BoT Saga Unfolding: Ballali ni Kafara

Mr Mikael

Hilo swala la Watanzania(waafrika) wakiwa na watu weupe hasa ulaya na Marekani hua wanafanya vizuri mnoo mie bado najiuliza hua nini haswa ? lakini huyo huyo ukimchanganya nyumbani ndiyo mborongaji mzuri

Hii si ki elimu tu hata ukianglia mpira wa mguu waafrika wanapochezea timu zao za ulaya wakichanganyikana na wazungu hua wanacheza vizuri mnoo lakini hao hao wakija kwenye timu yao ya taifa unaona kiwango kipo chini mnoooooo.

Mie hua wakati mwingine nafikiri wenda waafrika hua tunakitu kidogo tuna kimiss tunapokua wenyewe na ikitokea ukachanganyikana na mzugu hiyo weekness wenda mzungu hua ana i overcome na tunafanya vizuri.
 
balali anayo phd..kuna makala moja nimepata kusoma..inamtaja balali kama moja ya reliable eminent economist waajiriwa wa IMF..ambapo yeye akiwa na wenzake wanne walitumwa na world bank kwenda kusaidia reform policy zilizoifanya MALAYSIA kuwa tiger asia leo hii....na pia kwenye jarida hilo alitaja mikakati ambayo inaweza kuipaisha nchi kama tanzania kama ikifuatwa....sijui kwa nini watanzania wanaoheshimika nje wanashindwa kuwa msaada nyumbani..may be tuna wa misuse..

kuhusu phd alisema kule IMF hawapendi kujiita dr..simply kwa sababu karibu wote wenye ngazi ya juu na wa kati wengi ni phd holder...kwa hiyo wanaamua kurahisisha ..la kila mtu angeitwa dr..dr...ikumbukwe kuwa balali aliazimwa na mkapa toka IMF akaaza kwa kumshauri kidogo alipoingia 1995 kabla hajampa ugavana...kutokana na familia yake kuwa newyork aliishi new africa hotel kwa karibu mwaka mmoja,kabla ya kuhamia kwenye nyumba yake na baadaye kidogo kumuoa ms muganda..baada ya kuwa amemdivorce mkewe ulaya...ON SECONDMENT...nadhani ajira yake kule bado ipo...pamoja na huu wizi uliotokea mwishoni mwa mwaka 2005...sera za kiuchumi za balali walizokuwa wakimshauri mkapa pamoja na yule raia wa ghana ..zilifanikiwa..kwa kiasi fulani...

kwa reference ya gazeti la mtanzania daima...ndugu yake aliyehojiwa anasema balali ameandikisha maelezo ya anachojua yeye kuhusu ufisadi..akitaka kusafisha jina lake kwa kuonekana a sole player..na imeelezwa kuwa hii kashfa chanzo chake ni watu wazito zaidi yake..maelezo yamehifadhiwa kwa wakili asiyejulikana..na kuna ndugu zake wameshapewa maelezo kuwa if anything happens kabla hajaweza kuyatoa mwenyewe ..basi yatolewe for public consumption.....

Huenda Ballali mwenyewe aliomba asiitwe Dr na kufuata utaratibu wa huku kwa wenzetu.

Kama hauko vyuoni au kwenye reseach kikawaida hutakiwi kutumia hiyo title ya Dr. au Professor kwa maana ya kwamba una Ph.D. au ni professor.

Ninashangaa wanasiasa muda wote kujiita Dr. Mbona hata siku moja hatujawahi kusikia Dr. Brown (PM wa UK)?
 
The thing is - Mkapa, and by extension Balali, wamesifika sana katika kuubadilisha mwelekeo wa hali ya uchumi Tanzania (whether this is true or not I am not the one to judge).

Pengine haya ya kujihusisha kwao na ufisadi mkubwa yasingejitokeza wakati huu tungeendelea kuwapa heshima zao kubwa katika mafanikio ya kuleta mabadiliko hayo ya kiuchumi.

Mkamap:
No problem buddy.
 
