Breaking news: Gadaffi has left to south america

Guys hizi habari nimezipata kutoka tripol but soon nitakuja na confirmation report so stay tuned

uongo huu mmggh
ameapa atakufa na watu aijalishi idadi gani awe mama baba mtoto mjukuu kwa bullet na makombe ...hapa usa wamechemsha
 
Embu haya mapinduzi yahamie kwetu!Nataka kusikia kikwete kakimbilia sijui India...
 
Mimi mwenzenu nilikuwa mmojawapo wa wakimbiaji wa mabomu ya gongo la mboto.

Ni Kati ya wale waliokimbia kuelekea chanika. Nikiwa huko mstuni kwenye maficho, nilijifunza mambo mengi sana. Kwanza ndiko nilikojua kwamba makambi yote ya jeshi yalimpa kura Slaa, yakamnyima Kikwete, Pili, ndipo nilipojua kwamba watanzania wamemchoka kikwete kwa kumaanisha na si kwa utani.

Watanzania wengi wanasubiri tu muongozaji wa kuwaelekeza cha kufanya ili kwamba waweze kuingia katika maandamano ya kumuondoa Nduli Kikwete.

Watanzania wanatamani uchaguzi urudiwe ili waweze kufanya maamuzi sahihi. wengi wanajuta sana juu ya uamuzi wao wa kumchagua huyu kiongozi dikteta asiyeyahurumia maisha ya watanzania. Wapo waliofika mahali wakaonyesha wazi kuchoka na utawala huu wa kidemokrasia ambao unawaumiza na kuwakandamiza na kuona ni bora utawala wa kijeshi ambao unafahamika kuwa ni wa kikatili kuliko huu wa kidemokrasia ndani ya udikteta na ukatili mkubwa. Watu walikumbushana juu ya hali ngumu ya maisha iliyotokana na kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbli na kuongezeka kwa jumla kwa gharama ya maisha.

Watanzania wapo tayari kuandamana kuanzia sasa, anakosekana tu mhamasishaji. Kama atajitokeza yeyote ambaye yupo tayari kuanzisha hili vagi basi aamini kwamba watanzania wengi watamuunga mkono kwa dhati kabisa. Watanzania wamechoka, na kwa hisia za harakaharaka ni kwamba wanajeshi wanalipua yale mabomu makusudi ili kuongeza hasira za watanzania dhidi ya serikali yao. Na hili linaonekana kupata mafanikio makubwa sana. Maana watanzania wana hasira na Nduli Kikwete kupita kawaida.

Mkuu Lukolo kama ni hivyo basi, huyu jamaa yetu aanze kujipanga ili aondoke kiulaini asingoje kufukuzwa kwa aibu.Kwenye nyekundu sikubaliane na wewe maana huwezi kuchoma nyumba na wewe ukiwa ndani eti umepandisha munkali, hiyo ni haiwezekani.

Ila kweli Ndg yangu watu wamechoka ile mbaya. Accaunt za hawa jamaa zimejaa ile mbaya. Mfano tumeona Arusha kwa muda mfupi anga lote la Arusha lilinuka damu, wakati wa uchaguzi.

Nadhani hawa watawala watakapokosea watu waingie mitaani basi wahesabu hiyo ndio by by.Wajipange kuondoka dalilizimeisha anza kujionyesha. Aluta Continua!!!!!!
 
Mtoto wa Ghadaffi yeye amedai kua hawatishwi na kitu chochote watapigana mpaka saa ya mwisho lakini baba yake hataondoka madarakani kwa nguvu ya umma!

mkuu sijajua source ya maandamano ya libya ni nini?
 
