Kkimondoa
JF-Expert Member
- May 31, 2014
- 4,453
- 4,933
Bunge ni chombo ambacho kama kingekuwa kinafanya kazi yake ipasavyo hakika Tanzania ingekuwa mbali sana kwa sasa. Lakin Bunge la Tanzania ni miongoni mwa mabunge ya hovyo na hasara kwa Taifa, halina msaada wala mchango wowote ule kwa taifa hili.
Bunge linatia hasara Serikali kila mwaka. Bunge linakula posho bila michango chanya kwa taifa zaidi ya mipasho na malumbano ya kijinga. Kwa Tanzania bunge ni chombo cha kula posho tu na kupiga meza hakuna ambacho bunge linaweza kufanya chenye tija kwa taifa hili.
Bunge linaamuliwa mambo ya kufanya, Bunge haliwezi kujisimamia katika maamuzi yake lenyewe. Bunge halieleweki lina simamia nini, lipo kama ishara ya Bunge katika taifa. Maamuzi ya Bunge yanaweza kupindishwa hata na Mkuu wa Wilaya au Mkoa na ikiwezekana hata Mwenyekiti wa chama wilaya anaweza kulitunishia misuli Bunge.
Bunge la hivi la nini wakati halina faida kwenye nchi hata kwa 10%? Bora livunjwe pesa za posho na marupurupu mengine ziende kupeleka huduma kwa wananchi maana halina faida na halijui majukumu ya Bunge.
Si spika wa Bunge wala mwenyekiti wa Bunge, si Naibu wala Katibu na wabunge wote wanaojua umuhimu wa Bunge kuwepo.
Nasema hawajui tena hawajui wapo pale kula posho maana bado matatizo katika jamii yapo kwa kiwango kile kile kila mwaka mf.
1. Njia ni za msimu wa kiangazi tu masika hazipitiki na ni tangu uhuru
2. Maji bado shida sehemu kubwa ya nchi tangu uhuru
3. Umeme bado ni shida kwa wiki mnautumia siku tatu au nne tena kwa masaa
4. Huduma za afya na dawa bado shida palepale tangu uhuru
5. Elimu ndio kabisa ipo mahututi
Bunge linasema hivi na kuamua hivi lakini Serikali inafanya hivi na kuamua vile. Bunge hili la nini na linatumia pesa nyingi kujiendesha tena bila faida? Bunge lifutwe na lisiwepo kabisa, halina faida bunge hili.
Nawasilisha
Bunge linatia hasara Serikali kila mwaka. Bunge linakula posho bila michango chanya kwa taifa zaidi ya mipasho na malumbano ya kijinga. Kwa Tanzania bunge ni chombo cha kula posho tu na kupiga meza hakuna ambacho bunge linaweza kufanya chenye tija kwa taifa hili.
Bunge linaamuliwa mambo ya kufanya, Bunge haliwezi kujisimamia katika maamuzi yake lenyewe. Bunge halieleweki lina simamia nini, lipo kama ishara ya Bunge katika taifa. Maamuzi ya Bunge yanaweza kupindishwa hata na Mkuu wa Wilaya au Mkoa na ikiwezekana hata Mwenyekiti wa chama wilaya anaweza kulitunishia misuli Bunge.
Bunge la hivi la nini wakati halina faida kwenye nchi hata kwa 10%? Bora livunjwe pesa za posho na marupurupu mengine ziende kupeleka huduma kwa wananchi maana halina faida na halijui majukumu ya Bunge.
Si spika wa Bunge wala mwenyekiti wa Bunge, si Naibu wala Katibu na wabunge wote wanaojua umuhimu wa Bunge kuwepo.
Nasema hawajui tena hawajui wapo pale kula posho maana bado matatizo katika jamii yapo kwa kiwango kile kile kila mwaka mf.
1. Njia ni za msimu wa kiangazi tu masika hazipitiki na ni tangu uhuru
2. Maji bado shida sehemu kubwa ya nchi tangu uhuru
3. Umeme bado ni shida kwa wiki mnautumia siku tatu au nne tena kwa masaa
4. Huduma za afya na dawa bado shida palepale tangu uhuru
5. Elimu ndio kabisa ipo mahututi
Bunge linasema hivi na kuamua hivi lakini Serikali inafanya hivi na kuamua vile. Bunge hili la nini na linatumia pesa nyingi kujiendesha tena bila faida? Bunge lifutwe na lisiwepo kabisa, halina faida bunge hili.
Nawasilisha