Bora Hayati Dkt. Magufuli, haya yamerudi tena!

Filosofia ya Rorya

JF-Expert Member
Sep 20, 2021
3,214
3,587
Magazeti dada mawili ya The Citizen na Mwananchi yameripoti ukwepaji kodi wa kupindukia (Tzs.3.3 tr) huku tukikuza deni la taifa kwa kukopa hadi Mhimili wa Bunge unastuka. Magazeti haya yamejizolea sifa lukuki kwa uandishi wenye weledi.

Kauli ya Rais ni Sheria

Kaulimbiu ya kila mtu ale kwa urefu wa kamba yake inaligharimu taifa na kuleta madaraja ya maisha (stations or life) yanayostawisha matabaka kwenye jamii.

Hivi sasa watu wanakula mlo mmoja maana unga umetinga 2000/ kg, maharagwe 4000/ kg, mchele wa gredi ya chini 3000/ kg, sukari tangu enzi ya Dr. Omar VP imeshinda awamu zote 4 kushusha bei.

Mafuta ya kula hivi sasa ni anasa, watu wanakula chukuchuku kwenye nchi inayolima mawese, pamba, mahindi, karanga, minazi, ina samaki na wanyama vyote hivyo vinatoa mafuta ya kula.

Nchi inaenda kwenye uchaguzi bila agenda. Vyama havina agenda ilhali wananchi wana agenda ambayo vyama haviioni.

Haiyumkiniki kwamba hata miradi ya kimkakati ya maendeleo imekwama kumalizika kuelekea 2025 licha ya ela iliyokopwa Tzs.42 tr ni zaidi ya thamani-jumla ya miradi yote mikubwa.

Znz kuna paa hadi umeme wanaopewa hauwatoshi wamelazimika kuomba waongezewe kiwango cha umeme.

Znz hiyo hiyo bei ya bidhaa na huduma zimebaki kuwa himilivu wkt bara uwezo wa mlaji kununua (purchasing power) umeanguka hadi kula mlo mmoja. Znz na Tz Bara ni nchi moja.

Gazeti 1.jpg
Gazeti 2.jpg
 
Sasa kama awamu ya Mwendazake watu walikuwa hawakwepi Kodi ilikuaje kuaje Bajeti ikawa imeganda?

Yaani Ajira zilimshinda
Mishahara ilimshinda
Sekta zingine ziliparalyse etc.

Sasa inawezekanaje watu wanakwepa zote hizo yet miradi inafanyika mipya na zamani,Ajira Kila siku,Mishahara na stahiki za Watumishi zinalipwa kama pension nk?

Who is better Kwa muktadha huo?
 
Sasa kama awamu ya Mwendazake watu walikuwa hawakwepi Kodi ilikuaje kuaje Bajeti ikawa imeganda...
Hizo unazosema zinafanyika kwa mkopo ujuwe toka Breton Woods nk.

Ukiwa uchumi wa kati unatakiwa kuwa na vyanzo vya ndani imara vya mapato (ndicho alichofanya JPM. Opportunity Cost. Yaani hiki kisubiri, kile twende nacho sasa).

Hakuna miradi mipya mikubwa ya kimkakati iliyobuniwa awamu ya sita. Miradi kama shule, zahanati, matundu ya vyoo, Johnson Johnson ni ya kawaida tu na haina legacy kwa sababu kila awamu lazima ivijenge maana Watanzania wanazidi kuzaliana.

Aidha, hiyo ni miradi midogomidogo ambayo ni saizi ya Diwani kujenga, siyo hata Mbunge.
 
Ndo wanachokipenda Wabongo
Juma lililopita Bunge la Jamhuri ya Kenya kupitia Kamati yake ya Bajeti limeishauri serikali kuachana mara moja na mpango wa IMF wa kufufua uchumi wa taifa hilo kwamba mpango huo utaizika Kenya kabisa kimaendeleo.

Mataifa makubwa yanayoratibu taasisi hizi za kibeberu (Breton woods) ndiyo yalimuweka Ruto madarakani kwa kuingilia mambo ya ndani ya Jamhuri huru ya Kenya (uchaguzi) hata wakati uchaguzi ulipokuwa mikononi mwa Mahakama ya Upeo.

Jambo liwapo Mahakamani halipaswi kuingiliwa na mtu au taasisi.

US ilimtuma Sen. Chris Coons kuingilia masuala ya ndani ya Jamhuri huru ya Kenya kwa kujipa dhima, dhamana na wajibu wa Mahakama ya Kenya kusuluhisha mkwamo wkt hata rais mstaafu wa Botswana Festus Mogae aliipisha Kenya ifanye mambo yake ya ndani ambayo yalikuwa hayajafikia hatua ya usuluhishi na upatanishi (hata matokeo rasmi ya kura yalikuwa bado).

Rais Festus Mogae alitumwa na Jumuiya ya Madola lakini busara ilimuongoza kujiondokea ili kutunza heshima yake na ya nchi yake..
 
Sasa kama awamu ya Mwendazake watu walikuwa hawakwepi Kodi ilikuaje kuaje Bajeti ikawa imeganda?

Yaani Ajira zilimshinda
Mishahara ilimshinda
Sekta zingine ziliparalyse etc.

Sasa inawezekanaje watu wanakwepa zote hizo yet miradi inafanyika mipya na zamani,Ajira Kila siku,Mishahara na stahiki za Watumishi zinalipwa kama pension nk?

Who is better Kwa muktadha huo?
Ushangae watu sijui hamjui huyu mnaomsema ungekuta sasa hivi hata kusalimiana isingekuwepo
 
Back
Top Bottom