Sasa bado kwetu huku "uwezo tunao, nia tunayo,na sababu tunazo sijui tunangoja nini"
 
Mkuu Lukolo kama ni hivyo basi, huyu jamaa yetu aanze kujipanga ili aondoke kiulaini asingoje kufukuzwa kwa aibu.Kwenye nyekundu sikubaliane na wewe maana huwezi kuchoma nyumba na wewe ukiwa ndani eti umepandisha munkali, hiyo ni haiwezekani. Ila kweli Ndg yangu watu wamechoka ile mbaya. Accaunt za hawa jamaa zimejaa ile mbaya. Mfano tumeona Arusha kwa muda mfupi anga lote la Arusha lilinuka damu, wakati wa uchaguzi. Nadhani hawa watawala watakapokosea watu waingie mitaani basi wahesabu hiyo ndio by by.Wajipange kuondoka dalilizimeisha anza kujionyesha. Aluta Continua!!!!!!

Mukwano, nafikiri ile ya Mbagala ilikuwa ni technical error, ndiyo maana wanajeshi walikufa ndani ya ule mlipuko. Lakini hii ya Gongolamboto, inasemekana wanajeshi na familia zao waliyakimbia makazi yao tangu mchana. Pale kambini walibaki walinzi tu, ambao nao walijeruhiwa kidogodogo tu.

Kama walihamisha familia zao mchana, hii haimaanishi kwamba walikuwa wamejiandaa kwa hilo? Pili, jeshi lina vyombo mbalimbali vya kuwaalert wananchi kunapokuwa na hatari na mbinu mbalimbali za kuwatangazia wananchi tahadhari mbalimbali dhidi ya hali yoyote ya hatari inayojitokeza, lakini tangu yale mabomu yameanza kulipuka wananchi hawakupata taarifa yoyote kutoka jeshini ya kuwaelekeza cha kufanya ili kujiokoa na mabomu yale.

Na hata pale mabomu yalipoisha, wananchi walipokuwa wanayakimbia makazi yao, jeshi halikuchukua hatua yoyote ya kuwatangazia wananchi kwamba hali imeshakuwa tulivu. Wadadisi wa mambo wanasema hii ilikuwa pia ni mbinu mojawapo ya kuwafanya wananchi waathirike zaidi na kupata hasira zaidi dhidi ya serikali yao.

Kwa hiyo natamani kuamini kwamba yanayosemwa yana kaukweli kidogo ndani yake.
 
very good!!! reform movement is taking control in africa!! bado JK and Dictator Museven.
 
very good!!! reform movement is taking control in africa!! bado JK and Dictator Museven.

Haya yanayotokea katika nchi nyengine, sijui kwa viongozi wa serikali za Tanzania, wa vyombo vya ulinzi wanayachukuliaje na wanajitayarisha vipi.

Huwa sina jibu ninapojiuliza hivi viongozi wa Serikali za Tanzania hawaoni yanayotokea katika nchi nyingi sasa? Tunisia, Jordan, Algeria, Egypt, Yemen, Djibout......utengano wa Sudan.

Na bado hawaoni umuhimu wa kuanza meaningful reforms za kijamii, uchumi na za kisiasa ili nchi isitumbukie katika list ya hizo nchi?
Au wanafikiri wataweza kuzuia wimbi hili? Kama wanafikiri wana uwezo wa kuzuia mabadiliko naona wanajifanya "vipofu".

Risasi zilitumika mwanzoni katika nchi za Tunisia na Misri na mwishowe matokeo yake tumeyaona, jee viongozi wetu wanafikiri risasi ndio itakuwa jawabu ya kuzima maandamano ya wanafunzi wanaotaka Mikopo reforms? Risasi na unyimaji vibali vya polisi kwa mikutano au maandamano ndio suluhisho na utatuzi wa matatizo ya wafanyakazi?

Risasi na unyimaji wa vibali ndio suluhisho la kuvidhibiti vyama vya siasa?

Wito kwa serikali, Anzeni meaningful reforms vyenginevyo wekeni askari na risasi za kutosha..yaliyoanza katika nchi hizo mpaka yameingia Libya basi mujue wananchi itafika siku watajua kuwa njia pekee ya kudai maisha bora kwa kila mtanzania ni kufuata huu utaratibu mpya wa maandamano ya umma.
 
Back
Top Bottom