Bugando na ulanguzi wa dawa

johnmashilatu

JF-Expert Member
Sep 16, 2010
718
703
Wadau.
Nimeandika mara tatu hapa juu ya mambo yasiyofaa ambayo yanaendelea katika hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyoko jijini Mwanza, ingawa hoja hizo hazijapata majibu na pia kwamba sitarajii kupata majibu, nafikiri kuna haja ya kuendelea kueleza uozo huo ili tu uweze kufahamika kwa wengine.
Alhamisi ya wiki iliyopita, mgonjwa wangu aliyelazwa katika moja ya wadi iliyoko ghorofa ya nane, aliandikiwa aina mbili za dawa: Neurobion na Erythromycin( sina uhakika kama nimeziadika ipasavyo), lakini aliagizwa kwenda kununua, kwa kuwa hazikuwepo hospitalini hapo!
Ndani ya Hospitali kuna duka la dawa ( Pharmacy) ambapo ukikosa dawa ndani unakwenda nje na kukuta dawa unazohitaji! Naambiwa kuwa duka hili pia ni mali ya Hospitali> hospitali hiiyo isiyokuwa na dawa katika eneo moja inayo dawa hiyo hiyo, katika kitengo kingine!
Labda hiyo sio shida, Ndani ya duka hilo nilikuwakuta vija a wawili, wakiume na kike, ambapo dada aliyekuwa ndani baada ya kuona karatasi yangu ya dawa aliandika kuwa Dozi ya Erythromycin, inauzwa shilingi 9000, huku Neurobion ikiuzwa kwa shilingi 14000. Jumla kuu inatakiwa shilingi elfu 23.
Wakati natafakari juu ya gharama hiyo, mtu mmoja aliyekuwa jirani, aliniambia kuwa gharama za dawa katika duka hilo ni kubwa kwa zaidi ya asilimia 100 kuliko maduka ya mjini.
Nilikwenda Kayonza Pharmacy ambako dawa zote ambili nilizoambiwa kuwa Bugando zinauzwa shilingi 23000, Kayonza nilizipata kwa shilingi 4000!.
Mambo ni mengi lakini hiyo ndio Bugando
 
Duuuh! hao kweli walikuwa wanakukomoa.nina uhakika hata ukienda USA huwezi kupata kwa bei hiyo
 
Wadau.
Nimeandika mara tatu hapa juu ya mambo yasiyofaa ambayo yanaendelea katika hospitali ya Rufaa ya Bugando iliyoko jijini Mwanza, ingawa hoja hizo hazijapata majibu na pia kwamba sitarajii kupata majibu, nafikiri kuna haja ya kuendelea kueleza uozo huo ili tu uweze kufahamika kwa wengine.
Alhamisi ya wiki iliyopita, mgonjwa wangu aliyelazwa katika moja ya wadi iliyoko ghorofa ya nane, aliandikiwa aina mbili za dawa: Neurobion na Erythromycin( sina uhakika kama nimeziadika ipasavyo), lakini aliagizwa kwenda kununua, kwa kuwa hazikuwepo hospitalini hapo!
Ndani ya Hospitali kuna duka la dawa ( Pharmacy) ambapo ukikosa dawa ndani unakwenda nje na kukuta dawa unazohitaji! Naambiwa kuwa duka hili pia ni mali ya Hospitali> hospitali hiiyo isiyokuwa na dawa katika eneo moja inayo dawa hiyo hiyo, katika kitengo kingine!
Labda hiyo sio shida, Ndani ya duka hilo nilikuwakuta vija a wawili, wakiume na kike, ambapo dada aliyekuwa ndani baada ya kuona karatasi yangu ya dawa aliandika kuwa Dozi ya Erythromycin, inauzwa shilingi 9000, huku Neurobion ikiuzwa kwa shilingi 14000. Jumla kuu inatakiwa shilingi elfu 23.
Wakati natafakari juu ya gharama hiyo, mtu mmoja aliyekuwa jirani, aliniambia kuwa gharama za dawa katika duka hilo ni kubwa kwa zaidi ya asilimia 100 kuliko maduka ya mjini.
Nilikwenda Kayonza Pharmacy ambako dawa zote ambili nilizoambiwa kuwa Bugando zinauzwa shilingi 23000, Kayonza nilizipata kwa shilingi 4000!.
Mambo ni mengi lakini hiyo ndio Bugando

Huo ni wizi wa mchana.
 
