Nicodemas Tambo Mwikozi
JF-Expert Member
- Aug 13, 2016
- 663
- 1,047
- Thread starter
- #21
Based on truel story na kesi ipo polisi.....Jifunze kufupisha.. Kuna chumvi nyingi hapo ambazo hazikutakiwa kuwepo.. Na bado hadith yako ingeeleweka.
Based on truel story na kesi ipo polisi.....Jifunze kufupisha.. Kuna chumvi nyingi hapo ambazo hazikutakiwa kuwepo.. Na bado hadith yako ingeeleweka.
Truth 100%Ila sio stori ya kweli ni hadithi tuu ilio changanyika na ukweli hapo kwa mkuu wa mkoa Tumainiel kiwelu. Hongera lakini.
Twataizya mkwai mzee mwezangu wa kuvumbushaHahahahaah mkuu umenikumbusha mikokoli enzi hizo, unatoka hapo mdomo mweusiiii kwa jivu la moto wa pumba za mpunga.
Huyo jamaa black jesus namkumbuka sana.!
fala weDaah safi sana inasisimua sana..!! Hizi.ndio fani za kujivunia.
NiceSEHEMU YA II
BLACK JESUS
Baada ya kunipitisha dirishani, yeye pia alijipenyeza na kurukia nje kabla hata sijainuka pale chini nilipoangukia.
Akanishika mkono wangu kwa nguvu kisha akanisukuma kwa nguvu kiasi cha kupepesuka, japo sikuanguka. Alichonifanya hakikutofautiana na mfugaji anavyoswaga mfugo wake!
Ulikuwa ni msafara kuelekea nyumbani kwa kina John. Alinitanguliza kama msukule, na kwa namna ya ajabu sikuwa na nguvu japo ya kupiga kelele za kuomba msaada achilia mbali kukimbia. Black Jesus alikuwa amenishika pabaya.
Kiguu na njia mpaka mbele ya mlango wa nyumba ya kina John. Nikamuelekeza kwa kidole kuwa humo ndimo alimo mwenye chupa yake.
Akanikazia macho kisha akaniuliza kwa sauti ya kunong'onona.
"Una hakika huyo mwenzako aliyechukua chupa yangu anakaa humu?"
Nilimwitikia kwa kichwa huku nikimtazama kwa macho yaliyojaa hofu. Bado nilikuwa siamini kama huyu ndiye yule Black Jesus, mwendawazimu aliyeshinda kutwa akizunguka huku na kule akiwa na mazagazaga yake ya kiendawazimu!
Nilitamani Mungu afanye muujiza jua liwake ghafla, kisha watu wote watoke majumbani mwao na kuja hapa nilipo ili tushirikiane kumshangaa kiumbe huyu ambaye kwa sasa sikumtofautishi na zimwi au jini. Kichaa mchana kumbe usiku ni mzima kama jiwe?
Wakati nafikiria hayo ambayo kimsingi hayawezekani kutokea, alitoa kitu kama gundi ya karatasi(soltape) kisha akaifungua na kunibandika nayo mdomoni ili nisiweze kupiga kelele. Baada ya hapo akanifunga kamba miguuni na mikononi, ndipo akanisomba kimzobemzobe na kwenda kunificha kwenye moja ya vichaka vya maua yaliyozunguka nyumba yetu.
Yote haya niliyaona kama mwendelezo wa ndoto iliyoanzia chumbani kwangu wakati mvua ya ajabu ikiwa inapita dirishani na kunifuata kitandani. Sikuwa na nguvu ya kubisha wala kujitetea.
Kulikuwa na harufu fulani kwenye ile soltape iliyofungwa mdomoni iliyonifanya nipige chafya kama mbili au tatu. Tena nilipiga kwa tabu sana. Hebu fikiria mtu upige chafya huku mdomo ukiwa umefungwa, hiyo chafya inatofautiana vipi na chafya ya mbuzi?
Akiwa ameridhishwa na hizo chafya, nilimuona akigeuka taratibu na kuelekea kwenye moja ya madirisha ya nyumba ya kina John. Sikufanikiwa kuona alichokifanya kabla fahamu hazijanitoka!
