BoT yatangaza Noti mpya

BoT yatangaza Noti mpya

Huu Uzi bila kua na Picha tutakua tunajadili vitu ambavyo ni vya kijinga
Lete picha tuwe na mjadili halisia
 
Mimi naomba kusaidiwa kufahamu, kwanini serikali imebadilisha baazi ya noti kimia kimia? Je nini adhali za kiuchumi? au ndio kuingiza noti nyingi ilizitusadie kwenye uchanguzi? Wachumi naombeni msaada wenu!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
PierreLiquid,
Zote hizo ni fedha halali ili kutofaunisha na noti feki zingatia security features kwenye noti.
 
JF ni mtandao unaoongoza kwa kuwa na watu "Wajinga" kuliko sehemu nyingine.
Mtu mmoja humu JF kwa ujinga wake alileta Uzi unaosomeka:-
"Kutokana na hali ya uchumi kuwa mbaya nchini, kwa nini serikali isichapishe noti mpya na kuziongeza kwenye mzunguko?"
Halafu baada ya muda serikali imemsikiliza mjinga yule na kufanya aliyopendekeza!
Serikali yetu inasikiliza wajinga? Nashangaa

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu kuna wakati ni busara kukaa kimya.
  1. Wewe unajua fedha mbovu au zilizo chakaa kiasi gani zimerudishwa BOT?
  2. Unajua pesa kiasi gani zilifichwa na watu wenyewe wakafa au wapo jela, au zikaharibika, au zilizo ungua kwenye ajali za moto, zilizo zama kwenye mafuriko ajali za meli na vivuko?
  3. Unajua serikali ina mpango gani wa kuzikusanya fedha hizo za zamani taratibu kwa kuziondoa kwenye mzunguko?
  4. Unajua inachukua siku ngapi kufanya mabadiliko , kuchapisha fedha na kuzisafirisha toka nje zinako tengenezwa kwenda BOT kisha kwenye mabenki yetu ya kibiashara, maana muda alio andika yule mtu na leo fedha mpya ipo kwenye mzunguko ni muda mfupi sana.

Hizo zote namba 1 na 2 hazipo kwenye mizunguko tena, na anaye fuatilia pesa zilizo kwenye mzunguko ni BOT.
Kuna mengi ya kukufumbua akili lakini kwa sasa niishie hapo.

Ni akili ya ajabu sana kuamini watu wote serikalini, wizara ya fedha, BOT na baraza la mawaziri ni wajinga na wewe ndio pekee una akili nyingi sana.
 
Ukaona nchi inachaposha noti ujue uchumi umeporomoka. Hakuna pesa kwenye mzunguko inaongoza nyingine ambazo hazina uwezo wa kununua chochote nje. Mlitwambia nchi tajir hii haya sasa twende kaziiii

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh mtihani kwa nini basi Serikali isingebadili rangi ya hiyo noti ili kuitofautisha ama wangeipunguza size...
 
Back
Top Bottom