Pole sana,
Kwa kawaida hospitali za uma zinakuwa na in-hospital pharmacy (zile za ndani) ambazo zinahudumia wagonjwa wa ndani na nje. Hizi pharmacy za ndani zinategemea asilimia kubwa dawa kutoka msd. Dawa hz zinakuwa bei nafuu kwa ajili ya wagonjwa wa kawaida (yani gradeIII, II, msamaha, n.k.) Na kwa bahat mbaya sana zinafrequent outstock. Lengo la kuwepo na pharm ya nje ni kuhakikisha upatikanaji wa dawa kwa wagojwa wa Bima na ikumbukwe kwamba bima wana bei zao za dawa (depending on whch type of bima) ndo maana bei kidogo inakuwa juu kulingana na viwango walivyopanga. Hii haitegemei msd wala ruzuku na huwezi kuuza dawa hii kwa 4000 kwa mtu wa kawaida na dawa hyo hyo tena uuze 7000 kwa mtu mwingine kwenye duka hilo hilo pia kwa wale affordables wa gradeI,II or private na VIPs they can't rely on drugs from msd. Nakushauri kama hauna bima uende pharm za binafsi utapata kwa bei nzuri.
 
dawa ni kuacha kuzinunua kwenye hilo duka na kwenda kununua sehemu nyingine.
 
Pole sana ndugu kwa yaliyokukuta. Nafikiri vyombo husika vya kuregulate upatikanaji, matumizi pamoja na bei za dawa vinahitaji kufanya kazi yake. Pamoja na kuwepo kwa soko huria. Mara nyingi ultimate consumer ndiye amekuwa akiumia kutokana na bei. Ila pia bei za dawa haziko uniform inategemea kama ni brand gani uliyouziwa hapo BMC kwa sababu kuna dawa zinazotengenezwa Tz, Kenya, France, UK au US. Bei zatofautiana na kwa ufanyaji kazi so kama the same brand uliipata Kayonza that is too bad. Ila ujumbe kwa regulators wawasaidie wananchi haswa bei na ubora kwani kuna dawa nyingi sana zenye question marks kuhusu ubora.
 
unajua mtu kabla ya kusema unaibiwa jiulize kwanza je iyo bidhaa kwa bei izo 2 tofauti zina ubora gani?zimetengenezwa wapi?je expiring date zake je?mana unaweza uziwa kitu wewe ukijau unasave kumbe unauziwa takataka tena.pili dawa kalibia zote za hospitali ni ruzuku toka serikalini thr MSD ambako nako stock-out ni balaa yani huwezi kuta dawa hopsitalini ila utazikuta maduka ya nje napo bei lazima iwe juu mana nao wanafanya biashara kwani si wamezinunua?

binafsi nilishawai kutibiwa hospitali moja dar aiseee nilikutana na kisiki cha nesi mmoja ivi na iyo ni hospitali nilokua naitegemea kwa matibabu,nilichofanya badala ya kulalamika tu na kuandika facebook....nilichukua hatua ya kwenda kuonana uso kwa uso na utawala wa hospitali iyo na kueleza kinaga-ubaga uzembe wa manesi na lugha tata zinazotolewa (ofcourse nilionana na Mkurugenzi wa huduma za hospitali na akaja na matron mkuu) niliwaeleza izo madhila nilizopata na niliyoona muda wote nilolazwa hapo.so mtoa mada watu kama sie wenye kuchukizwa na vitendo vya wahudumu katika izi sehemu zinazotoa huduma inabidi tuwe wa kwanza kupeleka matendo hayo kwa uongozi kwani milango iko wazi bila hiyana wala kubagua,nenda toa maelezo na kama umeshika ushahidi apo ndo patamu mwana unashsusha details adi wanakubali na hii itawasaidia sana utawala wa eneo husika kwani wao sio miungu waweze jua kila liendalo humo.kumbuka wabongo wengi sijui tuna nini tukiwa na shida zetu binafsi tunazihamishia wa wagonjwa au watu wanaokuja kupata huduma.
wewe nenda apo BMC kuna ofisi toa maelezo au kama una ushahidi mwanwane kamwage mwaaaaa na naamini yatasaidia kupambana na matatizo haya katika eneo lao.
 
Back
Top Bottom