Botswana waichana live USA

Botswana waichana live USA

fca00763a570844bada7aa7ad6c2c3c7.jpg

DUUUU.NIMEIPENDA HII AISEEE.hilo ndio shimo lenyewe klumbeeee
 
Botswana wananifurahisha sana.

Nimetokakusemakwenye thread nyingine, nchi za Afrika zinatakiwa kufukuza hawa mabalozi wa Marekanina kuvunja uhusiano wa kibalozina Marekani mpaka rais wa Marekani aombe radhi.

Aone kwamba Marekanihata kama ina nguvu vipi, nayo pia inategemea ushirikianona nchi za ki Afrika katika vita dhidi ya ugaidi, biashara etc.

Afrika kwa sasa inaweza kirahisi sana kuamua kufanya biashara na Ulaya na China, ikaipotezea Marekani.
Ndoto za mchana hizo
 
Nafikiri BOTSWANA wamekasirika na wamejibu sababu wao wanajielewa ..huwezi kulinganisha uchumi wa botswana na nchi zingine za kiafrika.haswa zile zenye madikteta na demokrasia ni ndoto ..wengine wako kimya sababu wanaona ni KWELI
 
I think na nchi nyingine tu-condemn udhalilishaji huu wa lile dude. Tukikaa kimya itaonekana tumebariki matusi yake
Tuache ujinga,
Tu condemn kuambiwa ukweli,
Tunatakiwa kuwachana,ama kuwabana ama vyovyote utavyoita viongozi wetu maana ndo wanafanya tuonekane tundu la kinyesi,angalia wanayofanya km siyo chanzo cha ss kutukanwa,hata tusipotukanwa kwa kuambiwa lkn kwa vitendo tunatukanwa na ni sahihi,
Ss ni wa hovyo kabisa,
Sababu ya ss kuonekana wa hovyo ni viongozi wetu,
Wameshindwa kusimamia elimu bora ambayo ingetukomboa,wameshindwa kusimamia uchumi wetu Japo tuna Mali kibao ambazo zingefanya tuishi vyema,wameshindwa kusimamia demokrasia na haki ambavyo ndo vyanzo vya vita na maisha ya kukimbia kimbia nchi zetu,
Yes we ar *****
 
Aliyotendewa lissuh wapo wanaofrhia lkn wanasahau ndo yanayofanya tuonekane tundu la kinyesi,
Huo ni moja ya mfano,
Yanayofanyika somalia wapo wanaoshangilia sababu za dini lkn wanasahau ni moja ya yanayofanya tuitwe tundu la kinyesi,
Nk nk
 
Tatizo letu sisi wabongo ni kutokujua Kiingereza vizuri. Watu wengi wanatafsiri neno "shit-hole" moja kwa moja na kusema eti ni shimo la choo. Hapana, maana ya neno hili "shit-hole" ni sehemu chafu sana, ya ovyo ovyo isiyokuwa na mpangilio au unaweza kusema; sehemu isiyovutia.

shithole
ˈʃɪthəʊl/

noun
vulgar slang
noun: shit-hole

  1. an extremely dirty, shabby, or otherwise unpleasant place.
    "this place is a shit-hole, I hope you know that"
Kiukweli Trump hajakosea kusema Africa is a shit-hole, Africa ni chafu kwenye kila kitu, kwenye uongozi, kwenye mitaa, kwa watu binafsi wengi wetu ni wachafu sana. Miji yetu ni michafu mpaka karne hii ya 21 bado Africa kuna kipindu pindu hasa hapa kwetu Tanzania.

So if you put it metaphorically, Trump is right, Africa is really a shit-hole and I agree with 100%
 
Afrika inazo changamoto nyingi,lakini si sahihi hata kidogo kutumia kauli kama hiyo.

Hongera serilikali ya Botswana kwa kuliona hilo na kulichukulia hatua mapema.
Ulistahili uungwaji mkono,lakini bahati mbaya wenzio wako busy na masuala mengine ya kuwazia kubadili katiba hususan vipengele vya ukomo wa madaraka.
 
Botswana lalamiki matamshi ya Rais Trump
 

Attachments

  • IMG-20180112-WA0013.jpg
    IMG-20180112-WA0013.jpg
    36.1 KB · Views: 50
Kuna nchi Afrika zimeshtuka kimawazo,na kuna nchi zimelala kimawazo,moja katika nchi zilizoamka ni pamoja na nchi ya Botswana,na katika nchi zilizolala kimawazo ni nchi kama majirani zetu Kenya na Rwanda

Sio siku nyingi zilizopita raisi wa marekani alitanganza kuwa Jerusalem ni mji mkuu wa Israel,nchi nyingi zilipinga hatua hiyo,lakini Kenya na Rwanda zilikubaliana na Trump...

Tukumbuke Kenya vile vile ilikuwa inaunga mkono utawala wa ubaguzi wa rangi(Apatheid) Afrika Kusini....

Trump katika siasa zake zinaohusu uhamiaji,kauliza kwanini nchi zenye watu wachafu kama makalio, kakusudi watu wa Afrika ikiwemo Kenya,Rwanda na Haiti kwanini wanakuja kuishi marekani..?

Botswana imechukuwa hatua ya kumrejesha balozi wake nyumbani,ni hatua nzuri sana kwa watu wanojijua,kama nchi za Afrika zitaiga mfano wa Botswana basi dunia itaziheshimu nchi za Afrika

Je Tanzania tutasubutu kama walivyofanya Botswana....?


Habari kutoka BBC
taz.jpg

Serikali ya Botswana imemshutumu Rais wa Marekani kwa kusema mataifa ya Afrika ni "machafu" na kusema tamko lake rais huyo ni la kukosa kuwajibika, la kukera na "ubaguzi wa rangi".

Bw Trump alisema hayo alipokuwa akizungumzia sera ya uhamiaji ya Marekani, ambapo alisema anafikiti watu kutoka Haiti, El Salvador na nchi za Afrika hawafai kuruhusiwa kuingia kama wahamiaji Marekani.

Botswana imesema kupitia taarifa kwamba imemwita balozi wa Marekani nchini humo kufafanua iwapo Marekani inachukulia taifa hilo la kusini mwa Afrika kama "taifa chafu" na taifa la mabwege.

Taarifa hiyo ya Botswana imesema tamko la Trump ni la kukosea heshima taifa ambalo lina urafiki wa kufana na uhusiano wa kibalozi.

Botswana imeitaka jumuiya ya kiuchumi ya nchi za kusini mwa Afrika Sadc pamoja na Umoja wa Afrika kushutumu tamko hilo la Trump.

Bw Trump kwenye Twitter hata hivyo amejitetea na kusema hakutumia maneno hayo, lakini akasema aliyoyasema yalikuwa na "lugha kali".

Msemaji wa Umoja wa Mataifa amesema tamko hilo la Trump ni la kushangaza, la aibu na la ubaguzi wa rangi.

Rupert Colville amesema: "Iwapo yatathibitishwa, matamshi haya ni ya kushangaza na ya aibu sana kutoka kwa rais wa Marekani, nasikitika kwamba hakuna maneno mengine ya kueleza hili ila kusema kwamba ni ubaguzi wa rangi.

tru.jpg
 
Back
Top Bottom