Botswana waichana live USA

Botswana waichana live USA

Trump yuko sahihi kama vipi wachukue maamuzi magumu waandamane warudi nchini mwao Africa na Haiti..wasiporudi trump yuko sahihi
Bila kutukanwa hatutatoka tulipo,
Kuna watu wanajifunza kupitia makosa,
Kuna watu wanajifunza kwa kuiga
Kuna watu wanajifunza kwa kuambiwa,
Na kuna watu hata uwaambie hawajifunzi(ndo tulivyo sisi)
Ss bila kutukanwa hatujifunzi,
Narudia tena,
Tusilalamike kutukanwa,
Tujiulize tunatukanwa kwa kusingiziwa?
Nani wanaosababisha sisi kutukanwa?
Kifupi watawala wa afrika ndo sababu ya ss kutukanwa,
 
Wapo watanzania wengi wanafurahia na kutetea kuitwa shit holes.Kujikomboa toka kwenye Utumwa wa kifikra ni kazi kwelikweli.
Mkuu
Tafadhari
Tuliza akili,
Jihukumu kwa haki,
Hivi kweli yanayojiri afrika kijamii,kiuchumi,kisiasa na kiroho
Utalinganisha na wenzetu,?
Chanzo cha tusi ni :-
Tuna kila sababu ya kutokuwa tulipo lkn tumegoma makusudi kutoka tulipo,
Tunalia ufukara na uduni wakati tumehalalisha ufukara kuwa kawaida ktk maisha,
Mkuu
Hivi kweli ss ni wa kusaidiwa kujengewa VYOO na wa marekani!
Mkuu vyoo?!!
Yaani mzungu ajenge choo cha shule anayosoma mwanao,CHOO!??
ss ni zaidi ya hilo tusi,
Anapokuletea msaada wa kukujengea choo cha shule ukakubali na ukampingeza ni kukubali wewe ni mjinga zaidi ya kinachoingia chooni,
Ilishindikana nini kukataa ama kubadili tumizi la msaada huo,
Unaomba msaada wa kujengewa choo halafu ukiambiwa mchafu unalialia,
Usingejengewa choo ungejisaidia wapi km siyo porini maana ww umeshindwa kujenga na kunya ni lazima,
Ifike mahali tuwe wakali,
Wanaotutukanisha ni watawala wetu wa kiafrika,
Hivi hatuwezi jenga wenyewe vyoo,
Ukipenda mteremko ukubali na yatokanayo na mteremko,
 
Waafrika tutakubali kutukanwa maana hatuna ubavu wa kubishana na hawa jamaa
Ubavu tunao tatizo wanaotuongoza wana fikra za kitumwa,tukikataa misaada yao hatutakufa,shida zikizidi zitafanya tutafute suruhu,
Tatizo tunataka kuwafikia walipo pasipo kuuumia,tunataka tufike walipo kwa vya kupewa,
Hivi tukaamua kuishi kadri ya hali yetu,tukajikubali,na kupanga mikakati ya level yetu ya namna ya kujikwamua hatutajenga heshima yetu?
Uombaomba ndo unatuponza,kwani Korea wamefanyaje,mbona hawana misaada na wanaishi,
Maskini ukilegea utaibiwa hata mke,
Tuwe maskini jeuri hapo tutajenga heshima yetu,
Tuache kusalitiana na kuuana,tuache kufanya kazi kwa kusimamiwa,tujitume,tuache kujikomba,tuache kuwasapoti watawala wajinga
 
Maneno yake iwe chachu kwetu kuweka bidii na weledi katika kazi.
Tukipata hela atatuheshimu ,,, lakini tukiendelea kupeleka bakuri hataacha kutudharau kamwe.
 
Nchi za kiafrika wamezoea kila tamko la Trump ni kuunga mkono
 
Sema mkuu umezidisha tusi,
Nadhani wewe ni mmoja wa wavurumisha propaganda wa kijani wanaotupotoshaga daily,
Tusi halikuwa hivyo,
Labda umejinukuu ulivyo ukaamua kubambika
Mkuu kwanini kila kitu kitafsiriwe CCM au CDM hivi kweli watanzania hawana muamko mwengine kiakili?Mkuu dunia ina mambo mengi sana ya kufanya badala siasa,.....

Watanzania mmegubikwa na siasa za CCM na CHADEMA,mimi mkuu sio wa kijani wala wa blue mimi ni mimi,siasa yangu kubwa ni kutafuta pesa ile nihudumie familia yangu...
 
