Mkoba wa Mama
JF-Expert Member
- May 5, 2021
- 280
- 173
Kama nitakua nimekosea mtanielewesha, maana ninachofahamu mimi ni kwamba; Bunge linapelekewa Mswada wa sheria, kisha wabunge wanajadili na baadae kupitisha Mswada ili ukasainiwe na Rais, na sio kwamba Bunge ndio linauandaa huo Mswada wa sheria.
Kwa sababu huwa naona Mswada hupelekwa Bungeni, aidha na Mwanasheria Mkuu wa Serikali au Mawaziri wa Wizara husika.
Kwa maana hiyo; kwanini huwa tunasema Bunge linatunga sheria? Wakati kazi yake ni kujadili tu na kufanya marekebisho madogo, ambayo hata hayo marekebisho haliyafanyi Bunge, bali hupendekeza tu yafanyike?
Kwanini sasa tusitumie maneno; BUNGE HUPITISHA MSWADA WA SHERIA, BADALA YA BUNGE HUTUNGA SHERIA?
Kwa sababu huwa naona Mswada hupelekwa Bungeni, aidha na Mwanasheria Mkuu wa Serikali au Mawaziri wa Wizara husika.
Kwa maana hiyo; kwanini huwa tunasema Bunge linatunga sheria? Wakati kazi yake ni kujadili tu na kufanya marekebisho madogo, ambayo hata hayo marekebisho haliyafanyi Bunge, bali hupendekeza tu yafanyike?
Kwanini sasa tusitumie maneno; BUNGE HUPITISHA MSWADA WA SHERIA, BADALA YA BUNGE HUTUNGA SHERIA?