Wan JF.
Msipoamini habari nilizoandika kuhusu poision aliopewa huyu bwana balali hiyo ni shauri yenu. Lakini ukweli uko pale pale na ndio hicho kilichotokea.Aliyenipa hizi habari ni mwanafamilia wa Balali na unajua tena hawezi wenda indeep more that that maana naye hajui kama mimi nilikuwa namchota ili nilete habari au la! Lakini kwa kuwa ninaishi hapa na nimejiahidi kuyasaka yale nayoweza kuyapata kutoka kwa ndugu wa balali aliyeko hapo. Lakini tatizo la JF kuna ka-tabi ka kudhalilishana. Ukiniuliza maswali eti kwa nini hawakumpa maziwa mara baada ya kugundua amepewa sumu...sasa mimi unataka nikujibu nini. Ninachojua ni kwamba hiyo sumu iliharibu sehemu za utumbo wako kama nilivyoeleza ndio maana akafanyiwa operashion. Tuwe tunaheshimu mchango wa mawazo ya wenzetu kuliko kukandia na kuingiza ukabila kwa waota habari kama baadhi ya memmbers hapa mlivyonishambulia. Ukweli utakuja julikana na mimi naamini nilichokisema kitaibuka kuwa cha kweli na hakuna yeyote hapa atakayekubali kwamba nilishakisema. Mimi nitaendelea kudondosha habari kila nitakavyozipata.
"BALALI YUKO KWENYEHOTEL NDOGO YA MTAANI NA SI RAHISI KUMPATA KWASABABU HOTEL HIYO SI POPULAR SANA" hayo ni kati ya niliyoyataja kwenye thread yangu ya awali na yametoka kwa huyo mwanafamilia wake. Tuache ubishi usio na sababu bali tudadisi.

Nshomile,

Nina wasiwasi sana na maneno uliyoambiwa. Unajua suala la Ballali kuna spinning nyingi sana lakini wakati mwingine ni rahisi kuondoa spinning kutoka kwenye facts kwa kuangalia utendaji wa huku.

Ballali yuko USA, kama sumu ilitumika kumuunguza, hospitali yoyote alikoenda, kitu cha kwanza watatoa report polisi. Huo ni uhalifu na Dr.
yeyote huku magharibi akiona kitu kama hicho, anatakiwa kutoa taarifa polisi.

Nitashangaa kweli kwa USA kama itaonekana Ballali kapewa sumu na vyombo vya dola visiingilie, nitashangaa sana.

Huenda wanaotoa uvumi kama huo hawajui jinsi hospitali huku nje zinavyofanya kazi.

Hivi hapa hatuna madaktari ambao wanafanya kazi Europe au USA ambao wanaweza kutusaidia ku clarify juu ya hili?

Mimi ninachohisi ni kwamba Ballali anahusika kwenye wizi huo, ameshirikiana na watu wakubwa serikalini, wamemficha USA kwa faida yake yeye Ballali na hao watu wa serikali. Watajaribu kumtoa yeye kafara lakini hawatamtafuta kutaka arudi nyumbani.

Kuna ndugu wa Ballali wako hapa na laiti ingelikuwa issue ni sumu, ungesikia cheche ambavyo zingemwagwa. Naamini hakuna ukweli, hata wanaosema hayo ni kutaka kumlinda ndugu yao.

Walikuwa na uwezo wa kuitoa barua yake ya kujiuzulu, wakitegemea itasaidia kuondoa balaa la kufukuzwa kazi. Sasa naona wanaanza spinjing zingine.

Ballali inatakiwa afanye alicho fanya Marion Jones, atoke clean hata kama
itamfanye aadhibiwe. Waliosema "If you are in a hole, stop digging" hawakukosea. Usanii unaoendelea sasa huenda ukamletea matatizo zaidi huko mbele.
 
Mtanzania:
liyoyasema kuhusu kuripoti mambo yanayohusiana na uhalifu yana ukweli kwa kiasi fulani. Lakini pia usisahau utashi wa mgonjwa mwenyewe.

La mhimu zaidi, nina hakika hapo Ulaya na huko Marekani, ni uhifadhi wa habari za mhusika (Protection of Information). Ugumu unaongezeka zaidi uhalifu unapokuwa umefanyika nje ya mipaka na hapo anapotibiwa mgonjwa mwenyewe.
 