*****
Raia wema walikuwa wameniokota asubuhi kwenye yale maua na kunipeleka nyumbani.
Inavyoonesha bibi hakuwa na habari kama mjukuu wake sikuwa nimelala ndani. Lakini alivyokwenda chumbani na kwenda kukuta kitanda kitupu huku dirisha likiwa wazi, akaamini alichoambiwa na wale wasamaria.
Nilikuwa natetemeka kwa baridi iliyonipiga usiku kucha mfano wa kifaranga cha kuku. Baridi ilikuwa imepenya hadi kwenye mifupa.
Walijaribu kuniuliza hili na lile lakini sikuweza kuwajibu lolote zaidi ya kutoa machozi kimya kimya. Sikuwa sawa kisaikolojia.
Ndiyo maana ikashauriwa nipewe chai ya moto au uji. Bibi akaniandalia chai nzito na mayai mawili ya bata ambao tulikuwa tukiwafuga. Kidogo siha yangu ikarejea kwenye unafuu.
Hata hivyo ilishauriwa nipumzishwe chumbani kwa muda ili kuruhusu akili yangu ikae sawa kabla ya kuwasimulia kilichonikuta. Lakini mpaka muda huo kila mtu alikuwa anasema lake. Wengine waliamini tukio hilo lilikuwa la kishirikina, lakini kuna wengine walidhani pengine nilikuwa nimepatwa na zile ndoto ambazo huwafanya watu wainuke na kufanya vitendo vingi ilhali wakiwa bado usingizini.
Ni muda huo huo ndipo mama yake rafiki yangu John alipoingia pale ndani na kutoa taarifa iliyozua taharuki mpya. John alikuwa haonekani, na dirisha la chumba chake lilikutwa likiwa wazi huku milango yote ya nyumba yao ikiwa imefungwa.
Hapo ikabidi wazee wote wakiongozwa na bibi aliyekwishawadodosa kuhusiana na ule ugeni wa mtu asiyefahamika aliyekuja kuniulizia jana usiku, wanizingire upya na kunihoji kwa msisitizo wa kipekee.
Kugundua kwamba John pia alikuwa ametekwa na Black Jesus, sikuona haja ya kuendelea kuficha. Nikaamua kuanika ukweli wote hadharani, kuanzia ule muda tumekutana naye akitokea makaburini mpaka tulivyoenda kuchukua chupa yake iliyosindikwa kwa gunzi lililotushinda kufungua kwenye chumba chake pale uwanjani.
Nilishuhudia jinsi walivyopigwa butwaa kwa maelezo niliyowapa. Ni dhahiri, sehemu ya mshangao wao ilikuwa ikinihoji ni kwa vipi tulipata ujasiri wa kwenda kufukunyua siri za mwendawazimu yule asiye na ugomvi na mtu?
Sikuwaficha pia kuhusu mtu aliyeniingilia usiku kwa mbinu za mizimu kama sio kijasusi. Na nilipotanabahisha kwamba mtu huyo ambaye sikuwa na shaka ndiye aliyemteka John alikuwa ni yule kichaa maarufu Black Jesus, miguno iliwatoka wazee wa watu kwa mshangao!
Ikashauriwa kuwa ile chupa ijaribu kutafutwa kwenye maua ambayo John alikusudia kuificha. Hisia zilinijia kuwa usiku ule John hakuweza kukumbuka sehemu hasa alipoificha ile chupa, hivyo ikamchukiza na kumlazimu Black Jesus kuondoka naye baada ya kuikosa.
Wazee walianza zoezi la kufukunyua hapa na pale kuzunguka nyumba yetu. Baada ya dakika kumi na tano mtu mmoja alikuwa amekutana chupa nyeusi ilikuwa imeshindiliwa kwa gunzi. Na walipoileta mbele yangu kwa utambuzi, niliitikia kwa kichwa huku nikitetemeka kwa hofu. Mambo yalikuwa yamebadilika kwa kasi sana. Kutoka kwenye 'kuvumbosha mahindi' na kufikia hatua ya kutekana?! Halikuwa jambo dogo. Tena nilijuta kuliko unavyoweza kufikiria.
Swala likaja, ile chupa ifunguliwe au ipelekwe kituo cha polisi kwa uchunguzi zaidi?
