Kama unapenda kujifunza na kujielimisha, hii itakusaidia. Crimea imekaa kimkakati zaidi yaani kama wamagharibi walivyolazimisha muungano wa Tanganyika na Zanzibar!Vipi kuhusu uvamizi wa Crimea 2014?
Kujiunga NATO ni kufanya nini?Ukraine ilimkaribisha US lini?
Ukraine wenyewe huwezo huo wanao, hela ndio hawanaMarekani pamoja na kumchukia sana Urusi hawezi kamwe kuwawezesha ukraine kuwa na nyuklia kwasababu sio mjinga!
Sent from my SM-A135F using JamiiForums mobile app
Jibu basi kwanza ndio uulize swali.Lini Marekani au NATO walitaka kuweka makombora yao Ukraine? Kuna makombora ya Marekani huko Finland, Uturuki, Romania, Bulgaria, na Estonia?
Urusi walikubali kuondoka East Germany ambayo haikuwa eneo lao kwa kuanzia kwa makubaliano gani?
Ukimtoa Leonid Kravichuk ambaye ndo raisi wa kwanza 1991 aliyemfatia ni Leornid Kuchuma 1994 ambaye alitawala mpaka 2004 huyo unaemsema kuwa ni pro-russia viktor Yanukovych alikuwa ni prime minister kwenye serikali yake na mpaka kipindi Kuchuma anamaliza mda wake alikuwa anamsapoti huyo Viktor Yanukovych na chama chake kama mrithi wa kiti cha uraisi cha ukraine unazungumzia ufisadi huyo kuchma mwenyewe alikuwa na skendo za ufasadi mkubwa tu.Huo sio ukweli, Ukraine haijawahi kuwa na utaratibu wa viongozi kubadilishana madaraka kati ya Pro-west na Pro-Russia. Viongozi wote wa nyuma waliotangulia kabla ya Viktor Yanukovych hawakuwa na upande wowote, walikuwa neutral. Viktor Yanukovych aliyechaguliwa mwaka 2010 ndiye aliyeanzisha vurumai za Pro-Russia na Pro-Russia West kutokana na kuwa fisadi aliyepitiliza na maslahi binafsi makubwa ya biashara huko Russia.
Ilikuwa lazima watoe sababu kama hiyo unafikiri watakaa mbele ya kamera nakusema wanaivamia kwasababu ilitaka kujiunga na NATO. Tukirudi tu kwenye huu uvamizi wa sasa Ukraine putin si alisema anavamia Ukraine kwasababu anataka kuondoa Nazi ideology ambayo inapelekea Genocide kwa raia wa Russia waishio Ukraine wewe unafikiri ni kweli?Sababu waliyotoa Russia ya kuivamia Georgia mwaka 2008 ni madai ya kwamba serikali ya Georgia ilikuwa ikifanya mauaji ya kimbari"genocide" dhidi ya South Ossetia ambao walikuwa waasi wanaotaka kujitenga kama kule Donbas.
Jamani jitahidini kusoma historia,kama mambo yangekuwa rahisi hivyo kama unavyosema basi USA asingehangaika kuisambaratisha USSR.Na wewe ni mmoja wa victims walioathirika na hizo propaganda za Putin za kudai kuwa Marekani inataka kuiangusha Urusi. Iwapo Marekani ingekuwa inataka kufanya hivyo, kwanza isingesimamia hiyo Budapest memorandum kuhakikisha silaha zote za Nyuklia zinakwenda Urusi na kuiacha Ukraine haine Kitu. Pili, Marekani ilikuwa na takriban miaka kumi za kuingusha kabisa Urusi yote baada ya kuvunjika kwa USSR. Badala yake katika kipindi cha kuanzia 1994 hadi 2004 Marekani iliisaidia sana Urusi kuimarisha uchumi wake bila vikwazo vyovyote; Mpaka sasa hivi Urusi inadaiwa fedha nyingi sana na Marekani ilizokopeshwa kwa ajili ya kujenga uchumi wake. Elewa hapa kuwa inadaiwa pesa ilizokopa (kama Tanzania inavyokopa), siyo pesa za kuuza hati fungante kama ambazo Marekani inadaiwa.
Tatizo la Putin ni nia ya kung'ang'ania madaraka tu, kwani kosa kubwa la Ukraine na Georgia limekuwa lile la kufanya uchaguzi na kubadilisha viongozi. Huo unakuwa ni mfano mbaya sana mlangoni mwake ambaye haamini utamaduni wa kubadili viongozi; hawezi kuishambulia Belarus mpaka pale watakapobadilisha rais
Hicho kipindi cha 1994-2004 huyo USA alimsaidia nini Urusi??,hebu fafanua.Kuvamia nchi jirani siyo option. NATO ilikuwa na uwezo mkubwa sana wa kuitawanya Urusi katika kipindi cha kuanzia mwaka `1993 hadi 2004 kwani ilikuwa na control kubwa sana juu yake lakini haikufanya hivyo, badala yake ikajikita katika kuisaidia Urusi ili isimame imare tena, halafu baada ya hapo eti ndipo uadui uanza kama Putbi hakuwa na usongo wa ndani siku hizo zote?
Kitendo cha kuivamia Ukraine hakijasaidia lolote kwenye maslahi ya nchi yake bali ndipo ameikaribisha NATO zaidi mlangoni mwake huku vijana ambao niyo nguvu ya kesho ya taifa wakiwa wanakimbia nchi. Sasa hivi Putin anajivunia wale wazee wa zamani waliokulia ndani ya Soviet Union na watu wa vijijini wanasikiliza habari kwenye TV ya Taifa tu. siyo generation mpya inayoishi kwenye majiji kama Moscow na St Pettersberg.