Watz kujidharau! Haya, akitokea mtu kama JPM anayeonyesha nia ya dhati kuipeleka Nchi ifanane na hizo za wenzetu. Maneno. Tusijinyanyapae! Unadhani wazungu walifika walipo kwa mzaha? Watu wengi hata walikufa. Someni historia ya mataifa ya Dunia hii. Ni vita. Oh. uchumi unaporomoka! Ni lazima uporomoke. Ni nadharia rahisi, mtu mwenye hekima akiamua kujitegemea chakula hutumia hata mbegu za chakula kupanda shambani na haimtishi kwani anajua njaa hiyo ni ya kitambo tu. Tumuunge mkono JPM, nyie akina mangi. Dhiki hii ni ya kitambo tu. Kweli tuliopo pengine na hata watoto wa wajukuu zetu watakuta bado msingi haujaimarika. Tusikate tamaa. Tuache ubinafsi.
 
Kwani sasa ni wasafi?

Usafi wenu uko wapi?

Watu mmejaa uwongo uliokithiri. kuoneana kusikotamkika, hamuwezi kujitawala, hamthaminiani, mnapigana risasi hadharani na bado mnaidhinisha uonevu huo, viongozi wenu wanaidhinisha uvunjivfu wa amani na ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu. Hata sheria za nchi mliozojiwekea mnauhuru wa kuzivunja hadharani na kisha kutumia mabavu kulinda uvunjaji huo, hamtaki kufanya yale watu wengi wanataka ambayo ni bora kwa ustawi wa taifa badala ayke mnafanya usani i kwa maslahi ya watu wachache. Mnatumia ujinga wa binadamu kama nyenzo ya kuwatawala kwa maslahi yenu.

AU UNADHANI TRUMP AMESEMA HAYO KWA KUMANISHA USAFI WA NGUO NA MWONEKANO WA RANGI?

DAWA NI SIYO KUFUNGA UBALOZI. KUFUNGA BALOZI HAKUFENYI MUWE WASAFI. NI KAMA VILE KUMUUA TUNDU LISU AMBAVYO HAKUJATUPATIA NOAH KILA MTANZANIA, HAKUJAFANIKISHA KULETA NDEGE YETU HAPA NYUMBANI, HAKUJAPUNGUZA UGUMU WA MAISHA.

MKITAKA KUONEKANA WASAFI, ISHINI MAISHA SAFI NYUMBANI KWENU. MSITAKE KULAZIMISHA WATU WAWAITE WASAFI WAKATI MNASHEHENA CHAFU MIOYONI MWENU HUKU DAMU ZA NDUGU ZENU ZIKIWALILIA.
Kurudisha mabalozi nyumbani itasaidia kushinikiza Trump aache kudharau Nchi za Kiafrika,Nchi ya Marekani na Ulaya ya Magharibi ni mahodari sana wa kuweka vikwazo vya uchumi kama kuna nchi inafanya wasivyotaka wao...

Wakiona vikwazo vya uchumi havifanyi kazi kwa nchi husika huwa wanatumia mpaka vita ili nchi husika ikae kwenye mstari,huo ndio ukweli kaka
 
Halafu watu kma wewe huwa mnaongelea tu kwenye keyboard, fanya kwa vitendo hlf uwe msitari wa mbele tukuone mkuu, napenda watu wenye mawazo mazuri kma haya lkn kwa vitendo siyo kutanguliza wenzenu.
Ni tabia ya kila mtanzania kuwa na nidhamu ya woga,nafikiri Watanzania ni watu wa mwanzo dunia kuwa na nidhamu ya woga....,

Umeanza kuogoba hata hujaingia huko barabarani,kusoma tu hichi nilichokiandika tayari,surwali imeroa wa mikojo,nidhamu ya woga ni adui wa maisha,adui wa maendeleo..