Yakaibuka malumbano na mvutano wa hapa na pale, lakini kundi liliongozwa na mjumbe wa nyumba kumi ambaye tayari tulishakuwa naye hapa, lilishinda na kuafikiana kuifungua chupa.
Akachaguliwa kijana mmoja mwenye nguvu achomoe gunzi ili waone kilichokuwemo ndani ya chupa.
Aliibana ile chupa katikati ya miguu yake na kuvuta lile gunzi kwa nguvu mpaka akafanikiwa kulichomoa. Watu wote walikuwa wamemtumbulia macho kijana huyo kusubiri kuona kilichokuwemo ndani ya chupa.
" Kuna nini humo?" Mtu mmoja aliropoka baada ya kukosa simile. Waoga wachache walianza kurudi nyuma taratibu katika mkao ambao ungewawezesha kutimua mbio, endapo chochote cha kuhatarisha usalama wao kingetokea.
Huyu kijana baada ya kutikisa, kuchungulia na kuigeuza ile chupa huku na kule, aliwaomba watu wampatie kitu kama sahani au sinia. Kabla mshangao hawaujawamaliza, mtu mmoja alileta sahani.
Huyo kijana akaanza kumimina kitu kisichoeleweka kutoka ndani ya ile chupa kuelekea kwenye sahani aliyopewa. Ilichukua sekunde kadhaa kabla ya uji mzito uliometameta mfano wa madini ya fedha uliopoanza kububujikia taratibu kwenye ile sahani.
Ukimya uliokuwepo pale uwani ulidhihirisha hofu waliyokuwa nayo watu wote. Ile sahani ikaanza kuzungushwa ili kila mwenye ufahamu aweze kusema chochote kuhusiana na uji huo ambao ni dhahiri ulikuwa ni aina fulani ya madini adimu.
"Zebaki!" Mtu mmoja aliropoka.
"Ndiyo nini?" Mwingine akahoji.
"Ni aina ya madini...!"
Mvurugano ulioibuka ulipelekea taarifa zipelekwe kituo cha polisi.
Polisi walikuja na kuchukua ile chupa. Mimi pia nilichukuliwa, pamoja na bibi na mjumbe wa nyumba kumi kwa ajili ya kwenda kutoa maelezo ya kuwasaidia polisi.
Mpaka saa sita mchana tulikuwa tumerudi nyumbani baada ya kutoa ushirikiano uliowatosheleza polisi. Nilikuwa hoi kwa uchovu.
Ile chupa yenye madini ya zebaki ilibaki polisi.
Msako wa kumsaka Black Jesus na mtoto John ulianza. Cha ajabu siku hiyo Black Jesus hakuonekana kabisa sehemu zote alizozoeleka. Na hata kwenye chumba chake alichokitumia kulala kule Nelson Mandela, hakuwepo wala mizigo yake haikuonekana. Ni wazi Black Jesus alidhihirika kuwa mtu hatari ambaye hakuwa kichaa kama tulivyodhani.
Taarifa ziligaa mjini kwa kasi ya ajabu. Mji mzima ukawa na habari za matukio ya Black Jesus na jinsi alivyosakwa na polisi.
Mtaa wetu ulikuwa umezizima kwa simanzi na hofu ya majanga mazito ya kupotelewa na mtoto John. Hali yangu ndiyo ilikuwa mbaya zaidi. Kila nilipomfikiria John na jinsi jana jioni tulivyokuwa tukifurahia pamoja 'mikokoli' nilikosa raha. Machozi yakawa yananitoka muda wote.
Usiku ukaingia. Si John wala black Jesus aliyekuwa amepatikana.
Wazee wa mtaa wakiongozwa na mjumbe wa nyumba kumi, walikuwa wamekusanyika nyumbani kwa kina John huku vikao vya namna ya kuendesha uchunguzi na ukombozi wa mtoto John vikiwa vimepamba moto.
Kwenye saa mbili askari polisi wawili walikuja kwa lengo la kuwafariji wazazi wa John na kuwatia moyo kuhusiana na walipofikia juu ya harakati za kumpata John. Lakini wazee wenye hekima waligundua kuwa kazi ilishakuwa ngumu na askari hao walitumwa tu kuja kuangalia kama kuna lolote jipya kuhusiana utekwaji wa John.
