Bodaboda wangapi walilisikia tangazo la Rais?

isitoshe hili lilijulikana kabla hata njia zenyewe hazijazinduliwa. visingizio kwamba hawasikilizi au hawana redio/tv ni kiduchi sana. mbona mengine ya maandamano yanawafikia? wenzao waliogongwa kwa makosa ya kupitisha tukutuku zao hapo hawakupewa maonyo? yule abiria aliyeburutwa uvunguni mwa basi si aliponzwa na dereva asiyejua au aliyekaidi sheria? iweje leo tuendekeze na kulea makosa yatakayogharimu maisha ya wenzetu na vilema vya maisha ati ni kuogoapa sera ya 'wapiga kura' kwani wanaogongwa na kufa/kulemaa sio wapiga kura? tuweke itikadi kando tukemee na kupongeza inapobidi. mizaha na michezo michezo kwa uhai wa binadamu tuuepuke kabisa.
Tuone ni namna gani hawa watu watakavyoweza kupitiwa pia na mnyororo wa mzunguuko wa hela mifukoni mwao, bila hivyo watapita tu hata kama uking'oa matairi yao. Hata wao ni mashahidi wa wenzao walioburutwa na kufa kwenye njia hizo, kama ni kuacha basi wangeacha kwa kuona ajali zinazowapata wenzao. Ukweli vijana hao hawana cha kupoteza kwanza hata hizo pikipiki sio za kwao, kwao wao ni heri wafie barabarani kwa ajali kuliko kufia uvunguni mwa kitanda kwa njaa.
 
Sheria biila shuruti inawezekana

hasa tukizingatia shuruti inamilikiwa na wenye sheria

Tujitafakari kama tunahitaji sheria

Maana kanuni ya sheria ni kukata pande zote
inapokata upande mmoja INAITWAJE?

boda boda ni mimi na wewe

na ule mradi NI WETU

tuwekeane sheria au tufundishane ni uamuzi wetu,

tuamue tu
Ikiwa sheria kazi yake ni kuvunjwa!
Aisee umeongea vitu vya secondary Sana mkuu
 
watanzania wengi taarifa ya habari ni kama kituo cha polisi, ila mpira wahakosi hata kama ni saa 5 usiku.
Kusikiliza taarifa ya habari ni sawa na kuwaambia wakawasikilize wale wale waliowafikisha hapo walipo. Hakuna jipya kwao bora wakajipoze machungu kwa viroba na mpira ili kuzisahau kero zao, wamekata tamaa na kila kitu, wanaona kama vile hata kura zao hazina msaada tena kwao. Kifupi kuhangaika na bodaboda ni sawa na kuhangaika na watu waliokwisha kata tamaa. Kuchomoa tairi lake ni kumrudisha hatua nyingi sana nyuma, na huenda unafanya kosa kubwa la kuua kwa njaa familia yake inayomtegemea. Ni heri wachapwe viboko hadharani kuliko kuhaaribu ofisi/mgodi/kiwanda/kitendea kazi chake.
 
Unaruhusiwa kukatisha upande wapili katika sehemu rasmi iliyowekwa kama vile kwenye zebra, ila unashuka na kukokota pikipikiyako ukisha vuka unapanda, safari inaendelea na hukamatwi.
Nashukuru polisi jamii kwa ufafanuzi wako
 
Hili nalo watu wanasema boda wanaonewa? Ama kweli watanzania wapo wasiojua wanataka nini. Njia imetengenezwa maalum kwa ajili ya vyombo fulani halaf wenye vyombo tofauti na hivyo wanaingilia huku nyuma kuna watu wanawatetea!

Naikumbuka sana kauli ya Dr.Slaa, "Watanzania tuishi maisha halisi, tusipende kufuata mkumbo"
 
Back
Top Bottom