Juzi nilikua nawahisha mzigo flani uende mkoani, kutokoea k.koo,
Kuulizia Konda akaniambia ndio tunatoka ubungo, ikabidi nichukue boda niiwahi Basi mwenge,
Sipendagi kuharakisha hawa watu ila sikua na jinsi wakati anaufunga ule mzigo nikamwambi Uharakishe tuna mda mfupi sanaa gari inapita,
Sijapata ona aisee, Ile boda ilipigwa mguu, Tunafika Junction pale mwenge hata hakuangalia, ye kaona Gap pale kati kavuka,
Tulipishana na Semi Ubavu kwa ubavu,
Ninaposema hivi namaanisha Shati langu lilichafuliwa kabisa na bodi ya ile semi, na mzigo ukapigwa push kdg.
Mimi niliamini tayari, maana yenyewe ilikua inakata kona na sisi tunanyooka, kufuata zile tairi 6 za nyuma, kushtuka tushavuka, Na basi hio hapo, konda ndio akafungua mzigo kwenye boda mana jamaa naye kapata wenge kakaa kwenye kadaraja ka mbao Kwenye mtaro kainama kashika kichwa,
Ana zinduka tuu ananiuliza
"Tunarudi k.koo"?
Nikamwambia Baba rudi tu mwenyewe.