Polisi waliondoka, wazee wakaendelea kuwepo. Kwa namna fulani ni kama walikuwa wameanza maombolezo ya kuondokewa na mtoto John. Mara kadhaa kilio cha uchungu cha mama John kilisikika, kisha akatulizwa na wanawake wenzake. Hali ilitia simanzi mno.
Watu wakiwa wanaendelea kuota moto, kwenye majira ya saa nne na nusu usiku walishangaa kumuona mtoto John akiingia pale nyumbani huku akiwa anakimbia kwa hofu na mashaka. Ilikuwa kama ndoto.
Alikuwa amechafuka hafai! Yowe kubwa lilisikika na haikujulikana mara moja kama ilikuwa shangwe au mshangao. Watu waliokuwa wamerejea majumbani mwao walifurika upya nyumbani kwa kina John.
John mwenyewe akapotelewa na fahamu mara tu baada ya kufika kwenye mlango wa nyumba yao. Hakika ulikuwa usiku wa hekaheka!
Baada ya kumpatia huduma ya kwanza John alizinduka. Alikuwa amechakaa kwa kiasi cha kufadhaisha. Mwili wake ulijaa vidonda na damu zilizogandiana kila sehemu. Miguuni alikuwa amechanjwachanjwa kwa vitu mithili ya wembe mkali.
Baada ya kuogeshwa kwa maji moto na kupewa chakula, John akasimulia kilichomkuta.
Kumbe ule usiku baada ya kuchomolewa chumbani kwa staili ya kushangazwa kama ilivyotokea kwangu, aliamriwa aelekeze chupa ilipo. Naye kwa hofu ya kitoto hakumficha jinsi alivyoificha chupa ile kwenye maua. Walijaribu kuisaka bila mafanikio, na ndipo kwa hasira Black Jesus akaamua kumchukua kwa kuamini kuwa alikuwa akisema uongo.
Nyuma ya bohari kuu la serikali kulikuwa na vyumba vilivyowahi kuezuliwa na mvua kubwa iliyowahi kunyesha siku za nyuma. Eneo hili lilikuwa linatazama kabisa na makaburi. Na hakukuwa na makazi ya watu. Huko ndiko John alikoenda kufichwa na kufungwa kwa kamba.
Kama isingekuwa utundu na ujasiri alipkuwa nao, leo hii tungekuwa tunaongelea mengine.
Mtoto John alifungua zile kamba kwa meno yake na kufanikiwa kutoka nje ya jengo alokuwa kafichwa. Wakati anatoka ndipo akamuona Black Jesus kwa mbali akirudi na kuanza kumkimbiza kwa hasira.
John alijikuta amekimbilia kwenye mkondo wa maji ya mto Lwiche ambao umezingirwa na majani, matete na vichaka vikubwa. Ni huko ndiko alikojificha kutwa nzima akihofia kujitokeza na kudakwa na Black Jesus ambaye alionekana akimsaka huku na kule kando ya mto ule.
Ni usiku huu ndipo alipojipa ujasiri wa kutoka vichakani, akiwa ameshajeruhiwa kwa majani na miiba yenye ncha kali mpaka alipofanikiwa kutoka nje ya mto na kukimbilia nyumbani kwa staili ya kujifichaficha.
Watu walisikitika sana.
Taarifa hizi zilipowafikia polisi walikuja kumchukua kwa uchunguzi zaidi na kumrudisha nyumbani baadae sana.
Lakini walau watu walienda kulala wakiwa na amani mtoto John alikuwa hai. Japo dukuduku liliendelea kuwatafuna wote, Black Jesus alikuwa ni nani hasa? Alikuwa kajificha wapi? Alikuwa na malengo gani?
Na vipi kuhusu madini ya zebaki, alikusudia kufanyia nini?
Siku, wiki, mwezi na hatimaye miezi ilikatika bila Black Jesus kuonekana wala kusikika! Likabaki kuwa fumbo la imani.....
