namkumbuka sana huyu adam mwakanjuki, wakati akiwa waziri wa serikali ya mapinduzi huko visiwani, alitembelea kwetu kirafiki, wazazi walipokuwa nje kikazi, tulimwandalia chakula cha mchana tukifikiria ni mwenzetu kiimani kwa vile jina la adam mwakanjuki si la ustaadhi maalim. Alipokaribishwa alikula aina ya vyakula vyote vilivyowekwa mbele yake ila hakugusa nyama. Naona alifikiri ni kiti moto kwa vile siku iliyotangulia tulimtembeza kwa majirani wanaofuga kiti moto na kwetu kwenye zizi la ndama wa maziwa.
Kwa vyo vyote tunamkumbuka alikuwa mstaarabu na asiye na ubaguzi na kujenga uvumilivu wa hali ya juu kwa ajili ya umoja wa kitaifa.
Rip adam mkwakanjuki.