TANZIA Bondia George Foreman afariki dunia

TANZIA Bondia George Foreman afariki dunia

Hata hivyo aliwaweka kwenye ramani ya dunia ya masumbwi watu wengi sana... Kiufupi aliwapa maisha😅😅😅 kwahiyo wacha aendelee kuvuta pumzi kwanza
Yeah ila alimpiga za macho Mike Tyson,

Tyson angekuwa Bilionea akiwa chalii mdogo sana akiwa na Don
 
Moja Kati ya mabondia mahili wa uzani wa juu kuwahi kutokea huwezi kumsahau George Foreman.
Jana siku ya ijumaa mwamba ametutoka, ulimwengu wa ngumi na Sisi tuliopata walau bahati ya kupanda ulingoni hakika hatutamsahau huyu mwamba.

Machache Tu kuhusu George ni bondia anaeminika kuwa na ngumi nzito Sana, Kwa Hili Joe Frazier analifahamu baada ya kuvuliwa ubingwa wa dunia ndani ya raundi mbili na kuanguka chini (knockdown) mara 6.
George ndie bondia Mzee kuliko wote wa uzito wa juu kuwahi kutwaa ubingwa wa dunia akiwa na miaka 46 akimvua ubingwa Michael Moore aliekuwa na miaka 26 wakati huo. Moore alikuwa ndio ametoka Tu kumvua ubingwa Evander holyfield.

Zaidi ya hayo George ni bondia pekee kurudi ulingoni baada ya kustaafu Kwa miaka 20 na kufanikiwa kutwaa ubingwa wa dunia.

George alichukua medal ya dhahabu ya olympic akiwa amepigana mapambano 26 Tu tangu angie kwenye masumbwi.
Utakumbukwa daima.
"The Big George Foreman"
Ungeliweka na historia yake ya kuzaliwa.
Tujue mwaka na uraia, pia nini kimemsibu kupelekea kifo chake?
 
Rumble in the jungle....
October 30, 1974 Zaire

Hili lilikua pambano lake dhidi ya Mohamed Ali...
Kule Zaire (DRC) jamaa alifanywa achukiwe sana maana Mohamed Ali aliwaambia wacongoman kua George Foreman ni mbeligiji hivo Ali atampiga ili kulipiza kisasi cha wabeligiji kuwatesa wacongoman kumbuka wabeligiji ndo walikua wanaitawala Kongo...

Siku ya pambano Mohamed Ali alikua na mashabiki rundo wote wakiimba Ali mpige mbeligiji huyo.. "Ali boma ye..."

Na kweli jamaa alikula kichapo kama kahaba aliyefumaniwa...View attachment 3279887
Narekebisha mambo mawili Tu kwenye post yako:
1.Ali aliwaambia Wacongoman kuwa George ni kibaraka wa wazungu na sio wabelgiji
2.kwenye picha uliotumia hapo juu ni pambano la pili Kati ya Mohammed Ali na Sony Liston, unaweza kuona Ali akiwa bado kijana mbichi kabisa. Kwenye Rumble in the jungle Big George alivalia bukta nyekundu ambayo aliivaa tena alipouchukua tena ubingwa wa dunia dhidi ya Michael Moorer.
Mengine yote upo sahihi sina shida nayo🙏🙏
 
Ungeliweka na historia yake ya kuzaliwa.
Tujue mwaka na uraia, pia nini kimemsibu kupelekea kifo chake?
George Foreman aka the Big George alizaliwa huko Marshall Texas tarehe 10 Jan 1949 ni mmarekani mweusi.
Jumla alupigana mapambano takriban 81 kama professional boxer alishinda 76 na Kati ya hayo 68 ni Kwa knockout. Halafu Leo anakuja mjinga mmoja anapigana Mapambano 50 Tu tena ya kujichagulia wapinzani halafu uzito ndogo wa light weight anataka aonekane mkubwa kuliko hawa miamba.
Hapa namzungumzia Floyd Mayweather jr.
Huyu mwamba baada ya kupigwa bila kutarajia na Mohammed Ali akataka rematch Ali akawa anamkwepa, ili kuuaminisha umma kuwa bado ni wa Moto akawa Anandaa mapambano ya kupigana na mabondia Hadi 4 Kwa wakati mmoja na wote aliwachenyenta. Ila politics za ngumi kipindi kile zilimkataa na hazikumpa nafasi ya kugombea tena ubingwa wa dunia. Akawa frustrated na mwishoe akaishia kupigwa Kwa point na Jimmy Young na baada ya pambano Hilo la 1977 akatangaza kuokoka na kustaafu rasmi masumbwi na akaamua kumtumikia Mungu kama mhubiri. Miaka kumi baadae 1987 akarudi tena ulingoni na 1997 akawa bingwa tena wa dunia kabla ya kustaafu rasmi na kuendelea na uinjilisti wake. Ujasiliamali pamoja na uandishi wa vitabu na comedy kidogo.
Sababu za kifo chake bado hazijawekwa wazi ila familia yake imesema alifariki Kwa Amani huku akiwa amezungukwa na familia yake.
RIP the Big puncher George.
 
Back
Top Bottom