Siku Jenerali Tumaniel Kiwelu alipopata habari zake alituita kwenye ofisi yake, ili aweze kutufahamu na kutupongeza pia kwa ujasiri. Na picha hii hapa chini nilipiga na bibi baada ya kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Rukwa siku hiyo.
Lakini Black Jesus ni nani?
Alikuwa na lengo gani?
Na vipi kuhusu madini ya zebaki aliyokuwa akitembea nayo, alikusudia kuyafanyia nini?
Itaendelea...
SEHEMU YA II
BLACK JESUS
Baada ya kunipitisha dirishani, yeye pia alijipenyeza na kurukia nje kabla hata sijainuka pale chini nilipoangukia.
Akanishika mkono wangu kwa nguvu kisha akanisukuma kwa nguvu kiasi cha kupepesuka, japo sikuanguka. Alichonifanya hakikutofautiana na mfugaji anavyoswaga mfugo wake!
Ulikuwa ni msafara kuelekea nyumbani kwa kina John. Alinitanguliza kama msukule, na kwa namna ya ajabu sikuwa na nguvu japo ya kupiga kelele za kuomba msaada achilia mbali kukimbia. Black Jesus alikuwa amenishika pabaya.
Kiguu na njia mpaka mbele ya mlango wa nyumba ya kina John. Nikamuelekeza kwa kidole kuwa humo ndimo alimo mwenye chupa yake.
Akanikazia macho kisha akaniuliza kwa sauti ya kunong'onona.
"Una hakika huyo mwenzako aliyechukua chupa yangu anakaa humu?"
Nilimwitikia kwa kichwa huku nikimtazama kwa macho yaliyojaa hofu. Bado nilikuwa siamini kama huyu ndiye yule Black Jesus, mwendawazimu aliyeshinda kutwa akizunguka huku na kule akiwa na mazagazaga yake ya kiendawazimu!
Nilitamani Mungu afanye muujiza jua liwake ghafla, kisha watu wote watoke majumbani mwao na kuja hapa nilipo ili tushirikiane kumshangaa kiumbe huyu ambaye kwa sasa sikumtofautishi na zimwi au jini. Kichaa mchana kumbe usiku ni mzima kama jiwe?
Wakati nafikiria hayo ambayo kimsingi hayawezekani kutokea, alitoa kitu kama gundi ya karatasi(soltape) kisha akaifungua na kunibandika nayo mdomoni ili nisiweze kupiga kelele. Baada ya hapo akanifunga kamba miguuni na mikononi, ndipo akanisomba kimzobemzobe na kwenda kunificha kwenye moja ya vichaka vya maua yaliyozunguka nyumba yetu.
Yote haya niliyaona kama mwendelezo wa ndoto iliyoanzia chumbani kwangu wakati mvua ya ajabu ikiwa inapita dirishani na kunifuata kitandani. Sikuwa na nguvu ya kubisha wala kujitetea.
Kulikuwa na harufu fulani kwenye ile soltape iliyofungwa mdomoni iliyonifanya nipige chafya kama mbili au tatu. Tena nilipiga kwa tabu sana. Hebu fikiria mtu upige chafya huku mdomo ukiwa umefungwa, hiyo chafya inatofautiana vipi na chafya ya mbuzi?
Akiwa ameridhishwa na hizo chafya, nilimuona akigeuka taratibu na kuelekea kwenye moja ya madirisha ya nyumba ya kina John. Sikufanikiwa kuona alichokifanya kabla fahamu hazijanitoka!
*****
Raia wema walikuwa wameniokota asubuhi kwenye yale maua na kunipeleka nyumbani.
Inavyoonesha bibi hakuwa na habari kama mjukuu wake sikuwa nimelala ndani. Lakini alivyokwenda chumbani na kwenda kukuta kitanda kitupu huku dirisha likiwa wazi, akaamini alichoambiwa na wale wasamaria.
Nilikuwa natetemeka kwa baridi iliyonipiga usiku kucha mfano wa kifaranga cha kuku. Baridi ilikuwa imepenya hadi kwenye mifupa.
Walijaribu kuniuliza hili na lile lakini sikuweza kuwajibu lolote zaidi ya kutoa machozi kimya kimya. Sikuwa sawa kisaikolojia.
