sulphadoxine
JF-Expert Member
- Nov 1, 2010
- 2,257
- 645
BODI ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu(HESLB), imeurarua Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM), kutokana na kile ilichokiita ni kutoa taarifa, "za kizushi na za kukurupuka," na kutaka isigeuzwe jimbo la uchaguzi la wanasiasa.Tamko hilo la HESLB chini ya kichwa cha habari, "Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu haihusiki na Migomo ya hivi karibuni katika Vyuo vya Elimu ya Juu," linajibu mapigo ya tamko la UVCCM, lililotaka mapinduzi ndani ya bodi hiyo ikiituhumu kushindwa kukidhi mahitaji ya wanafunzi wa elimu ya juu nchini.
Hata hivyo, ikitoa ufafanuzi wa tuhuma moja hadi nyingine kati ya zilizoelekezwa kwake, bodi ilipiga kombora ikisema, "mmoja wa viongozi UVCCM, amekitolea mfano Chuo Kikuu kishiriki Mkwawa (MUCE) kama mfano, wakati akitoa tamko la kukurupuka dhidi ya bodi bila hata kufanya uchunguzi wa sababu za ndani za migomo ya wanafunzi wa vyuo."
Vijana hao wa CCM katika tamko lao, walisema, UVCCM umebaini kuna urasimu unaofanywa na watendaji na haiingii akilini, Mkwawa University wagome kwa kutolipwa posho zao na baada ya siku moja walipwe posho zao baada ya kugoma. Jambo hili si utamaduni wa vijana wa Kitanzania, wale wote wanaohusika CCM ichukue hatua,
Hata hivyo, ikitoa ufafanuzi wa tuhuma moja hadi nyingine kati ya zilizoelekezwa kwake, bodi ilipiga kombora ikisema, "mmoja wa viongozi UVCCM, amekitolea mfano Chuo Kikuu kishiriki Mkwawa (MUCE) kama mfano, wakati akitoa tamko la kukurupuka dhidi ya bodi bila hata kufanya uchunguzi wa sababu za ndani za migomo ya wanafunzi wa vyuo."
Vijana hao wa CCM katika tamko lao, walisema, UVCCM umebaini kuna urasimu unaofanywa na watendaji na haiingii akilini, Mkwawa University wagome kwa kutolipwa posho zao na baada ya siku moja walipwe posho zao baada ya kugoma. Jambo hili si utamaduni wa vijana wa Kitanzania, wale wote wanaohusika CCM ichukue hatua,