Bomoabomoa Dar yatua rasmi Temeke - Keko wapewa notisi...

Bomoabomoa Dar yatua rasmi Temeke - Keko wapewa notisi...

Maelekezo waliyopewa ni kuhakikisha wale wote waliojenga mabondeni , kwenye viwanja vya wazi , juu ya bomba kubwa la majitaka wabomoe nyumba zao kabla ya tarehe Januari 5 .

Hii notisi imebandikwa jana na imesainiwa na mkurugenzi wa manispaa ya Temeke ( nimeiona ).

Wahanga ni pamoja na waliojenga nyuma ya gereza la Keko , Keko Mwanga , Keko Machungwa hasa wale waliojenga kandokando ya mfereji wa maji unaoanzia kota za polisi maarufu kama Mchomba line , wakazi wa Keko juu nao hawajasahaulika hasa walio chini ya Kisiwani bar , tuendelee kutega sikio .


KWA KWELI HUU NI UONEVU WA HALI YA JUU KWA NCHI ZA WENZETU HII HALI HAIKUBALIKI .WATU HAWA WOTE WALIACHIWA KUJENGA KWA MIAKA KADHAA LEO WANARUDI KUWAHUJUMU MAISHA YAO . NYUMBA ELFU 3 NA KUENDELEA NI NYINGI SANA TUJAALIE KILA NYUMBA WANAISHI 3 HAPA TUNAPATA WATU ELFU 9 MBALI WATOTO NADHANI HAPA MH MAGUFULI ANAHUJUMIWA NA WANATAKA KUMHARIBIA UONGOZI WAKE .

NATOWA WITO KWA WANYONGE WOTE WANAOKABILIWA NA JANGA HILI WAUNGANE PAMOJA KAMA NI MAANDAMANO AU NJIA NYENGINE YOYOTE WASIMAMIE HAKI YAO .

HII SI MOVE YA KUSAPORT KWA KWELI .
 
KWA KWELI HUU NI UONEVU WA HALI YA JUU KWA NCHI ZA WENZETU HII HALI HAIKUBALIKI .WATU HAWA WOTE WALIACHIWA KUJENGA KWA MIAKA KADHAA LEO WANARUDI KUWAHUJUMU MAISHA YAO . NYUMBA ELFU 3 NA KUENDELEA NI NYINGI SANA TUJAALIE KILA NYUMBA WANAISHI 3 HAPA TUNAPATA WATU ELFU 9 MBALI WATOTO NADHANI HAPA MH MAGUFULI ANAHUJUMIWA NA WANATAKA KUMHARIBIA UONGOZI WAKE .

NATOWA WITO KWA WANYONGE WOTE WANAOKABILIWA NA JANGA HILI WAUNGANE PAMOJA KAMA NI MAANDAMANO AU NJIA NYENGINE YOYOTE WASIMAMIE HAKI YAO .

HII SI MOVE YA KUSAPORT KWA KWELI .

mlizoea kuishi kwa mazoea bila kufuata sheria sasa mnatumbuliwa mnaanza kulia lia...
 
mlizoea kuishi kwa mazoea bila kufuata sheria sasa mnatumbuliwa mnaanza kulia lia...
MKUBWA HII NCHI WATENDAJI WA SERIKALI NDIO WALIOKOSA KUFATA SHERIA KWA KWELI HAIWEZEKANI MTU ANAJENGA NYUMBA MPAKA ANAMALIZA SHERIA HAIJAFATA MKONDO WAKE . KWA NCHI AU SERIKALI ZINAZOFATA SHERIA HUWEZI KUTA HALI KAMA HII INATOKEA.

HIZI NYUMBA ZA WANYONGE HAZIKUSIMAMA SIKU MOJA WAPO WAPI WAHUSIKA HAPA UNAKUTA KUNA WAZIRI NA WIZARA NA WAFANYAKAZI WANALIPWA MISHAHARA KWA KUSIMAMIA WIZARA YA NYUMBA ,BARA BARA NA MIPANGO YA MJI NA HII HAIKIUJA JUZI JANA .
HAWA NDIO WA KUWAJIBISHWA KABLA KUWAVUNJIA WANYONGE MAJUMBA YAO. HEBU FIKIRIA RAIS AMA WAZIR MKUU ANAWAAGIZA WAFANYA BIASHARA WALIOKWEPA KODI WARUDISHE KODI WALIZOKWEPA KIUTENDAJI HAYA NI AIBU ILIOPINDUKIA .PALE KUNA WAFANYAKAZI WANALIPWA MISHAHARA MIKUBWA KWA AJILI YA KUKUSANYA KODI NA MAMBO MENGI INAKUAJE MTU ANAKOSA KULIPA KODI MPAKA ANAKUJA RAIS AMA WAZIR MKUU ?