Tanzania tunazungukwa na Nchi 8 katika pande zote na Zanzibar ni ya 9 je kiusalama na kiuchumi katika hizo Nchi 9 ni yupi ambaye ni threat kwa Tanzania???Finland na lithuan wamejiunga NATO na majiran wakaribu wa Urussi kwanini hajawashambulia
We jamaa unavituko,sasa kama haogopi hawezi kuvamiwa why kukimbilia kujiunga na NATo?Urusi haiwezi kuishambulia Finland kwa sababu tangu uvamizi wa USSR kwa Finland mwaka 1940 uliozua Winter War Finland imekuwa ikijiandaa kikamilifu kivita na Urusi wakati wowote.
Ni kweli vyote vipo katika ardhi yako lakini vyote sio vyako.vitakuwa vyako kama una kiongozi aina ya Nyerere au Magufuli.Tanzania hapa una kisingizio gani wakati mna kila kitu. Visingizio hivi vya kijinga vitafanya Afrika ibakie kuwa kichekesho cha dunia milele.
Kumbuka yelstin ameingia ndipo siasa za ubepari zinaanza kushika hatamu Urusi.Yelstin alizungukwa na matajiri wa kubepari wwngi wakiwa wenye mafungamano na West,alipoona maji yanazidi unga ndio akaamua ampe Mwamba putin adili nao.Yaani wewe ni mrusi zaid ya Gorbachev kweli kiashi cha kumwita puppet wa west? Usilete utani hapa
Je Boris Yelstin ambaye ndiye aliyesini ile Budapest Memorandum na ndiye aliyemchagua Putin kumrithi kuwa Rais wa Urusi naye alikuwa "Puppet wa west?"
Wewe kuwa na anti-west attitude kama ya Putin haina maana kuwa basi Putin yuko sahii
Mkuu, nilikuwa naamini ukiandika kitu basi ni madini matupu, ila sasa napata mashaka kama una ID moja au?Na wewe ni mmoja wa victims walioathirika na hizo propaganda za Putin za kudai kuwa Marekani inataka kuiangusha Urusi. Iwapo Marekani ingekuwa inataka kufanya hivyo, kwanza isingesimamia hiyo Budapest memorandum kuhakikisha silaha zote za Nyuklia zinakwenda Urusi na kuiacha Ukraine haine Kitu. Pili, Marekani ilikuwa na takriban miaka kumi za kuingusha kabisa Urusi yote baada ya kuvunjika kwa USSR. Badala yake katika kipindi cha kuanzia 1994 hadi 2004 Marekani iliisaidia sana Urusi kuimarisha uchumi wake bila vikwazo vyovyote; Mpaka sasa hivi Urusi inadaiwa fedha nyingi sana na Marekani ilizokopeshwa kwa ajili ya kujenga uchumi wake. Elewa hapa kuwa inadaiwa pesa ilizokopa (kama Tanzania inavyokopa), siyo pesa za kuuza hati fungante kama ambazo Marekani inadaiwa.
Tatizo la Putin ni nia ya kung'ang'ania madaraka tu, kwani kosa kubwa la Ukraine na Georgia limekuwa lile la kufanya uchaguzi na kubadilisha viongozi. Huo unakuwa ni mfano mbaya sana mlangoni mwake ambaye haamini utamaduni wa kubadili viongozi; hawezi kuishambulia Belarus mpaka pale watakapobadilisha rais
Afrika bado hatuna viongozi hata hao unaowataja hawana lolote wamefanya nini waliiacha nchi ikiwa maskini zaidi ya walivyoikuta wakati wanaingia madarakani.Ni kweli vyote vipo katika ardhi yako lakini vyote sio vyako.vitakuwa vyako kama una kiongozi aina ya Nyerere au Magufuli.
Mfano mdogo kabisa ni ule wa issue za madini vs Magufuli.
1. Utajiri wa Afrika unaporwaje wakati tunaona kila nchi ya Afrika ikiwa inatawaliwa na waafrika wenyewe. Unaweza ukatupa uthibitisho wowote wa madai yako..?
2. Mimi nafikiri Ukraine ni nchi huru tu kama vile Tanzania, Kenya, Zambia nk, sasa kuna nchi duniani yenye haki ya kuichagulia nchi yoyote maadui au marafiki.
3. Unafahamu chochote kuhusu Budapest Agreement iliyohusisha mataifa ya Ukraine, Marekani, Uingereza na Russia.
1. Utajiri wa Afrika unaporwaje wakati tunaona kila nchi ya Afrika ikiwa inatawaliwa na waafrika wenyewe. Unaweza ukatupa uthibitisho wowote wa madai yako..?
2. Mimi nafikiri Ukraine ni nchi huru tu kama vile Tanzania, Kenya, Zambia nk, sasa kuna nchi duniani yenye haki ya kuichagulia nchi yoyote maadui au marafiki.
3. Unafahamu chochote kuhusu Budapest Agreement iliyohusisha mataifa ya Ukraine, Marekani, Uingereza na Russia.
1. Utajiri wa Afrika unaporwaje wakati tunaona kila nchi ya Afrika ikiwa inatawaliwa na waafrika wenyewe. Unaweza ukatupa uthibitisho wowote wa madai yako..?
2. Mimi nafikiri Ukraine ni nchi huru tu kama vile Tanzania, Kenya, Zambia nk, sasa kuna nchi duniani yenye haki ya kuichagulia nchi yoyote maadui au marafiki.
3. Unafahamu chochote kuhusu Budapest Agreement iliyohusisha mataifa ya Ukraine, Marekani, Uingereza na Russia.