Bodaboda wangapi walilisikia tangazo la Rais?

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,233
12,507
Nijuavyo mimi bodaboda wengi hawana TV, ving'amuzi wala muda wa kuangalia TV au kusikiliza redio. Muda mwingi wanasikiliza muziki kwenye flash zao kwenye pikipiki ili kujaribu kuvutia wateja wapande bodaboda zao. Tangazo la rais kuhusu kung'oa matairi ya bodaboda zao huenda halikusikika kwao, hivyo sio vizuri watendaji kumchonganisha Rais na wananchi wake kwa kushindwa kutafsiri kauli zake.

Mimi nilidhani kuwa baada ya mh. Rais kutamka vile nyie watendaji mngejiongeza kwa kutoa elimu zaidi kwa waendesha bodaboda kuhusu utekelezaji wa kauli ya Rais na ubaya wa kupita kwenye barabara za UDART kabla ya kuanza kung'oa tairi za bodaboda fasta fasta huku mkipaza sauti kuwa mnatekeleza agizo la Rais.

Kusudio kuu la Rais pale halikuwa kung'oa tairi za bodaboda bali alitaka watendaji wakuu kuepusha ajali za barabarani kwa nguvu zote kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizoko kwenye makablasha yetu. Kung'oa tairi la mkosaji ni kanuni au sheria namba gani ya usalama barabarani?

Ningekuwa mimi ndio mh. Magufuli ningewatumbua waliong'oa tairi za bodaboda za wapiga kura wake, maana wameshindwa kazi kwa kushindwa kujiongeza, kutafsiri na kuzuia ajali za barabarani kwa kutumia sheria na kanuni zilizopo za kuzuia makosa ya barabarani. over!
 
Polisi wameongezewa kula ukiingia hata kwa kukatisha itabidi uchague ung'olewe tairi au utoe buku 10
 
Sheria biila shuruti inawezekana

hasa tukizingatia shuruti inamilikiwa na wenye sheria

Tujitafakari kama tunahitaji sheria

Maana kanuni ya sheria ni kukata pande zote
inapokata upande mmoja INAITWAJE?

boda boda ni mimi na wewe

na ule mradi NI WETU

tuwekeane sheria au tufundishane ni uamuzi wetu,

tuamue tu
Ikiwa sheria kazi yake ni kuvunjwa!
 
Uhakika ni kwamba bodaboda hatakiwi kupita njia ya mwendokasi.
Hakuwa na haja ya kumsikiliza Rais zaidi ya kufuata sheria.
Kazi za polisi wa barabarani ni pamoja ni kuzuia bodaboda wasipite njia ya mwendokasi hawakua na haja ya kumsubiri Rais aseme. Hakukuwa na upungufu wa sheria katika kuhakikisha kuwa bodaboda hawapi kwenye njia hizo.
 
Polisi wameongezewa kula ukiingia hata kwa kukatisha itabidi uchague ung'olewe tairi au utoe buku 10
Unaruhusiwa kukatisha upande wapili katika sehemu rasmi iliyowekwa kama vile kwenye zebra, ila unashuka na kukokota pikipikiyako ukisha vuka unapanda, safari inaendelea na hukamatwi.
 
Kazi za polisi wa barabarani ni pamoja ni kuzuia bodaboda wasipite njia ya mwendokasi hawakua na haja ya kumsubiri Rais aseme. Hakukuwa na upungufu wa sheria katika kuhakikisha kuwa bodaboda hawapi kwenye njia hizo.
Ili askari wa barabarani wazuie bodaboda wasiingie mwendokasi road inabidi wawe kama 10,000 kuanzia mbezi hadi kivukoni.
Yote nadhani yanafanyika kwa faida ya bodaboda wenyewe. Pale shekilango alikufa abilia wa bodaboda kwa kupasuka kichwa baada ya bodaboda kuforce kuvuka sehemu isiyo sahihi Bila kujua basi lipo karibu, dereva aliruka. Tusikubali kutetea uvunjwaji wa sheria maana sheria zipo kwa manufaa yetu sisi wenyewe.
 
Bodaboda wasumbufu sana na ukamataji wao ni mgumu sana maana huwa haogopi kumgonga hata askari nadhani hili ung'oaji matairi itasaidia kupunguza kidogo
 
Yani kuwatetea bodaboda unatakiwa labda ujitoe fahamu, maana siku zote hawa ni watu wa kuvunja sheria tu. Ni mara ngapi imetangazwa wasipite kwenye barabara ya mwendo kasi lakini wanapuuza tu! Hiyo kauli ya Mheshimiwa Rais alikuwa anatilia mkazo tu. Hao bodaboda hata wangewekewa matangazo kila kona bado hawawezi badilika. Hivyo inahitajika nguvu ya ziada kuwafanya wabadilike ili wafuate sheria.
 