Mtanzania:
liyoyasema kuhusu kuripoti mambo yanayohusiana na uhalifu yana ukweli kwa kiasi fulani. Lakini pia usisahau utashi wa mgonjwa mwenyewe.

La mhimu zaidi, nina hakika hapo Ulaya na huko Marekani, ni uhifadhi wa habari za mhusika (Protection of Information). Ugumu unaongezeka zaidi uhalifu unapokuwa umefanyika nje ya mipaka na hapo anapotibiwa mgonjwa mwenyewe.

Kalamu,
Kama kuna mchezo mchafu hakuna cha kusubiri utashi wa mgonjwa. Labda mgonjwa mwenyewe sijui atumie njia gani kuelezea kwamba alikunywa sumu kwa bahati mbaya, lakini in most cases, polisi wataitwa.

Pia nitamwona Ballali mjinga kweli, yaani anapewa chakula chenye sumu ili afe, anaenda USA ambako ana uhuru wote, ana nyumba na familia na si ajabi hata uraia, anakaa kimya mpaka afe. Ballali sio mjinga kiasi hicho hata siku moja.

Hata kama umefanya makosa, lakini mtu anataka kukuua na bado unakaa kimya?

Hii story nzima ya sumu hainiingii kabisa kichwani. Kuna spinning kubwa sana inaendelea. Hata huyo mkewe na nafasi yote World Bank, bwanake anapewa sumu, eti atakaa kimya? Nitakuwa wa mwisho kuamini story kama hiyo.
 
Nililo na uhakika nalo ni kwamba hakuna hospitali yoyote huko USA itakayotoa taarifa kuhusu habari zozote za mgonjwa wao Balali, awe amenyweshwa sumu au la bila ya ridhaa yake.

Spinning kubwa ninayoiona hapa ni kuhusu serikali kujifanya hawajui mengi juu ya mtumishi wao wa ngazi ya juu, kiasi kwamba hawataki wananchi wajue.

Balali na serikali (au mafisadi waliomo serikalini) wamo katika mchezo wa 'chess' Kila mmoja wao analinda upande wake.
 
Nililo na uhakika nalo ni kwamba hakuna hospitali yoyote huko USA itakayotoa taarifa kuhusu habari zozote za mgonjwa wao Balali, awe amenyweshwa sumu au la bila ya ridhaa yake.

Kalamu,

Hapo sikubaliani na wewe, labda kama una maana hospitali kutoa taarifa kwa vyombo vya habari. Lakini kutoa taarifa polisi ni wajibu wao. Kumnywesha sumu mtu ni crime na kila raia ana wajibu wa kutoa taarifa polisi anapokuwa na ushahidi au wasiwasi wa kuonyesha kwamba huenda kuna crime imetendeka.

Hata TZ tu ukienda hospitali na jeraha la ajabu ajabu ambalo linaweza kuwa limetokana na uhalifu wa aina fulani, bado wanatoa taarifa polisi hata bila idhini yako.
 
Mtanzania:
Unachukua liberty ya ku-assume kuwa Balali alikwenda pale hospitalini kuripoti kuwa amenyweshwa sumu' mimi sijui kama hivyo ndivyo alivyofanya. Na kama katika uchunguzi wao hapo hospitalini wakigundua kuwa ni sumu ndiyo iliyomletea madhara, je wamlazimishe awaambie ni nani aliyemnywesha hiyo sumu ili wamlipoti polisi?

Hospitali zinaogopa sana mambo ya kutoa taarifa za wagonjwa bila wagonjwa wenyewe kukubali na kushirikishwa kwa karibu sana; complication inaongezeka wakati uharifu wenyewe umetendeka nje ya nchi.
 
Mtanzania:
Unachukua liberty ya ku-assume kuwa Balali alikwenda pale hospitalini kuripoti kuwa amenyweshwa sumu' mimi sijui kama hivyo ndivyo alivyofanya. Na kama katika uchunguzi wao hapo hospitalini wakigundua kuwa ni sumu ndiyo iliyomletea madhara, je wamlazimishe awaambie ni nani aliyemnywesha hiyo sumu ili wamlipoti polisi?

Hospitali zinaogopa sana mambo ya kutoa taarifa za wagonjwa bila wagonjwa wenyewe kukubali na kushirikishwa kwa karibu sana; complication inaongezeka wakati uharifu wenyewe umetendeka nje ya nchi.

