TANZIA Bondia George Foreman afariki dunia

TANZIA Bondia George Foreman afariki dunia

Gumilapua

JF-Expert Member
Joined
Sep 13, 2011
Posts
935
Reaction score
733
Moja Kati ya mabondia mahili wa uzani wa juu kuwahi kutokea huwezi kumsahau George Foreman.
Jana siku ya ijumaa mwamba ametutoka, ulimwengu wa ngumi na Sisi tuliopata walau bahati ya kupanda ulingoni hakika hatutamsahau huyu mwamba.

Machache Tu kuhusu George ni bondia anaeminika kuwa na ngumi nzito Sana, Kwa Hili Joe Frazier analifahamu baada ya kuvuliwa ubingwa wa dunia ndani ya raundi mbili na kuanguka chini (knockdown) mara 6.
George ndie bondia Mzee kuliko wote wa uzito wa juu kuwahi kutwaa ubingwa wa dunia akiwa na miaka 46 akimvua ubingwa Michael Moore aliekuwa na miaka 26 wakati huo. Moore alikuwa ndio ametoka Tu kumvua ubingwa Evander holyfield.

Zaidi ya hayo George ni bondia pekee kurudi ulingoni baada ya kustaafu Kwa miaka 20 na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa dunia.

George alichukua medal ya dhahabu ya olympic akiwa amepigana mapambano 26 Tu tangu angie kwenye masumbwi.
Utakumbukwa daima.
"The Big George Foreman"
 

Attachments

  • 18c4e61d13fd42e1932f1b105466ff8d.jpg
    18c4e61d13fd42e1932f1b105466ff8d.jpg
    58.8 KB · Views: 28
Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.
 
Rumble in the jungle....
October 30, 1974 Zaire

Hili lilikua pambano lake dhidi ya Mohamed Ali...
Kule Zaire (DRC) jamaa alifanywa achukiwe sana maana Mohamed Ali aliwaambia wacongoman kua George Foreman ni mbeligiji hivo Ali atampiga ili kulipiza kisasi cha wabeligiji kuwatesa wacongoman kumbuka wabeligiji ndo walikua wanaitawala Kongo...

Siku ya pambano Mohamed Ali alikua na mashabiki rundo wote wakiimba Ali mpige mbeligiji huyo.. "Ali boma ye..."

Na kweli jamaa alikula kichapo kama kahaba aliyefumaniwa...
1001_1200x.jpg
 
Rumble in the jungle....
October 30, 1974 Zaire

Hili lilikua pambano lake dhidi ya Mohamed Ali...
Kule Zaire (DRC) jamaa alifanywa achukiwe sana maana Mohamed Ali aliwaambia wacongoman kua George Foreman ni mbeligiji hivo Ali atampiga ili kulipiza kisasi cha wabeligiji kuwatesa wacongoman kumbuka wabeligiji ndo walikua wanaitawala Kongo...

Siku ya pambano Mohamed Ali alikua na mashabiki rundo wote wakiimba Ali mpige mbeligiji huyo.. "Ali boma ye..."

Na kweli jamaa alikula kichapo kama kahaba aliyefumaniwa...View attachment 3279887
Lile songi la The_game_Ali_bomaye ndo hii kumbe
 
Goerge Foreman alikuwa Bondia Hatari sana kukutana nae, na alikuwa na stamina moja hatari...yaani kumuangusha ni kipengele...na alikuwa na ngumi jiwe

Hakika katika ngumi huyu ni LEGEND level ya kina Mohamed Ali

Mungu awafariji Ndugu, jamaa, Marafiki na wapenda Ndondi wote.
 
Rumble in the jungle....
October 30, 1974 Zaire

Hili lilikua pambano lake dhidi ya Mohamed Ali...
Kule Zaire (DRC) jamaa alifanywa achukiwe sana maana Mohamed Ali aliwaambia wacongoman kua George Foreman ni mbeligiji hivo Ali atampiga ili kulipiza kisasi cha wabeligiji kuwatesa wacongoman kumbuka wabeligiji ndo walikua wanaitawala Kongo...

Siku ya pambano Mohamed Ali alikua na mashabiki rundo wote wakiimba Ali mpige mbeligiji huyo.. "Ali boma ye..."

Na kweli jamaa alikula kichapo kama kahaba aliyefumaniwa...View attachment 3279887
Na hili ndio lilikua pambano la kwanza jamaa kuanguka e? Humu ndio ile style ya ya rope-a-dope ya Ali ilifanya kazi sana... Malegend wote wanapukutika sasa.
 
Na hili ndio lilikua pambano la kwanza jamaa kuanguka e? Humu ndio ile style ya ya rope-a-dope ya Ali ilifanya kazi sana... Malegend wote wanapukutika sasa.
Halafu DON KING bado yupo tu...Daah
 
Huko juu wanasema bado mwakinyo
🙌🙌🙌🙌
Huyu jamaa ameacha legacy kubwa kwenye boxing, sasa kumtaja simbilisi kama Mwakinyo wakati tunamzungumzia Mwamba ni kumkosea heshima legend wetu. 😁😁
 
Halafu DON KING bado yupo tu...Daah
Hata hivyo aliwaweka kwenye ramani ya dunia ya masumbwi watu wengi sana... Kiufupi aliwapa maisha😅😅😅 kwahiyo wacha aendelee kuvuta pumzi kwanza
 
Rip legend.
Niliwahi kumuandika hapa ilipotimia miaka 50 ya pambano lake la rumble in the jungle.
 
Back
Top Bottom