Nchi na watu walioendelea kwanza wamejitolea muhanga, wameondoa woga ndio wakafanikiwa kwa kile wanachokifanya
 
Nimeangalia maana ya shithole ni "very dirty or unpleasant place" yaani mahali pachafu sana au pasipovutia. Sasa kwa baadhi yetu ambao tumebahatika kufika au kuishi kwenye moja ya miji katika nchi zilizoendelea hususani ulaya, amerika na kwingineko utaona wazi kuwa Trump hajakosea. Chukulia jiji la Dar es Salaam ambalo ndio tunategemea liwe kioo cha nchi, unapita mitaani barabara hazina lami, hakuna pavements sehemu za waenda kwa miguu, yaani kila sehemu ni mivumbi tu inatimka, nyumba ni kama magofu zimejengwa shaghalabagala, mitaro imejaa takataka na maji machafu, barabara ni mashimo ikinyesha mvua kidogo zinageuka kuwa mabwawa, watu wanafungulia chemba za choo, umeme kukatika ni kawaida vitu ambavyo ni nadra kukutana navyo kwenye nchi za wenzetu. Badala yake nchi za kiafrika zimeghubikwa na tawala mbovu, ufisadi, rushwa, siasa zisizo na tija, ubinafsi wa kujilimbikizia mali na madaraka na uwajibikaji wa kiwango cha chini. Kwa hiyo, ni bora tujitafakari wenyewe kuliko kubaki tukilalama tu kuwa tumetukanwa
 
Mkuu kwanini kila kitu kitafsiriwe CCM au CDM hivi kweli watanzania hawana muamko mwengine kiakili?Mkuu dunia ina mambo mengi sana ya kufanya badala siasa,.....

Watanzania mmegubikwa na siasa za CCM na CHADEMA,mimi mkuu sio wa kijani wala wa blue mimi ni mimi,siasa yangu kubwa ni kutafuta pesa ile nihudumie familia yangu...
Upo sahihi lkn kwanza kubali ulilizoom tusi kwa sababu unazozijua,
Pili nikukumbushe kitu ambacho yamkini unajisahaulisha,
Siasa inaendesha maisha ya kila mtu kila siku,
Hata ninyi mnaodhani hamshiriki siasa,mnaodhani mnachofanya hakiguswi na siasa eti sababu hamjihusishi na vyama,
Km unakataa fukunyua sababu za ss kutukanwa na trump ni sababu za kisiasa,kwa maana ya aibu wanayotusababishia watawala wetu,
 
Ni tabia ya kila mtanzania kuwa na nidhamu ya woga,nafikiri Watanzania ni watu wa mwanzo dunia kuwa na nidhamu ya woga....,

Umeanza kuogoba hata hujaingia huko barabarani,kusoma tu hichi nilichokiandika tayari,surwali imeroa wa mikojo,nidhamu ya woga ni adui wa maisha,adui wa maendeleo..

Nchi na watu walioendelea kwanza wamejitolea muhanga, wameondoa woga ndio wakafanikiwa kwa kile wanachokifanya
Hujazaliwa jana, hebu anzisha basi kwa vitendo mi niko nyuma yako
 
Watz kujidharau! Haya, akitokea mtu kama JPM anayeonyesha nia ya dhati kuipeleka Nchi ifanane na hizo za wenzetu. Maneno. Tusijinyanyapae! Unadhani wazungu walifika walipo kwa mzaha? Watu wengi hata walikufa. Someni historia ya mataifa ya Dunia hii. Ni vita. Oh. uchumi unaporomoka! Ni lazima uporomoke. Ni nadharia rahisi, mtu mwenye hekima akiamua kujitegemea chakula hutumia hata mbegu za chakula kupanda shambani na haimtishi kwani anajua njaa hiyo ni ya kitambo tu. Tumuunge mkono JPM, nyie akina mangi. Dhiki hii ni ya kitambo tu. Kweli tuliopo pengine na hata watoto wa wajukuu zetu watakuta bado msingi haujaimarika. Tusikate tamaa. Tuache ubinafsi.
Ondoa itikadi uchwara na propaganda tumika,humu tunajadili upana wa jambo zaidi ya itikadi za kitumwa,
Kwani yanayojiri tz hakuna lililo chanzo cha tusi tulilotukanwa!?
 
Kurudisha mabalozi nyumbani itasaidia kushinikiza Trump aache kudharau Nchi za Kiafrika,Nchi ya Marekani na Ulaya ya Magharibi ni mahodari sana wa kuweka vikwazo vya uchumi kama kuna nchi inafanya wasivyotaka wao...

Wakiona vikwazo vya uchumi havifanyi kazi kwa nchi husika huwa wanatumia mpaka vita ili nchi husika ikae kwenye mstari,huo ndio ukweli kaka
Dharau haiishi kwa wao kuacha kututukana midomoni,
Dharau itaisha kwa ss kujitambua,
Wanaweza wasitutamkie mdomoni lkn mioyo yao ikawa inatuchukulia zaidi ya tusi
 
Back
Top Bottom