Ndiyo maana ikashauriwa nipewe chai ya moto au uji. Bibi akaniandalia chai nzito na mayai mawili ya bata ambao tulikuwa tukiwafuga. Kidogo siha yangu ikarejea kwenye unafuu.
Hata hivyo ilishauriwa nipumzishwe chumbani kwa muda ili kuruhusu akili yangu ikae sawa kabla ya kuwasimulia kilichonikuta. Lakini mpaka muda huo kila mtu alikuwa anasema lake. Wengine waliamini tukio hilo lilikuwa la kishirikina, lakini kuna wengine walidhani pengine nilikuwa nimepatwa na zile ndoto ambazo huwafanya watu wainuke na kufanya vitendo vingi ilhali wakiwa bado usingizini.
Ni muda huo huo ndipo mama yake rafiki yangu John alipoingia pale ndani na kutoa taarifa iliyozua taharuki mpya. John alikuwa haonekani, na dirisha la chumba chake lilikutwa likiwa wazi huku milango yote ya nyumba yao ikiwa imefungwa.
Hapo ikabidi wazee wote wakiongozwa na bibi aliyekwishawadodosa kuhusiana na ule ugeni wa mtu asiyefahamika aliyekuja kuniulizia jana usiku, wanizingire upya na kunihoji kwa msisitizo wa kipekee.
Kugundua kwamba John pia alikuwa ametekwa na Black Jesus, sikuona haja ya kuendelea kuficha. Nikaamua kuanika ukweli wote hadharani, kuanzia ule muda tumekutana naye akitokea makaburini mpaka tulivyoenda kuchukua chupa yake iliyosindikwa kwa gunzi lililotushinda kufungua kwenye chumba chake pale uwanjani.
Nilishuhudia jinsi walivyopigwa butwaa kwa maelezo niliyowapa. Ni dhahiri, sehemu ya mshangao wao ilikuwa ikinihoji ni kwa vipi tulipata ujasiri wa kwenda kufukunyua siri za mwendawazimu yule asiye na ugomvi na mtu?
Sikuwaficha pia kuhusu mtu aliyeniingilia usiku kwa mbinu za mizimu kama sio kijasusi. Na nilipotanabahisha kwamba mtu huyo ambaye sikuwa na shaka ndiye aliyemteka John alikuwa ni yule kichaa maarufu Black Jesus, miguno iliwatoka wazee wa watu kwa mshangao!
Ikashauriwa kuwa ile chupa ijaribu kutafutwa kwenye maua ambayo John alikusudia kuificha. Hisia zilinijia kuwa usiku ule John hakuweza kukumbuka sehemu hasa alipoificha ile chupa, hivyo ikamchukiza na kumlazimu Black Jesus kuondoka naye baada ya kuikosa.
Wazee walianza zoezi la kufukunyua hapa na pale kuzunguka nyumba yetu. Baada ya dakika kumi na tano mtu mmoja alikuwa amekutana chupa nyeusi ilikuwa imeshindiliwa kwa gunzi. Na walipoileta mbele yangu kwa utambuzi, niliitikia kwa kichwa huku nikitetemeka kwa hofu. Mambo yalikuwa yamebadilika kwa kasi sana. Kutoka kwenye 'kuvumbosha mahindi' na kufikia hatua ya kutekana?! Halikuwa jambo dogo. Tena nilijuta kuliko unavyoweza kufikiria.
Swala likaja, ile chupa ifunguliwe au ipelekwe kituo cha polisi kwa uchunguzi zaidi?
Yakaibuka malumbano na mvutano wa hapa na pale, lakini kundi liliongozwa na mjumbe wa nyumba kumi ambaye tayari tulishakuwa naye hapa, lilishinda na kuafikiana kuifungua chupa.
Akachaguliwa kijana mmoja mwenye nguvu achomoe gunzi ili waone kilichokuwemo ndani ya chupa.
Aliibana ile chupa katikati ya miguu yake na kuvuta lile gunzi kwa nguvu mpaka akafanikiwa kulichomoa. Watu wote walikuwa wamemtumbulia macho kijana huyo kusubiri kuona kilichokuwemo ndani ya chupa.