Kalamu,

Mimi scenario yangu ni kwamba, mgonjwa anafika hospitali akiumwa tumbo, anachukuliwa vipimo. Majibu yanaonyesha ni sumu, mgonjwa anahojiwa, asipotoa maelezo ambayo yanatosheleza, sio kazi ya madaktari kufanya uchunguzi, wanapeleka taarifa polisi. Polisi ndio wanafanya uchunguzi juu ya nini kimetokea na how.

Mfano mwingine hata kwa TZ, mama anafika hospitali, kaumia usoni, daktari
anamwuliza nini kimetokea, mama anasema ameanguka, daktari asiporidhika basi anatoa taarifa polisi bila ya idhini ya huyo mama. Ni kazi ya polisi kuchunguza huyo mama kaumiaje. Wanaweza kugundua kapigwa na bwanake na anaogopa kumfunga asije akakosa bwana.

Cases zote hizi mbili, kama daktari asipotoa taarifa polisi basi ana makosa. Kwa TZ mara nyingi kama una jeraha ambalo halieleweki, unaambiwa huwezi kutibiwa mpaka uje na form ya polisi. Hiyo ni kuhakikisha polisi wanapata nafasi ya kuchunguza kama kuna crime imetendeka.

Kwa wenzetu hurudishwi ili uende polisi kwanza, ila tu hiyo taarifa inapelekwa polisi na watakusubiri tu upate nafuu ili wakuhoji.
 
Mtanzania:
Hili tuliachie hapa. Ukweli ni kwamba, kwa hali ya Marekani, hospitali yoyote haina madaraka ya kulipeleka jambo la matibabu ya Balalli polisi bila ya ridhaa yake binafsi, au bila ya kuwepo mtu ambaye anadai kuwa na udhuru/manufaa na jambo hilo.
 
Mtanzania:
Hili tuliachie hapa. Ukweli ni kwamba, kwa hali ya Marekani, hospitali yoyote haina madaraka ya kulipeleka jambo la matibabu ya Balalli polisi bila ya ridhaa yake binafsi, au bila ya kuwepo mtu ambaye anadai kuwa na udhuru/manufaa na jambo hilo.

Kalamu,

Mimi siishi USA kwahiyo inabidi niseme sijui utaratibu wa huko ukoje. Ila nitashangaa sana kama wanafanya tofauti na sehemu kama UK ambapo nina uzoefu napo.

Hata kama ni mwangaliaji wa picha, kuna cases kama hizi nyingi tu na polisi huwa wanaitwa. Kwa ueleo wangu mara nyingi picha huwa zina reflect the laws of the land.

Any way sio muhimu, muhimu tu ni kwamba mpaka upewe sumu na bado unakaa kimya? Kweli haiingii kichwani.

Aliko Ballali ni makubaliano yake na hao anaowalindia siri, vinginevyo angekuwa kufikia sasa anatapika kila siri aliyonayo.

Kwa USA kama viongozi walijaribu kumuua kwa kumpa sumu, hata wakimtaka arejeshwe, haiwezekani, atashinda tu mahakamani. Kwahiyo kwa kweli sioni kabisa sababu ya yeye kukaa kimya hata baada ya kupewa sumu.

Naona story nzima ina viraka vingi mno.
 
Mtanzania,
Nikupe upande mwingine wa issue? What if the powers that be do not want the former governor to return home? Unadhani hawa watachukua hatua zozote arejeshwe nyumbani baada ya RO kumwambia bayana kwamba asirudi Bongo na kupona kwake ni miracle? Balali's mother, brothers and sisters are in Dar. He would love to be with them. But all in all tuvute subira. Time will tell
 
Naendelea kuamini kuwa Ballali amejichimbia mahali anamalizia manuscript ya true story, "The BoT saga: The Untold Story" ambayo itakuwa bestseller. New York Times watainunua kwa $ 500,000.
 
