Birthday For Lowassa: JK ndani ya nyumba

Birthday For Lowassa: JK ndani ya nyumba

Hata mimi nimesikia ilikuwa jana Monduli, vigogo wote wazito walikuwa huko
 
Hapa basi kwishne picha tumeliona na star tumenjua!!
 
to hell eddo!king of mafisadi
TO HELL!
I HATE YOU
 
hii inmenipa raha mkuu..the next prezidaaaa...imenipa stimu ngoja niende kutazama chelsea wakimuadhibu mtu leo

Mazee kuna wakati nakata tamaa na nchi yangu..... nachukia mfumo tulio nao.....kila mtu anaangalia tumbo lake kwa gharama za walala hoi...ama kweli sisi ni wa pipi si zaidi ya hapo! JK alifikisha ujumbe mzito sana kwa sisi wenye akili alipogawa zile pipi....

Mazee namimi ndo chama langu hilo nimevalia top ya Lamps....kila laheri ndugu yangu..
 
Party la birthday lilikuwa la aina yake.
Nilikuwepo ila simu yangu ikashindwa kuwaunga live ili wana JF muone na "kujumuika nae."
Waliokuwepo ambao mimi nawafahamu ni KARAMAGI,MNDOLWA (DAWASCO),MKUU WA CHUO,TANZANIA MILITARY ACADEMY,mhubiri maarufu MWAKASEGE,FLORA MBASHA na kundi lake la nyimbo.
Waliotambulishwa na EL ni MAASKOFU WA ANGLIKANI KUTOKA ARUSHA,KILIMAJARO,MOROGORO NA MWAKILISHI WA ASKOFU MKUU ANGLIKANI TZ,PAROKO WA KANISA KATOLIKI MONDULI.
Vikundi vya kwaya mbali mbali kama RC UNGALIMITED etc.
Wengine niliowaona,ni watu ambao huwa nawaona kwenye misafara ya JK mikoani kama wanausalama(UWT)hawa walikuwa kama 10 na ndio waongozaji wa shughuli hii.
Shughuli ilianza saa 6 mchana na kuendelea na watu walikuwa wengi maana wananchi wote wa MÖNDULI walialikwa na hakuna utambulisho wa kuingia(kadi).
Baada ya mimi kuondoka around saa 11 jioni,naambiwa kufika saa moja ndo kama sherehe ilianza maana du,...........
Nimesahau kumtaja OLE NAIKO(CTI) nae alikuwepo.
Taarifa nilizopata,zinasema party la usiku lilikuwa babkubwa kwani kila aina ya kileo kilikuwepo,tofauti na mchana ambapo kulikuwa na vinywaji laini tu,pia naambiwa MAWAZIRI NA MANAIBU MAWAZIRI WENGI PAMOJA NA WABUNGE WENGI WALIKUWEPO
NB.Wakati wa mchana,LOWASA HAKUMTAMBULISHI MWANASIASA YEYOTE AU MTU YOYOTE TOKA KUNDI LINGINE ZAIDI YA WACHUNGAJI NA MAASKOFU.
 
Last edited:
tetesi nilizozipata A-Town, hiyo licha ilikuwa birthday lakini pia ilikuwa mahsusi kwa mafisadi kujipongeza kwa mambo yaliyojili pade Dodoma kwenye vikao vya chama kwa kuweza kumbana spika Sitta
 
JK ndio kwanza anaingia Dar..... kutokea?????
 
Nasikia EL siku hizi anasali sana, msimuhukumu labda ameungama mbele ya PILATO na akasamehewa makosa yake ya zamani.

Si mnasikia alienda 'KUHIJI' Jerusalem?
5689d1251032389-a-bounce-back-by-jacob-zuma.jpg
 

Attachments

  • Bounce back by Jacob Zuma.jpg
    Bounce back by Jacob Zuma.jpg
    22.2 KB · Views: 194
tetesi nilizozipata A-Town, hiyo licha ilikuwa birthday lakini pia ilikuwa mahsusi kwa mafisadi kujipongeza kwa mambo yaliyojili pade Dodoma kwenye vikao vya chama kwa kuweza kumbana spika Sitta

TEHE Teh,
INAWEZEKANA MAANA WAKATI ANASALIMIA WAALIKWA ALISEMA "NAISHUKURU FAMILIA YANGU KWA KUNIPA USHIRIKIANO NA WAMENISHAURI MAADHIMISHO HAYA NIYAFANYE LEO BADALA YA TRH 26 AMBAYO NDIO SIKU HASA YA KUZALIWA KWANGU,ILI WAWEZE KUJUMUIKA KWA PAMOJA".
 
Hisia zangu ni kwamba uhusiano huu ni zaidi ya siasa. Huenda kuna mahusiano ya ziada kati ya mtu huyu na hao waliohudhulia pati hiyo.

Anawapa furaha gani zaidi ya siasa?
 
Kazi ipo kweli kweli...siasa ya Tanzania kweli ni mchezo wa kuigiza kwa kwenda mbele
 
Back
Top Bottom