo nilishaapa huko nyuma kwa mizimu ya kikwetu kuwa sitakaa kimya na nitaendelea kupaza sauti yangu kama Yohana Mbatizaji kuwatangazia watu kuwa wakati wa "toba" ni sasa kwani "shoka limeshainuliwa dhidi ya shina!"
 
Mzeewabusara, wakati mwingine naingiwa na shaka kidogo maana unaweza kupiga kelele sana watu wakaamua kukunyamazisha!!! Maana nasikia kuna umafia mafia wa aina fulani unaendelea Tanzania kulinda maslahi ya kikundi fulani cha watu!!!
 
Mze Mwanakijiji: Hoja zako nzito. Hata hivyo nasita kukubaliana na wewe kuhusu wapinzani kukaa kimya. Si wewe mwenyewe umesema kuwa Zitto ndo alitoa hiyo hoja-sasa Zitto si mpinzani ulitaka afanye nini tena? Halafu Zitto huyohuyo alitoa hotuba kali lakini vyombo vya habari vya Tanzania, Mkandara, Mzee Es et al wakaamua kuangalia kipengele kimoja tu, na hotuba nzima ikapotoshwa. Kwa maoni yangu wapunge wa upinzani kwa kuzingatia uchache wao bungeni wanafanya kazi kubwa na kuna wakati inabidi wapongezwe kama njia ya kuwatia moyo.

Kuhusu, vyombo vya habari, naam, nimerudi jana Bongo na nitakuwa hapa kwa utafiti kwa miezi mitatu. Leo nimejaribu kudodoza magazeti; mpaka sasa niandikapo hii post sijaamua ninunue gazeti gani! Kila gazeti limesheeni, pamoja na Tanzania Daima ambayo imesifiwa kuwa na mlengo tofauti, habari za kumtukuza JK na serikali yake. Hamna hoja mpya. Kwa hiyo ukinunua gazeti moja huna haja ya lingine. Na kama unatafuta kitu gani kinaendelea ndani ya nchi zaidi ya sifa kwa serikali itakuwa vigumu kupata.
 
Mwanasiasa,

Umeshakaa majuu mzee, sasa si unaelewa kuwa article ikiwa na sentesi moja ya uongo na uzushi, basi yote inakuwa ni nonesense! Kwenye dunia hii ya sayansi huwezi tena ukarusha mawe bila ushahidi bro,

kibinadamu nmekubaliana na waziri kivuli baada ya maelezo yake kule kumekucha, kuwa spirit aliyokuwa nayo wakati wa kuyatoa maelezo ilikuwa ni njema ila tatizo alisema uongo, tena uzushi NO! hayo ndiyo yanawaponza CUF kila siku, sasa tujifunze kutorudia makosa yale yale kila siku!

Halafu pongezi kwa Chadema kuwa midomoni mwa wancnhi wengi na wanaforum hii, ambao matokeo ya uchaguzi uliopita yanaonyesha kuwa sio wapiga kura!
 
Mzee ES, samahani sijaelewa unachosema ni kuwa unakubaliana na hoja ya Dr. Maua kuwa Wabunge "haiwahusu" kuingalia hii mikataba kwa vile Bunge halihusiki moja kwa moja na utekelezaji wa mkataba huo?
 
Wanabodi,
Hii ndiyo hasara ya kutokuwa na wabunge wengi wa Upinzani bungeni. Mtu mmoja kama Zitto na ujasiri wake ataonekana kama mbabaishaji tu na kuzomewa juu kwa sababu hana support. Kiti cha urais ni kimoja tu na nafasi ya wapinzani kuweza kushika kiti hicho ni asilimia 2 hali Ubunge unavuta hadi aslimia 50% kwa wapinzani. Nakumbuka mama Mongela na sifa zote za kupambwa sana aliondoka na asilimia 52 tu, hatufahamu ngapi ziliibiwa. lakini kama wap[inzani wataweka nguvu yote ktk Wabunge na kupata viti hata nusu.. Huko bungeni kungewaka moto.

Mwanasiasa,
Hakuna mtu anayesema Zitto sii jasiri, hata Mbowe pia jasiri, mwanamme wa shoka hasa, jembe - jembe very strong na anajua kuzungumza vizuri sana. Tatizo lake ni pale alipoweka nguvu yake, ni sawa na mcheza mpira ambaye anataka kufunga goli peke yake hali kuna wachezaji wengine kumi uwanjani. Kama umewahi kucheza mpira nadhani utakubaliana na mimi kwamba sii rahisi kwa mchezaji uwanjani kugundua dhamira ya mcheza mwenzie isipokuwa watazamaji walioko nje huona zaidi mbali na hiyo formation ya kutafuta goli. Mara nyingi washabiki hawatakubali kumkosoa star wao anapojaribu kufunga yeye badala ya kuugawa mpira kwa yule aliyekuwa wazi kufunga goli.

