Bongo flavour hatarini kutoweka

Makupa

JF-Expert Member
Apr 11, 2011
5,002
2,536
Nimefuatilia kwa muda sasa studio ambazo kazi yao kubwa ni kuuza kazi za wasanii hususani nyimbo.Nilichogundua ni kwamba kwa kila cd mia moja zinazouzwa thamani ni za nyimbo za dini ,hivyo kuna kila dalili ya kuwa muda si mrefu mziki wa kizazi kipya utatoweka kabisa Wadau naombeni mtupe mawazo ni jinsi gani ya kuokoa hili jahazi linalozama hasa ukitilia maanani ya kuwa mziki wa kizazi kipya ni chanzo cha ajira
 
Nimefuatilia kwa muda sasa studio ambazo kazi yao kubwa ni kuuza kazi za wasanii hususani nyimbo.Nilichogundua ni kwamba kwa kila cd mia moja zinazouzwa thamani ni za nyimbo za dini ,hivyo kuna kila dalili ya kuwa muda si mrefu mziki wa kizazi kipya utatoweka kabisa Wadau naombeni mtupe mawazo ni jinsi gani ya kuokoa hili jahazi linalozama hasa ukitilia maanani ya kuwa mziki wa kizazi kipya ni chanzo cha ajira
wabongo fleva hawategemei sana kuuza cd ili kupata mshiko.
deal ni kutoa single kali na iki hit basi utakula mialiko ya kumwaga kupiga show(kwa wiki show kama 4 kila show anadaka kuanzia kilo5 kuendelea), single ikipoa ndio imetoka unakuna kichwa upya
wanadini wao waisikilizaji wao wananunua zaidi sababu hawapigi sana mashow ya kibiashara
huo ndio mfumo wa soko la muziki bongo
 
Kwani wanamziki wa bongo na shombeshombe bob junior yupo? Kama naye mbongo flavor sishangai kushuka au kuja kufa kwa bongoflavor,oyoyooooo na nana na nini na nana nanini crap
 
BOB JUNIA, CPWAA, DIAMOND, sijui MAVOKO, BARNABA, AMINI, BEKA, KASSIM..HAWA NDIO WAANZE KUTOWEKA...WANA ACT KAMA MASHOGA! KUNA SIKU NILIMSIKIA KASSIM AKIJITAMBA KUWA SHOOTING YA WIMBO WAKE IMEKULA M11, DUH!!! CHEZEA M11 WEYE!!! ANAIJUA IKOJE?
 
Kifo hakitibiki na mauti hayana dawa ndugu zangu,kifo cha huu mziki unaitwa bigji kpo na ipo siku utakufa tu...wanasaidia nini zaidi ya kuwaharibu wanetu kifikra?eti kioo cha jamii,sharobaro awe kioo wa nani..nauliza awe role model wa nani?wafe kabisa wala sitaki kuwaskia
 
duh! Lakini bongo game linachange mara taarab,mduara,charanga yani vaisvesa sasa hivi kuna vigodoro dj shushu na msagasumu nyie wa kishua hamwajui hawa
 
Na ife tu bongo flava, hawana ubunifu, wanajiweka kimagharibi zaidi.

Mimi bado tu niko na wazee wa msondo na sikinde, ndio wanipao raha ya muziki miaka yote.
 
Kifo hakitibiki na mauti hayana dawa ndugu zangu,kifo cha huu mziki unaitwa bigji kpo na ipo siku utakufa tu...wanasaidia nini zaidi ya kuwaharibu wanetu kifikra?eti kioo cha jamii,sharobaro awe kioo wa nani..nauliza awe role model wa nani?wafe kabisa wala sitaki kuwaskia

Ndoto za Mchana!!!

Kila zama na mambo yao...kwa vijana wa kileo, mambo yao ni bongo fleva..hata kama unaona haikufunzi kitu, ni wewe...wenyewe inawafunza na wanao role models wao..tazama kama mnyoo wao wa kiduku jinsi ulivyobamba...all over sasa ni kiduku mpaka ma-footballer wa Europe ni hivyo hivyo...ndiyo zama zao hizi kaka...kama nyinyi mlivyokuwa na zenu za panky, denge n.k.

We kama hutaki kuwasikia basi kufa na kijiba chako cha roho...wapo, na wataendelea kuwapo...Alianza Saleh Jabir kwenye early 1990s akiimba kwa mabiti ya uzunguni na america, wakati huo tulidhani hizo ni tafsiri za nyimbo za kimarekani kumbe ni instrumental ikatiwa mashairi ya kiswahili...kama unaikumbuka OPP(naughty By nature) n.k.

Muziki ukakua(call it evolution) pale studio za kutengeneza music kwa computers zilipoanza...wakati huo wengine wakajiita wana-hip hop(Rap) na majina kama walume ndago, wagumu nk yakawa ni common, hip hop ilipoonekana kufikia saturation, vijana wakabuni mchanganyiko wa hip hop na kuimba(hapo ukawaona kina juma nature wakiimba lakini kiugumu ugumu bila kubana pua), vijana walipogundua kubana pua kuna ladha yake wakaanza kubana pua one-way mpaka leo tuna akina Diamond ukipenda muite Platinum, wabana pua mahiri, Ally Ulaya(Kiba), Barnaba nk...

kwa ujumla ni kuwa muziki ni utamaduni, na ilivyo kila utamaduni una watu wake..ili utamaduni huo ufe ni mpaka pale wenye-utamaduni huo watakapotoweka na bahati mbaya kwako ndugu ni kuwa hilo halitotokea kwa sababu tu wewe na wengine wenye mawazo mafupi kama yako mngetamani litokee...POLE!!!

Nawasilisha!!!
 
Kifo hakitibiki na mauti hayana dawa ndugu zangu,kifo cha huu mziki unaitwa bigji kpo na ipo siku utakufa tu...wanasaidia nini zaidi ya kuwaharibu wanetu kifikra?eti kioo cha jamii,sharobaro awe kioo wa nani..nauliza awe role model wa nani?wafe kabisa wala sitaki kuwaskia
 
Mkuu Legagnat,

Ni kweli kabisa nyimbo za hawa BF hazina ujumbe zaidi ya kujisifu sifu na umagharibi kibao.Mimi ikifika Ijumaa nakaa na redio yangu nasikiliza hizi nazo kujamaa mmoja anachambua historia za wanamuziki wa zamani hadi unafurahi.Ujumbe na maudhui ya nyimbo za zamani karibu zote ulizingatiwa sana siku hizi hakuna ujumbe.


Na ife tu bongo flava, hawana ubunifu, wanajiweka kimagharibi zaidi.

Mimi bado tu niko na wazee wa msondo na sikinde, ndio wanipao raha ya muziki miaka yote.
 
Tena kabla ya kufa inatakiwa ipigwe ban kabisa. Hakuna wanalofanya zaidi ya kuongea ongea pumba tu, bora nginde na msondo .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom