Bodi ya mikopo haina watu wenye ubunifu katika kazi

kibaravumba

JF-Expert Member
Dec 21, 2012
6,635
7,005
Nimeona orodha ya Taasisi sugu zinzodaiwa kutokupeleka majina ya waajiwa wao wanaodaiwa na bodi.Orodha ndogo niliyoiona ndiyo imenifanya nione hawa jamaa hawafikiri vizuri.

Kama wana sababu yoyote ya msingi wangeweza kuitafutia ufumbuzi mapema.Mfano iwapo wanakazi nyingi na wamezidiwa na kazi,wanashindwa nini kuwaomba wakuu wa wilaya wawasaidie kujua taasisi nyingi zilizomikoani zenye waajiriwa wanaodaiwa mikopo na hawajaanza kulipa?

mathalani zipo shule nyingi binafsi zenye waajiriwa wanaodaiwa mikopo,pia makampuni mfano wakandarasi wa ujenzi,hospitali za binafsi na mashirika ya dini,famasi zote Tanzania ni lazima ili zipewe kibali kuwe na mtu mwenye digrii anayedhamini na ziko zaidi ya 1000 tanzania nzima,baadhi ya NGOs zina waajiriwa wengi sana lakini sijaziona katika orodha na taasisi moja ninayofanya kazi wapo zaidi ya kumi na hawana mpango wa kulipa wala mwajiri hana mpango wa kupeleka majina.

Maoni yangu ni kwamba kama mmeshindwa kazi na mmeshindwa kuwa wabunifu,kwa nini msitumbuliwe wapewe kazi watu wengine ili walipe vizuri madeni yao?
 
Hawa bodi ya mikopo wanajuwa kuna wadaiwa wanawaita sugu ni wale ambao walikuwa wanafunzi hewa na wao walikuwa wanakula hizo hela sasa tuanze na bodi zile hela walizokula nani atalipa? Sijasikia hata siku moja serikali ikiongelea hili. Pia kuna wanafunzi walikuwa wanalipiwa na mashirika mbalimbali lakini bodi wakafanya ujanja wakaingiza majina yao kwenye mikopo na wakawa wanachukuwa wao zile hela na sijasikia wakiliongelea hili suala. Serikali itoe tamko kuhusu hizi hela maana hawa jamaa naona wanakwepa kuongelea haya mambo waliyofanya.
 
Binafsi sioni mdaiwa sugu hapo maana kazi zao kudai watu pesa ila hawafkrii kwenda utumishi kufanya ufumbuzi wa hawa watu kupata ajira kwanza wamalizapo chuo ili iwe rahc kwako kurudisha mkopo au kufanya uchunguzi kazi uyo mtu kwenye bado ni mwajiliwa wa shirika hilo binafc wanakurupuka tu.
Mfano kuna watu wanasugua nyumban miaka 3 hadi 4 unahisi akipata kazi atawaza mkopo au kufanya hali yake kwanza iwe sawaa.
Mwisho: kuna baadh ya tasisi hazifuati policy za kazi na wahusika wapo mwajiri anakaa kazini hata mwaka ajasain contract na hata kuuona hvyo anakuwepo pale kama kibarua huo mkopo anaurudisha vipi.
Maoni yangu kwao: kwanza wajitahidi kuwapa hawa watu ajira au kuwafanyia wepesa wa kuzipata hizo ajira tena za kudumu ndio wawe na uhakika wa mambo km udaiwa kashindw kwa sabb zake binafc pia haya mashirika yasimamiwe ilivyo katika mishahara na kufuata utaratibu wa kuajili siyo tu kuwapa miongoz ili kuifatilia zero
 
Back
Top Bottom