Unajua kwa nini? huwa hawana imani na huyo mchezaji mwingine na kibaya zaidi kama ikitokea akapewa pasi kisha akashindwa kufunga... Loooh, vita yake haitakwisha. Lakini basi kwa mjuzi wa mpira ataweza kutambua kipaji na uwezo wa mcheza kulingana na nafasi yake. Mpira utachezwa kila kona sii lazima star awe mbele ya kila nafasi ya kupata goli ama ushindi. Na hata kama hakufunga yeye bado sifa zitakuwepo na yeye ataendelea kuwa star. lakni hawa washabiki siku zote wapo radhi star wao akose goli lakini sii mchezaji mwingine. Je, sifa ua ushindi hunoga pale star anapofunga yeye kuliko kushinda mtu mwingine?

Nachouliza mimi ikiwa hamna imani na baadhi ya wachezaji kwa nini mnawapa nafasi ktk timu ya kwanza?. Utakubaliana nami kwamba mpira hachezi mtu mmoja na Zitto katuonyesha kwamba yeye pia ni mcheza na anaweza kufunga magoli.

Natumai lugha hii sio nzito!
 
Hivi hawa wabunge wetu wanafikiria nini hasa kwa UMOJA wao kuhusu eti mikataba inayowahusu wananchi kuwa siri hata kwao. ARE THESE MPS REALLY RESPONSIBLE TO THEIR PEOPLE?? i doubt!!!

Ndg wabunge kama mnasoma hii forum "SHAME ON YOU" how the hell could someone like Ole Naiko/Rubambe be on Top of "ALL OF YOU MPS"?,

Inauma sana, kwani nafahamu kuna watanzania wanafanya kazi nchi za watu hu-review so many Heads of Agreements kwa manufaa ya mataifa hayo wakati nyumbani wataalamu wetu huwa, ni mstari as "SUICIDE BOMBERS" ......yes they are(Ole Naiko, Rubambe et al) suicide bombers kwa sababu sisi wananchi ndio huathirika at the end of the day.

Mwalimu JKN alisema, tuikomboe nchi yetu toka kwenye umasikini kwa kutumia juhudi na maarifa na rasilimali tulizonazo...."Play your party.....it can be done"
 
Wabunge ndio wawakilishi wetu. Serikali haiwezi kuwawakilisha wabunge. Wabunge ndio wanatunga sheria za nchi, kwa niaba yetu. Hakuwezi kuwa na mkataba halali unaoihusu serikali ambao unalikataza Bunge lisiuangalie. Kama inadaiwa upo, basi Bunge jasiri lingetunga sheria hapo hapo ya kuliruhusu kuangalia huo mkataba.

Kinachokosekana bungeni kwetu ni ujasiri. Kuna mawazo ya kukanyagwa vile vile. Juzi juzi Spika alimtoa nje Mheshimiwa Amina Chifupa kwa kuvaa kofia. Sheria aliyotumia Spika ni ya miaka kabla ya uhuru, na inasema ukivaa kofia bungeni shurti uvae vile vile gloves. Mheshimiwa Chifupa alikuwa amevaa kofia maridadi sana, lakni alisahau kuvaa gloves (nyeupe).

Sasa bunge linalofungwa na sheria kama hizi ni bunge kweli? Bunge lenye majasiri litatunga sheria za kufutilia mbali upuuzi wowote utakaojitokeza. Mwalimu angekuwa hai angecheka sana kusikia Sitta wake amemfukuza kijana bungeni kwa kutovaa gloves (nyeupe) pamoja na kofia yake.

Augustine Moshi
 
Ama kweli wadanganyika tuna taabu?
Looh hii mpya na kubwa kuliko zote!
Sijawahi kusikia kabisa kwamba mtu akivaa kofia LAZIMA avae pia gloves nyeupe.
Huu uzungu weusi umetoka wapi jamani, hata spika wetu kauvalia suti?(njuga). Ama kweli safari ndefu. Bunge ni sehemu ya kujadili maswala ya nchi na sio sehemu ya kutoana nishai kwa mavazi hasa vitu kama gloves.
Hivi, gloves zinahusiana vipi hasa na kofia kwa kina mama?
 