" Kuna nini humo?" Mtu mmoja aliropoka baada ya kukosa simile. Waoga wachache walianza kurudi nyuma taratibu katika mkao ambao ungewawezesha kutimua mbio, endapo chochote cha kuhatarisha usalama wao kingetokea.
Huyu kijana baada ya kutikisa, kuchungulia na kuigeuza ile chupa huku na kule, aliwaomba watu wampatie kitu kama sahani au sinia. Kabla mshangao hawaujawamaliza, mtu mmoja alileta sahani.
Huyo kijana akaanza kumimina kitu kisichoeleweka kutoka ndani ya ile chupa kuelekea kwenye sahani aliyopewa. Ilichukua sekunde kadhaa kabla ya uji mzito uliometameta mfano wa madini ya fedha uliopoanza kububujikia taratibu kwenye ile sahani.
Ukimya uliokuwepo pale uwani ulidhihirisha hofu waliyokuwa nayo watu wote. Ile sahani ikaanza kuzungushwa ili kila mwenye ufahamu aweze kusema chochote kuhusiana na uji huo ambao ni dhahiri ulikuwa ni aina fulani ya madini adimu.
"Zebaki!" Mtu mmoja aliropoka.
"Ndiyo nini?" Mwingine akahoji.
"Ni aina ya madini...!"
Mvurugano ulioibuka ulipelekea taarifa zipelekwe kituo cha polisi.
Polisi walikuja na kuchukua ile chupa. Mimi pia nilichukuliwa, pamoja na bibi na mjumbe wa nyumba kumi kwa ajili ya kwenda kutoa maelezo ya kuwasaidia polisi.
Mpaka saa sita mchana tulikuwa tumerudi nyumbani baada ya kutoa ushirikiano uliowatosheleza polisi. Nilikuwa hoi kwa uchovu.
Ile chupa yenye madini ya zebaki ilibaki polisi.
Msako wa kumsaka Black Jesus na mtoto John ulianza. Cha ajabu siku hiyo Black Jesus hakuonekana kabisa sehemu zote alizozoeleka. Na hata kwenye chumba chake alichokitumia kulala kule Nelson Mandela, hakuwepo wala mizigo yake haikuonekana. Ni wazi Black Jesus alidhihirika kuwa mtu hatari ambaye hakuwa kichaa kama tulivyodhani.
Taarifa ziligaa mjini kwa kasi ya ajabu. Mji mzima ukawa na habari za matukio ya Black Jesus na jinsi alivyosakwa na polisi.
Mtaa wetu ulikuwa umezizima kwa simanzi na hofu ya majanga mazito ya kupotelewa na mtoto John. Hali yangu ndiyo ilikuwa mbaya zaidi. Kila nilipomfikiria John na jinsi jana jioni tulivyokuwa tukifurahia pamoja 'mikokoli' nilikosa raha. Machozi yakawa yananitoka muda wote.
Usiku ukaingia. Si John wala black Jesus aliyekuwa amepatikana.
Wazee wa mtaa wakiongozwa na mjumbe wa nyumba kumi, walikuwa wamekusanyika nyumbani kwa kina John huku vikao vya namna ya kuendesha uchunguzi na ukombozi wa mtoto John vikiwa vimepamba moto.
Kwenye saa mbili askari polisi wawili walikuja kwa lengo la kuwafariji wazazi wa John na kuwatia moyo kuhusiana na walipofikia juu ya harakati za kumpata John. Lakini wazee wenye hekima waligundua kuwa kazi ilishakuwa ngumu na askari hao walitumwa tu kuja kuangalia kama kuna lolote jipya kuhusiana utekwaji wa John.
Polisi waliondoka, wazee wakaendelea kuwepo. Kwa namna fulani ni kama walikuwa wameanza maombolezo ya kuondokewa na mtoto John. Mara kadhaa kilio cha uchungu cha mama John kilisikika, kisha akatulizwa na wanawake wenzake. Hali ilitia simanzi mno.
Watu wakiwa wanaendelea kuota moto, kwenye majira ya saa nne na nusu usiku walishangaa kumuona mtoto John akiingia pale nyumbani huku akiwa anakimbia kwa hofu na mashaka. Ilikuwa kama ndoto.
