Boda boda wa KIVUKONI ni kero kubwa kwa watembea kwa miguu

Boda boda wa KIVUKONI ni kero kubwa kwa watembea kwa miguu

waba

New Member
Joined
Apr 30, 2025
Posts
2
Reaction score
0
Boda boda wa KIVUKONI ni kero kubwa abiria watembea kwa miguu wanapata shida kutembea kwa uhuru hadi kuna Wakati mwingine wanaleta msongamano kwa kupaki bodaboda zao kati Kati ya barabara za watembea kwa miguu .Naomba Mamlaka husika iwataftie eneo maalumu kwa ajiri ya kusafirisha Abiria.
 
Tatizo lipo pia gongo la mboto, sehemu za watembea kwa miguu wapika chips wameweka majiko watembea kwa miguu wanatembea kwenye njia za magari, hii inaleta msongamano kuanzia gongo la mboto hadi tazara, hivi kweli tunajenga barabara za lami kwa ajili wa kuweka majiko ya mishikaki na chips? kweli watu wachelewe kwenda majumbani kazini kisa magari yameshindwa kupishana na majiko ya nyamachoma? mbaya hizo nyama wanatia pilipili na sijawahi ona mtu akinunua na hawafilisiki nadhani kuna mtu anafadhili hizi kero
 
Ninashauri waondolewe pale,, kwanza bodaboda mjini hawatakiwi,, tujifunze majiji ya wenzetu
 
Tatizo lipo pia gongo la mboto, sehemu za watembea kwa miguu wapika chips wameweka majiko watembea kwa miguu wanatembea kwenye njia za magari, hii inaleta msongamano kuanzia gongo la mboto hadi tazara, hivi kweli tunajenga barabara za lami kwa ajili wa kuweka majiko ya mishikaki na chips? kweli watu wachelewe kwenda majumbani kazini kisa magari yameshindwa kupishana na majiko ya nyamachoma? mbaya hizo nyama wanatia pilipili na sijawahi ona mtu akinunua na hawafilisiki nadhani kuna mtu anafadhili hizi kero
hili nakazia, imagine mpaka sehemu kubwa kama k/koo
 
Bodaboda na bajaji ziondolewe katikati ya mji.
Sio hapo tu. Tazama pale mbele ya ferry za Zanzibar, sehemu mpya za watembea kwa miguu Azikiwe avenue. Nk. Kwa nini wanaruhusiwa kupark kwenye sidewalks?
Kama hawajawatengenezea sehemu za kupark ina maana hawapaswi kuwepo.
 
Ninashauri waondolewe pale,, kwanza bodaboda mjini hawatakiwi,, tujifunze majiji ya wenzetu
Naunga mkono hoja, wamejaa mijini huko sio kawaida. Hawa waishie nje ya miji, ni aheri hata bajaji.
 
Boda boda wa KIVUKONI ni kero kubwa abiria watembea kwa miguu wanapata shida kutembea kwa uhuru hadi kuna Wakati mwingine wanaleta msongamano kwa kupaki bodaboda zao kati Kati ya barabara za watembea kwa miguu .Naomba Mamlaka husika iwataftie eneo maalumu kwa ajiri ya kusafirisha Abiria.
na ukikaa vibaya wanakugonga wale jamaa
 
Hii Mikandio iliyopigwa humu siyo ya kawaida,vijicho,husda na vijino pembe ni kila mahali kuwahusu Bodaboda na Bajaji!

Aisee ndugu zangu Bodaboda na Bajaji tukae mkao wa kuliwa,siyo Kwa Nongwa hizi!
 
Hii Mikandio iliyopigwa humu siyo ya kawaida,vijicho,husda na vijino pembe ni kila mahali kuwahusu Bodaboda na Bajaji!

Aisee ndugu zangu Bodaboda na Bajaji tukae mkao wa kuliwa,siyo Kwa Nongwa hizi!
kweli hawana maana, na hata ukiuza huduma wanaanza kutizamana they are not there for business wako ku create kero tu
 
na ikiwezekana tupige marufuku bajaj za petrol zinapiga makelele zinachafua hewa, turuhusu bajaj za umeme tu
 
Boda boda wa KIVUKONI ni kero kubwa abiria watembea kwa miguu wanapata shida kutembea kwa uhuru hadi kuna Wakati mwingine wanaleta msongamano kwa kupaki bodaboda zao kati Kati ya barabara za watembea kwa miguu .Naomba Mamlaka husika iwataftie eneo maalumu kwa ajiri ya kusafirisha Abiria.
Mamlaka zipi ?
Hizi za wala RUSHWA traffic?
Sahau hilo
 
Back
Top Bottom