Maelekezo waliyopewa ni kuhakikisha wale wote waliojenga mabondeni , kwenye viwanja vya wazi , juu ya bomba kubwa la majitaka wanaobomoa nyumba zao kabla ya tarehe 5 january , hii notisi imebandikwa jana na imesainiwa na mkurugenzi wa manispaa ya Temeke ( nimeiona )
wahanga ni pamoja na waliojenga nyuma ya gereza la keko , keko mwanga , keko machungwa hasa wale waliojenga kandokando ya mfereji wa maji unaoanzia kota za polisi maarufu kama mchomba line , wakazi wa keko juu nao hawajasahaulika hasa walio chini ya kisiwani bar , tuendelee kutega sikio .