Alikuwa amechafuka hafai! Yowe kubwa lilisikika na haikujulikana mara moja kama ilikuwa shangwe au mshangao. Watu waliokuwa wamerejea majumbani mwao walifurika upya nyumbani kwa kina John.
John mwenyewe akapotelewa na fahamu mara tu baada ya kufika kwenye mlango wa nyumba yao. Hakika ulikuwa usiku wa hekaheka!
Baada ya kumpatia huduma ya kwanza John alizinduka. Alikuwa amechakaa kwa kiasi cha kufadhaisha. Mwili wake ulijaa vidonda na damu zilizogandiana kila sehemu. Miguuni alikuwa amechanjwachanjwa kwa vitu mithili ya wembe mkali.
Baada ya kuogeshwa kwa maji moto na kupewa chakula, John akasimulia kilichomkuta.
Kumbe ule usiku baada ya kuchomolewa chumbani kwa staili ya kushangazwa kama ilivyotokea kwangu, aliamriwa aelekeze chupa ilipo. Naye kwa hofu ya kitoto hakumficha jinsi alivyoificha chupa ile kwenye maua. Walijaribu kuisaka bila mafanikio, na ndipo kwa hasira Black Jesus akaamua kumchukua kwa kuamini kuwa alikuwa akisema uongo.
Nyuma ya bohari kuu la serikali kulikuwa na vyumba vilivyowahi kuezuliwa na mvua kubwa iliyowahi kunyesha siku za nyuma. Eneo hili lilikuwa linatazama kabisa na makaburi. Na hakukuwa na makazi ya watu. Huko ndiko John alikoenda kufichwa na kufungwa kwa kamba.
Kama isingekuwa utundu na ujasiri alipkuwa nao, leo hii tungekuwa tunaongelea mengine.
Mtoto John alifungua zile kamba kwa meno yake na kufanikiwa kutoka nje ya jengo alokuwa kafichwa. Wakati anatoka ndipo akamuona Black Jesus kwa mbali akirudi na kuanza kumkimbiza kwa hasira.
John alijikuta amekimbilia kwenye mkondo wa maji ya mto Lwiche ambao umezingirwa na majani, matete na vichaka vikubwa. Ni huko ndiko alikojificha kutwa nzima akihofia kujitokeza na kudakwa na Black Jesus ambaye alionekana akimsaka huku na kule kando ya mto ule.
Ni usiku huu ndipo alipojipa ujasiri wa kutoka vichakani, akiwa ameshajeruhiwa kwa majani na miiba yenye ncha kali mpaka alipofanikiwa kutoka nje ya mto na kukimbilia nyumbani kwa staili ya kujifichaficha.
Watu walisikitika sana.
Taarifa hizi zilipowafikia polisi walikuja kumchukua kwa uchunguzi zaidi na kumrudisha nyumbani baadae sana.
Lakini walau watu walienda kulala wakiwa na amani mtoto John alikuwa hai. Japo dukuduku liliendelea kuwatafuna wote, Black Jesus alikuwa ni nani hasa? Alikuwa kajificha wapi? Alikuwa na malengo gani?
Na vipi kuhusu madini ya zebaki, alikusudia kufanyia nini?
Siku, wiki, mwezi na hatimaye miezi ilikatika bila Black Jesus kuonekana wala kusikika! Likabaki kuwa fumbo la imani.....
Siku Jenerali Tumaniel Kiwelu alipopata habari zake alituita kwenye ofisi yake, ili aweze kutufahamu na kutupongeza pia kwa ujasiri. Na picha hii hapa chini nilipiga na bibi baada ya kutoka kwa mkuu wa mkoa wa Rukwa siku hiyo.
Lakini Black Jesus ni nani?
Alikuwa na lengo gani?
Na vipi kuhusu madini ya zebaki aliyokuwa akitembea nayo, alikusudia kuyafanyia nini?
Itaendelea...

Sijakuelewa mkuuuUnaboa,andika Kila Kwa Pc Yako Hapa Uje Copy And Paste,sisi Si Kama John Aliokuwa Anakupelekesha,jirekebishe
HowDah utamu unakuja,utqmu unakatq