HAPA NIPO TULIPOKOSEA NA SIO KUKURUPUKA KUWAONEA WANYONGE .MKUU WACHA KUFURAHIA UJINGA HII MOVE INGEKUA NZURI KWA KUANZA KUWACHUKULIA HATUA WATENDAJI WA SERIKALI WALIOKOSA KUFANYA KAZI ZAO .
 
Mkandara hicho kipande chako chatosha. Kama mtu hataki basi asaga chupe kisha---


Umeongea ukweli ila kuna mambo usiyoyajua.... Kwa hili suala pande zote mbili kwa maana watumishi wa serikali wenye mamlaka ya kusimamia mazingira na wananchi waliojenga kwenye maeneo yasiyoruhusiwa wana makosa.... Ni makosa makubwa mno kuendelea kusema wananchi hawajavunja sheria na mzigo kuwatupia watumish tu..

Ukumbuke kutokujua sheria sio sababu ya kutokutiwa hatiani... wananchi kujenga kwa kutokujua maeneo yasiyoruhusiwa si sababu ya kutobomolewa nyumba zao... Nenda kasome sheria ya mazingira inasemaje na sio kuongea ongea tu...

Cha msingi ni watanzania tuache kuishi kimazoea kama ilivyokawaida yetu... tufuate sheria kwenye mamlaka husika ambazo wanalipwa kodi zetu ili kutufanyia kazi.....

Mind you simaanishi kuwa mamlaka husika hazihusiki
 
hapo wanafunzi wengi wa DUCE watapatkana tu! maana mabondeni wengi wao ndio wanakopatikana na vyumba ni bei rahisi
 
Nona wewe ni mwenyeji mno keko, vp yule mzee kachimbe ubungo tupo?,napakumbuka miaka ya 70 mpaka 80, kekoilikuwa imenyooka, nikaja kupita hapo last year nilihuzunika, nakumbuka tikipita ile changombe road asubuhi ilikuwa kimya watu wakijiendea viwandani, na ile Gloria bakery naona imesha kufa pale keko magurumbasi, kulikuwa na bobby soap factory nayo imebaki mifupa huko iliko
Kaka bobby soap ni toroli now anamilik bakhresa anaifaz azam embe na energy drink
 
Jamani vp mliopo dar leo mahakama imeamua vp kesi iliyofunguliwa juu ya nyumba za mabondeni?
 
2020 CCM watajuta na watakuwa wadogo kama "piritoni" na kila goti watapiga lakini haitasaidia.

Tusubiri maana wao wanadhani by 2020 watu watakuwa wamesahau haya wanayoyafanya leo bila huruma.

Nyimbo na mashairi yao havitofua dafu mbele ya kumbukumbu ya mateso na machungu haya.It will always be a bitter memory that won't easily go away.
2020 CCM watajuta na watakuwa wadogo kama "piritoni" na kila goti watapiga lakini haitasaidia.

Tusubiri maana wao wanadhani by 2020 watu watakuwa wamesahau haya wanayoyafanya leo bila huruma.

Nyimbo na mashairi yao havitofua dafu mbele ya kumbukumbu ya mateso na machungu haya.It will always be a bitter memory that won't easily go away.
Nyie watu ni wapumbavu sana! Kwa hiyo mlitaka awafumbie macho? Wakibomolewa watu wa Mbezi mnafurahii! Ikifika kwenu mnaanza kulia lia! Mtamkumbuka sana mkwere.

Note; Sheria ni msumeno!
 
Yaani 2020 CCM itapata kura nyingi zaidi kwani watu wengi watakaohama mjini wakati huo watakua na maisha bora sana kijijini kwamba watakua wanamshukuru sana Mgfl .....

Umenichekesha aiseeee.
 
Duuh nakumbuka ilikuwa inamilikiwa na wahindi wawili ndugu, walikuwa wanaitwa virani enzi zile walikuwa na race cars,kwa hiyo sasa sabuni mbunju huko nani anazalisha?,na mbele ilikuwa ddc,vp cosata nayo ipo pale kwenye duka la bora?
 
wakuu pale keko mwanga watabomoa maeneo gani hasa na je watabomoa leo au kesho?
 
Unaweza kuachia iyo notisi tuione
 
siweezi kaa dar zaidi ya wiki maana ni kero kwanza mji unanuka halafu hata mtu alietoka Uru kishumundu jana na gari ya ndizi akikaa wiki tuu anaona kuwa mjanja wa kutupwa
 
Back
Top Bottom