Hivi karibuni kampuni ya NMB ilidhamini mafunzo ya ukocha wa awali yanayotolewa na Chama Cha Soka Wilaya ya Kinondoni (KIFA). NMB ilitoa tracksuits, mipira, pamoja na raba kwa ajili ya washiriki wa hayo mafunzo. Cha kushangaza ni kwamba mafunzo yameanza zaidi ya wiki sasa na hakuna kifaa hata kimoja kutoka NMB kinachotumika na wanamafunzo, hii maana yake nini? Je ndo kusema hivyo vifaa ndo mali ya KIFA? Je NMB wanataarifa kwamba vifaa vyao havitumiki kama ilivyokusudiwa? Ni lini tutaachana na hizi njaa za ajabu ajabu????????