Mtanzania,
Nikupe upande mwingine wa issue? What if the powers that be do not want the former governor to return home? Unadhani hawa watachukua hatua zozote arejeshwe nyumbani baada ya RO kumwambia bayana kwamba asirudi Bongo na kupona kwake ni miracle? Balali's mother, brothers and sisters are in Dar. He would love to be with them. But all in all tuvute subira. Time will tell

Jasusi,

Naamini ulichoandika hapo ndio karibu na ukweli. Serikali hawataki Ballali arudi kwasababu wana siri naye moja.

Ila tu haiingii akilini kwamba Ballali kanyweshwa sumu, kakimbia USA ambako ana familia na makazi na bado ameendelea kukaa kimya. Nitamshangaa kweli
kama kafanya hivyo.

Ninachoamini serikali wamemtoa kafara yeye, kwahiyo yuko USA kwa faida yake na faida ya hao vigogo.
 
Nikupe upande mwingine wa issue? What if the powers that be do not want the former governor to return home? Unadhani hawa watachukua hatua zozote arejeshwe nyumbani baada ya RO kumwambia bayana kwamba asirudi Bongo na kupona kwake ni miracle? Balali's mother, brothers and sisters are in Dar. He would love to be with them. But all in all tuvute subira. Time will tell


Very strong and powerful, mkuu Jasusi tunakuaminia wewe na MMJ, tuwekeeni dataz tuzichambue, shukrani japo kwa mwanga kidogo, maana ukijumlisha hii na ile ya MMJ, unapata something!
 
Wan JF.
Msipoamini habari nilizoandika kuhusu poision aliopewa huyu bwana balali hiyo ni shauri yenu. Lakini ukweli uko pale pale na ndio hicho kilichotokea.Aliyenipa hizi habari ni mwanafamilia wa Balali na unajua tena hawezi wenda indeep more that that maana naye hajui kama mimi nilikuwa namchota ili nilete habari au la! Lakini kwa kuwa ninaishi hapa na nimejiahidi kuyasaka yale nayoweza kuyapata kutoka kwa ndugu wa balali aliyeko hapo. Lakini tatizo la JF kuna ka-tabi ka kudhalilishana. Ukiniuliza maswali eti kwa nini hawakumpa maziwa mara baada ya kugundua amepewa sumu...sasa mimi unataka nikujibu nini. Ninachojua ni kwamba hiyo sumu iliharibu sehemu za utumbo wako kama nilivyoeleza ndio maana akafanyiwa operashion. Tuwe tunaheshimu mchango wa mawazo ya wenzetu kuliko kukandia na kuingiza ukabila kwa waota habari kama baadhi ya memmbers hapa mlivyonishambulia. Ukweli utakuja julikana na mimi naamini nilichokisema kitaibuka kuwa cha kweli na hakuna yeyote hapa atakayekubali kwamba nilishakisema. Mimi nitaendelea kudondosha habari kila nitakavyozipata.
"BALALI YUKO KWENYEHOTEL NDOGO YA MTAANI NA SI RAHISI KUMPATA KWASABABU HOTEL HIYO SI POPULAR SANA" hayo ni kati ya niliyoyataja kwenye thread yangu ya awali na yametoka kwa huyo mwanafamilia wake. Tuache ubishi usio na sababu bali tudadisi.

Sisi wabongo ni wafalme wa conspiracy theories,isay!....Karume aliuawa na Salim,Kolimba aliuawa na CCM,Kombe aliuawa na usalama wa taifa,Ippi Malecela aliuawa na Nchimbi,Rutihinda nae alitiliwa sumu na serikali,Sokoine nae aliuawa na wahujumu uchumi,Kighoma Malima nae aliuawa na serikali....hata Mwalimu wanasema aliuawa, na sasa Balali....the list is endless.
 
Sisi wabongo ni wafalme wa conspiracy theories,isay!....Karume aliuawa na Salim,Kolimba aliuawa na CCM,Kombe aliuawa na usalama wa taifa,Ippi Malecela aliuawa na Nchimbi,Rutihinda nae alitiliwa sumu na serikali,Sokoine nae aliuawa na wahujumu uchumi,Kighoma Malima nae aliuawa na serikali....hata Mwalimu wanasema aliuawa, na sasa Balali....the list is endless.

