Grader
JF-Expert Member
- Feb 23, 2009
- 445
- 65
Kilichofanya niweke bandiko ni mambo mawili, kwanza kueleza tukio husika, pili kuna mleta mada anayejiita Grader kapost uongo kutokana na hiki ntakachoandika, amemsingizia huyo marehemu Panya road azikwa kifahari Buguruni kisiwani, pili amesema Buruguni ni kitongoji chenye kila aina ya laana! Kweli? Hivi mtu humjui hata jina, umri wake wala maisha yake unaazaje kumkashifu mtu.
Then unakashifu eneo husika unadai kuna kila aina ya ufedhuli na vijana wake wamepotoka, ina mana wakazi wa Buguruni wote hatuna maana? Au mwenzetu anaishi peponi?
Stori kamil ilikuaa hivi; Jumapili ya tarehe 31 mwezi Mei mtaani kulikuwa na sherehe, kuna binti anaitwa Zena alikuwa anaolewa, huyo Zena na marehemu walikuwa mtu na mjomba wake na ilipangwa tarehe 5 Ijumaa, marehemu arudi ili aje kufungishwa ndoa.
Hivi panya road anaweza kusubiriwa toka Sauzi aje bongo kufungisha ndoa? Tena anakuja kwa ndege? Bahati mbaya Jumatatu bongo wanamfanyia kitchen party Zena kule mjomba wake anapigwa risasi akiwa supermaket.
Baada ya kupewa ripoti Jumanne asubuhi walilia na sherehe ikawa basi!
Itaendelea part 2
=> Part 2
Kiukwel ilipangwa sherehe bab kubwa ifanyike pale mtaani. Sherehe ilipangwa ifanyike wiki nzima kuanzia tar 31 May had tar 7 June. Jumapili paliwekwa ngoma, Jumatatu usiku ikafanyika kitchen party lakini kwa bahati mbaya tulipokea taarifa zilizostua mioyo ya wengi pale tulipoambiwa kaka yao mkubwa anayeitwa Hamis ametutoka duniani.
Alifariki kwa kupigwa risasi akiwa supermarket nchin Afrika Kusini, taarifa ambayo ilizima chereko pale mtaani na kukatisha ratiba ya sherehe iliyosalia ambayo ilitakiwa Jumatano ipigwe baikoko, Alhamis upigwe mnanda, Ijumaa ipigwe taarab live band kutoka kwa mashauzi Classic na Jumamosi wamalizie na rusha roho kisha Jumapili waende ukumbini kwa ajili ya harusi lakini mambo hayakuwa hivyo sherehe yageuka msiba!! unajua chanzo cha marehemu kuuawa?
Ungana nami sehemu ya tatu.
Chanzo: Mimi ni jirani yao.
Nafikiri haujui unachokitetea, Mimi ni mzoefu sana kwa shughuli za uandishi wa habari za uchunguzi zaidi ya miaka 10 sasa, nilikuwa nisafiri kuelekea Dodoma siku ya jumatatu sijaenda kwani niliamua kubaki ili nikamilishe report hii ya kiuchunguzi. Ukweli unayejiita Dr Aluta huifahamu Buguruni na uhalifu unaofanywa(uvunjwaji wa sheria na maadili). Nimebahatika kufanya mahojiano ya ana kwa ana na ndugu,jamaa na rafiki wa Hamisi. Pia nimechunguza maeneo yote korofi na kufanya mahojiano ya kina na wahusika na kuridhika pasipo shaka Buguruni ni sehemu maarufu kwa uhalifu kama wizi,ujambazi,ukabaji,chabo,madawa ya kulevya,bangi,utumiaji na uuzaji wa pombe haramu,ukahaba,chuma ulete n.k. Mimi sijasimuliwa na mtu habari hiyo bali nimeifuatilia mpaka mwisho wake. Kwa kweli wanaokaa Buguruni chukueni tahadhali .