Na kwa nini askari wakae kwa ajili ya kukamata bodaboda wakati wanajua sheria haiwaruhusu kupita mwendo kasi mkuu. Bodaboda waache ujinga wafuate sheria waone kama watakamatwa kwa kosa hilo.
 
boda boda na daladala hasa wa arusha ni tatizo nadhani kuna lugha wanaielewa ,kama hiyo ya kuwangolea tayari
 
Hata Kama wewe ni bodaboda huwezi kujiuliza tu kwanini Upo peke yako barabarani....!?
Au hadi usikie tangazo la Raisi
 
Uhakika ni kwamba bodaboda hatakiwi kupita njia ya mwendokasi.
Hakuwa na haja ya kumsikiliza Rais zaidi ya kufuata sheria.
isitoshe hili lilijulikana kabla hata njia zenyewe hazijazinduliwa. visingizio kwamba hawasikilizi au hawana redio/tv ni kiduchi sana. mbona mengine ya maandamano yanawafikia? wenzao waliogongwa kwa makosa ya kupitisha tukutuku zao hapo hawakupewa maonyo? yule abiria aliyeburutwa uvunguni mwa basi si aliponzwa na dereva asiyejua au aliyekaidi sheria? iweje leo tuendekeze na kulea makosa yatakayogharimu maisha ya wenzetu na vilema vya maisha ati ni kuogoapa sera ya 'wapiga kura' kwani wanaogongwa na kufa/kulemaa sio wapiga kura? tuweke itikadi kando tukemee na kupongeza inapobidi. mizaha na michezo michezo kwa uhai wa binadamu tuuepuke kabisa.
 
Yani kuwatetea bodaboda unatakiwa labda ujitoe fahamu, maana siku zote hawa ni watu wa kuvunja sheria tu. Ni mara ngapi imetangazwa wasipite kwenye barabara ya mwendo kasi lakini wanapuuza tu! Hiyo kauli ya Mheshimiwa Rais alikuwa anatilia mkazo tu. Hao bodaboda hata wangewekewa matangazo kila kona bado hawawezi badilika. Hivyo inahitajika nguvu ya ziada kuwafanya wabadilike ili wafuate sheria.
mwenye njaa tangu lini akatii sheria?, tuangalie na kulaumu kule tulipojikwaa sio tulikoangukia. Unapoongelea suala la bodaboda na machinga lazima uwe makini sana.
 
Kumfanya mtu asikilize redio hyo nayo ni kazi ya serikali? Hoja yako haina mashiko, kwani wewe umepataje taarifa?
 
Nijuavyo mimi bodaboda wengi hawana TV, ving'amuzi wala muda wa kuangalia TV au kusikiliza redio. Muda mwingi wanasikiliza muziki kwenye flash zao kwenye pikipiki ili kujaribu kuvutia wateja wapande bodaboda zao. Tangazo la rais kuhusu kung'oa matairi ya bodaboda zao huenda halikusikika kwao, hivyo sio vizuri watendaji kumchonganisha Rais na wananchi wake kwa kushindwa kutafsiri kauli zake.

Mimi nilidhani kuwa baada ya mh. Rais kutamka vile nyie watendaji mngejiongeza kwa kutoa elimu zaidi kwa waendesha bodaboda kuhusu utekelezaji wa kauli ya Rais na ubaya wa kupita kwenye barabara za UDART kabla ya kuanza kung'oa tairi za bodaboda fasta fasta huku mkipaza sauti kuwa mnatekeleza agizo la Rais.

Kusudio kuu la Rais pale halikuwa kung'oa tairi za bodaboda bali alitaka watendaji wakuu kuepusha ajali za barabarani kwa nguvu zote kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizoko kwenye makablasha yetu. Kung'oa tairi la mkosaji ni kanuni au sheria namba gani ya usalama barabarani?

Ningekuwa mimi ndio mh. Magufuli ningewatumbua waliong'oa tairi za bodaboda za wapiga kura wake, maana wameshindwa kazi kwa kushindwa kujiongeza, kutafsiri na kuzuia ajali za barabarani kwa kutumia sheria na kanuni zilizopo za kuzuia makosa ya barabarani. over!
We bwana sijui wataka nn.. Karne hii ya 21 mwaka wa 2017.. Kweli utasingizia hujapata taarifa.??
Okay.. Zike ni njia maalum za magari special.. Kwanini akapite pale..
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom