Bomba za gesi zarudishwa

Bomba za gesi zarudishwa

GNA

JF-Expert Member
Joined
Dec 28, 2012
Posts
246
Reaction score
72
Ndugu zangu nipo maeneo ya kongowe, njia ya kuelekea Mtwara yanapo pelekwa mabomba ya gesi kwa malori, cha ajabu naona malori ambayo siku zote, hubeba mabomba ya gesi kupeleka kusini, mwa nchi kule kunako chimwa gesi, leo naona baadhi ya malori yanatoa manomba mtwara yana leta dar, bado natafiti tatizo nini hadi mabomba haya yanarudi. Labda kunagari imepinduka, au ndo maisha ya 10%. Kwa sababu kilichotokea leo cha kurudisha mabomba kilitokea mwezi wa tisa tena mwaka huu 2013, Ndio maana nimesema nafanya uchunguzi kujuaa tatizo nini? Mabomba haya yameifadhiwa eneo la mbagala mzinga dar es salaam na eneo mwandege wilaya ya mkuranga karibu na kiwanda cha matunda cha Azam huku pwani, nikiwa naandika taarifa hii mengine yamepita sasa hivi saa 15:12pm leo tarehe 30/12/2013, naomba wadau tupeane uelewa, sija lalamika wala kumlaumu mtu yoyote, ila napenda kupata ufafanuzi ili limekaaje. Source mimi mwenyewe.
 
Mengine yapo hapo Mwanambaya pembeni mwa daraja, mengine yapo Msufini, daraja la mto Mbezi, yawezekana hayana viungio, pengine yamepishana diameter, au yamebaki baada ya kutimia na sasa yanarudishwa store.

Kaka usiumize kichwa, mambo ya wenyewe hayo, sisi tusubiri ngonjera.
 
ujazo wa gesi umepungua...ka nyege na shahawa
 
Si kwamba yanarudishwa Dar, bali yanatolewa huko yanakohifadhiwa (base) na kupelekwa site ambako yanaunganishwa na kuzikwa ardhini.

Kumbuka bomba la gesi halipiti hapo yalipohifadhiwa hayo mabomba bali linapitia porini huko. Hivyo ni lazima yasafirishwe kuelekea huko ambako yanatumika.
 
Si kwamba yanarudishwa Dar, bali yanatolewa huko yanakohifadhiwa (base) na kupelekwa site ambako yanaunganishwa na kuzikwa ardhini.

Kumbuka bomba la gesi halipiti hapo yalipohifadhiwa hayo mabomba bali linapitia porini huko. Hivyo ni lazima yasafirishwe kuelekea huko ambako yanatumika.

Sasa kwa nini yalivyoshushwa bandarini DSM yasipelekwe straight kwenye hizo base na badala yake yakawa yanapelekwa kusini? Nadhani ndicho kinachomshangaza mleta mada, kwamba yamepelekwa kusini na sasa yamerudishwa tena Dar au Pwani.
 
Watu wanakula na hela ya trip mkuu, kwani wanajua sana mabomba mangapi yaende wapi na mangapi yabaki wapi.

ONLY IN TANZANIA.
 
Sasa kwa nini yalivyoshushwa bandarini DSM yasipelekwe straight kwenye hizo base na badala yake yakawa yanapelekwa kusini? Nadhani ndicho kinachomshangaza mleta mada, kwamba yamepelekwa kusini na sasa yamerudishwa tena Dar au Pwani.

huyo jamaa yupo kongowe anajuaje kama mabomba yanatoka kusini kwenda dar? angesema amesafiri nayo labda lakini yupo barabarani ana judge tu direction?
 
Yamepitia bandari ya Mtwara hayo mkuu! So ni lazima yasafirishwe kwenda site!
 
Back
Top Bottom