Baadhi ya Watz mnasikitisha sana. Suala la ndege kupata matatizo ya kiufundi ni kitu cha kawaida haijalishi ni pangaboi au jet. Fastjet leo ni siku ya tatu ndo safari zake za kuja Mwanza kwa ndege yao ya usiku ndo zmerudi kwenye ratiba zake za kawaida. Kabla ya hizi siku ndege zao zilipata hitilafu kwa kupokezana ndani ya siku moja. Labda kwakuwa mlio wengi humu mnapita airports wakati wa safari tu. Kwahiyo siku unapopita ukakuta ndege imepata hitilafu kwa siku hiyo,basi mnapiga kelele ndege mbovu eti za ATCL tu !!! Kwanini isiwe Fastjet au Precision Air ambazo nazo zimekuwa zikiharibika tena mara nyingi zaidi kuliko hata ATCL. Naona hizi ni chuki juu ya Magufuri baada ya kuziba na kuvuruga mitandao ya wizi wa pesa za serikali. Tuwe waungwana hata jambo zuri akilitenda adui yako,lipokee kwa mtazamo chanya. Upinzani sio kupinga kila linalotendwa na mpinzani wako,bali ni kujenga hoja. Mnapaswa kumpongeza mh rais kwan baada ya kuja ATCL unyanyasaji uliokuwa unafanywa na Fastjet walau umepungua kidogo japo bado upo,lkn kuna usafiri mbadala walau mtu anaweza kubadilisha ndege kuliko ilivyokuwa awali. Tuwe wazalendo kwa kuvipenda na kuvithamini vyetu ili kuvipa uwezo wa kutia huduma bora zaidi. Nilikuwa napita tuu maana nimewasikia baadhi mmekariri ule ubeti wa viongozi wenu kuwa Rais kanunua ndege mbovu,kitu ambacho ni tungo za wanasiasa wetu tuu.