Mkuu Zanaki,

Heshima yako, wengi kati ya uliowataja hapo juu ambao ni marehemu tumepewa dataz zao za jinsi walivyokuwa-Kolimbad, sasa tatizo la wananchi kama wewe huwa wanakataa bila dataz ndio mana huwa tunawaaamini the kings wa Conspiracy Theories, maana angalau huwa wana dataz ku-back up their therioes, sasa once for a change vipi ukitupatia dataz juu ya vifo vyao maana tumeshapewa the otherside tayari!

It is about time tukaanza kusema na dataz, na kunyamaza kama hatuna maana ninazimani 110% dataz za Jasusi on ex-Gavana, kama unazo tofauti wekahapa kama huna kaaa pembeni ule dataz maana hii ni JF, kama wewe huna wengine wanazo!
 
Consiparcy theories are born of people getting half information and connecting the dots. Lakini huwa katika conspiracy theory yoyote kile kuna some level of truth. To what extent that depends.
I think that we should explore the possibility of Balali being poisoned, kama hiyo sumu aliipata Bongo kwa nani na ilikuwaje. Mimi napenda kujua zaidi kuhusu symtoms zake. Kama alitapika mara baada ya kurudi inaweza kuwa sumu fulani fulani etc. Kuna madaktari wanaweza kutusaidia kuchambua. Hivi kuna mtu amejaribu kupiga ile namba ya Balali iliyoandikwa hapa? Sidhani kama ni kitu kigumu hivyo kumpata mtu Marekani.
Mimi binafsi naamini Balali alienda kwa ridhaa ya serikali lakini sasa hivi hawaaminiani. Kila mtu anajaribu kuangalia maslahi yake. Balali hawezi kukubali wamharibie jina wakati walihakikishiwa protection! Hapo patamu! Tunasubiri hiyo bestseller itoke!
 
Mkuu Zanaki,

Heshima yako, wengi kati ya uliowataja hapo juu ambao ni marehemu tumepewa dataz zao za jinsi walivyokuwa-Kolimbad, sasa tatizo la wananchi kama wewe huwa wanakataa bila dataz ndio mana huwa tunawaaamini the kings wa Conspiracy Theories, maana angalau huwa wana dataz ku-back up their therioes, sasa once for a change vipi ukitupatia dataz juu ya vifo vyao maana tumeshapewa the otherside tayari!

It is about time tukaanza kusema na dataz, na kunyamaza kama hatuna maana ninazimani 110% dataz za Jasusi on ex-Gavana, kama unazo tofauti wekahapa kama huna kaaa pembeni ule dataz maana hii ni JF, kama wewe huna wengine wanazo!

Huo ni udikteta sasa! Sina haja ya kuwa na data zaidi ya nilizosema,na sijakataa kitu.Nani hapa alikuja na death certificate inyoonyesha cause of death ku proove their point? Hizi ndio data,kama za yule mrusi wa Polonium.

Hata mimi naweza kuzua tu kuwa mjomba wangu alilogwa na shemeji yake,sasa hio utiita ni data kwa sababu aliye kufa ni mjomba wangu na mimi ndio niliyosema?
Huwezi kumwambia mtu akae pembeni simply because u do not agree with what he says,what i sed is my opinion,si sikutegemea kuwa kila mtu atakubalina na mimi,na ndio maana tunakuwa na mijadala,na wengi tumejifunza mambo mengi sana humu.Mimi nimetoa mifano ya watu wote 'waliouawa' sikusema mtu yeyote ni muongo.Kama hii ni JF na wewe una data,basi lete death certificate zinazoonyesha sababu za vifo hivyo,hizo ndio dataz! Zilizobaki ni speculations tu ambazo 90% ya watu humu wanatoa,and theres nothing wrong with that.
Lakini hii biashara ya kupigana mikwara eti mtu akae pembeni kama hana dataz ni mambo ya kizamani,na pia ita deter watu ambao maybe they have something to say,lakini wanajua kuna watu kama wewe watawaambia wakae pembeni.
This is a free society,if what i say is crap to u then treat it like so,lakini i'm sure kuna mwingine ataona sio crap..or rather dont read whatever that has been posted by Zanaki,lakini ujue pia kuwa i have the same rights in here as u do
....mimi na wewe ni members tu,none of us owns this forum.
 
Back
Top Bottom