Mzee Mwanakijiji said:
Hata hivyo Naibu Waziri wa Miundo Mbinu Dr. Maua Daftari alisema kuwa kipengele cha 30.4 cha mkataba huo “kinaifunga serikali na mbia wake, Kilimanjaro Airports Development Company (KADCO), kutoa habari kwa mtu yeyote ambaye si mhusika wa moja kwa moja kwenye utekelezaji wa mkataba huo.” Kwa mujibu wa Dr. Daftari na ilivyonukuliwa na gazeti mojawapo nchini “wabunge si wahusika wa moja kwa moja na mkataba huo, badala yake serikali itaendelea kuwawakilisha

Mzee Mwanakijiji;Naomba kuelimishwa hapa,vipengele vya mikataba huwa viko juu ya sheria?Je mikataba haitakiwi iwe chini ya sheria?Wabunge hawahusiki na sheria?Ama sheria na mikataba havihusiani?
Ningeshukuru.
 
Hili swali linaniumiza sana kichwani, Je kama Mbunge wa chama tawala au upinzani na mkataba uko ndani ya Jimbo lako, Swali:je kuna kipengele chochote kinachomzuia mbunge kutoka hapo jimboni kujua nikipi wabia wameruhusiwa na Serikali kufanya na kipi wamezuiliwa kufanya ndani ya jimbo lake? kwani hapa waziri kasema kipengele cha 30.4 cha mkataba huo "kinaifunga serikali na mbia wake. Je kama mbia anafanya mambo tofauti na Mbunge hajui ninini mbia ameruhusiwa kufanya atawateteaje wananchi?
 
serikali imechukua hisa zote za KADCO. Tunamshukuru huyu kijana kwa kufanya kazi nzuri ya kuibua hoja hii ya kilimanjaro na sasa uwanja unarudi kwetu.

Tatizo linakuja je hisa hizo wamenunua kwa shilingi ngapi?
 
serikali imechukua hisa zote za KADCO. Tunamshukuru huyu kijana kwa kufanya kazi nzuri ya kuibua hoja hii ya kilimanjaro na sasa uwanja unarudi kwetu.

Tatizo linakuja je hisa hizo wamenunua kwa shilingi ngapi?

kati ya mambo yote niliyoyasimamia katika miaka minne iliyopita ni mawili ambayo nimepoteza na yananiuma:

a. La Amina Chifupa
b. La vijana wetu kule Ukraine

kwenye mengine yote my record stand for itself and against anybody's. I'm grateful for all who made it possible.
 
Mzee Mwanakijiji, essence ya mkataba ni its binding nature vinginevyo ni kuvunja mkataba. Mikataba mingi ina kipengele konyesha mkataba huo ni siri, kama kipengele hicho kipo, then mkataba huo ni siri ya wahusika, hata bungeni ni hailetwi, udhalilishaji wa bunge hapa uko wapi?.

Hata rais wa nchi, hana mamlaka ya kuingilia mikataba sembuse Bunge?.

Mikataba yote iko governed na the law of contract, hivyo inategemea drafting wameweka vipengele gani, mwanasheria mkuu ana kila uwezo kulazimisha mikataba yote mikuu, yenye maslahi kwa taifa na kuhusu rasilimali za taifa, lazima iridhiwe na Bunge, kama hili halijafanyika ni weakness on part of government, utekelezaji ni maters of law no politics, bunge limedhalilishwa wapi?.

Nliwahi sema kule nyuma, hata mkataba wa Vithlani kwenye deal ya rada ni mkataba safi, hauna makosa ya kisheria hata rais hawezi fanya chochote.

Nikiokota chungwa la thamani ya Shilingi Mia, nikakuambia hili ni chungwa nimelichukua toka dinner table ya Obama, hivyo naliuza milioni 100!. Ukikubali, its a deal and its over, hata ukuja kugundua kumbe sio kweli, hakuna any mis representation kwasababu umenunua chungwa uliloliona mwenyewe kwa macho, ile Obama ni just sales techniques kama 'the best'.

Mikataba ni private maters ndio maana hata mikataba mingi ya kiserikali, inafanyiwa attestation na mawakili binafsi na ndiko Mkono alipoibukia enzi za Mwalimu.

Haya ni masuala ya kisheria na sio politiki.

Pasco
 
Back
Top Bottom