Binti yako kama hana elimu asikanyage Dar es Salaam

Sjawahi kujua kwann nyie mlioko dar mnaaminisha watu upuuz kwmb wakfka dar kila ktu knabadilika yan n kufanikiwa tu wkt si kwel eti misosi sjui ndo ipi hiyo samaki vibua, dagaa mchele, miguu ya kuku au visgno vya kuku, utumbo wa nguruwe watu dar wana maisha magumu sn sn napaelewa vema nimezaliwa huko nimesoma huko mpk university udsm kwaiyo hakuna wa kunidanganya kwasasa npo kanda ya ziwa sjawahi tena kushawishka kurud kuish dar acha kupotosha watu.
 
Sjawahi kujua kwann nyie mlioko dar mnaaminisha watu upuuz kwmb wakfka dar kila ktu knabadilika yan n kufanikiwa tu wkt si kwel eti misosi sjui ndo ipi hiyo samaki vibua, dagaa mchele, miguu ya kuku au visgno vya kuku, utumbo wa nguruwe watu dar wana maisha magumu sn sn napaelewa vema nimezaliwa huko nimesoma huko mpk university udsm kwaiyo hakuna wa kunidanganya kwasasa npo kanda ya ziwa sjawahi tena kushawishka kurud kuish dar acha kupotosha watu.
kwa sababu una akili ndio maana unalielewa hilo, ila hamna aliyepotoshwa hapo. mimi nimetoa elimu kwa wanaoingia dar wasiige maisha ya watu, au wazazi wawafatilie watoto wao pindi wanaenda kwa ndugu na kukaa muda mrefu.
 
Ndefu kidogo....

Leo acha niseme kidogo kuhusu dada zetu tuseme Betina aka Tyner.

Picha linaanza akifika Dar, ngozi halisi inaanza kuonekana. Kumbe hakuwa mweusi tii bali ni rangi ya chokoleti. Maji ya chumvi, vipodozi, misosi flani, sabuni na mafuta anayoanza kupaka. Kombinesheni yote hii inazalisha kiumbe tofauti na kile kilichokua Itigi bondeni kule. Alikua na haki ya kujiita Tyner badala ya Betina.

Kutokana na hilo unaweza kuamini hili, kwamba hata majina yetu wazazi walitupatia kutokana na mazingira ya eneo husika. Mazingira tunayoaishi baadaye yanaanza kutulazimisha tujibatize upya majina na kuyatupa ya awali. ,abinti wanaongoza kwenye jambo hili. Betina ni mmoja wapo.

Akishafika dar hawezi kurudi Singida, akafanye nini?? wakati mwili wake ushakuwa na thamani ya shoo kadhaa za Konde Boy. Sura yake inawalazimu panya road waokoke papohapo bila kusubiri neno la Mwakasege na Kimaro wa Kijitonyama. Ashakua mzuri mpaka uzuri wenyewe unaona wivu juu ya uzuri wake. Kawa kisu kweli kweli sio tena yule Betina wa kuchunga punda Itigi.

Anarudije Manyoni? Akafanye nini na punda za Itigi? Amwachie nani viwanja vya bata hapa mjini Daslama. Ndio kwanza ameanza kuonja laadha ya utamu wa jiji hili, Rafiki yake anayeishi Sinza, aliyeanza kujitegemea baada ya kupitia njia anazopitia sasa Tyner, ndie aliyempokea, amamhifadhi, wakaishi.

Gheto lenye kila kitu ndani kinachotakiwa kwa mtoto wa kike wa mjini. Maana kuna mtoto wa kike na mtoto wa kike wa mjini. Kinavutia kuliko sura nashepu za mastaa wengi wa Bongo Movie. Kuna vyumba vya watoto wa kike vina urembo kulik warembo wenyewe.. pale mjini TikTok mnaviona. Ndo hiki alichopokelewa Tyner.

Ndo yale magheto ya watoto wa kike, ambayo mwanaume unajikuta bwege tu. Utampa nini sasa labda figo. Na Hiyo figo uwe nayo sasa, figo za masela wengi zimechakaa kama ardhi ya pale Jangwani wakati wa masika. Imechakazwa kwa sumu zote unazojua wewe hapa duniani.

Haya yote yanakuja baada ya Tyner kufukuzwa nyumbani kwa dada yake, (siyo tumbo moja ila wanatoka sehemu moja pale Itigi Singda). Ambaye alimleta Daslama kumsaidia shughuli zake za saluni. Haukupita mwaka kabla ya kuanza kuraruana kwa sababu za kipuuzi, 'Mabwana'.

Aliingia Daslama kama msichana wa kawaida sana. Mitoko na pamba alizoiga kutoka kwa wateja wa saluni ya dada, ghafla akawa kiumbe pendwa tyner. Wateja wa saluni wakageuka kuwa mawakala wa mwili wake, anauzwa kama mwanasoka na huduma yake inakuwa sio ya nchi hii. Kila pedeshee anataka kummiliki walau aonje ladha adimu kwa wasio na pesa.

Anaanza kutishia himaya ya mwenyeji wake (dada), hajioni tena kama mfanyakazi wa saluni. Kwani usiku mmoja anaingiza pesa nyingi kuliko mtaji wa saluni na faidaa zake. Itakuwa rahisi Konde Boy kurudi WCB kuliko Tyner kuendelea kuishi kwa dada. Ndipo akatimuliwa usiku usiku.

Anaempokea Sinza ni miongoni mwa wateja wa saluni, ambaye alishiriki kumnadi Tyner kwa wanaume. Mrembo ni rahisi kumjua mrembo mwenzake. Anampokea kwa bashasha la kike akijua sasa atavuna pesa za ukuwadi kwa uhuru zaidi. Wanangu wa Telegram mnaelewa.

Ungewatembelea mchana muda wote wamelala, sure zimekunjamana kwa ukosefu wa usingizi, Nyakati za jioni wakijipara, ukiwaona utashangaa na matajiri wote hapa mjini wanakosaje kuolewa? Okay sawa na waoaji hawapo na mabrazameni wanaozalisha akina Tanasha hawawaoni kina Tyner?

Mwka mmoja baada ya Tyner kulainika zaidi ngozi kuongezavifurushi vya bando kwenye umbile. Sasa anakuwa Tyner hasa, mashosti wanamchukia kwa wivu. Hajali, kwani ana marafiki wengi wa kiume kuliko wa kike na hao ndio anawahitaji. Humwambii kitu..

Anazidi kuvutia zaidi, Sinza nako hawezi kudumu kwani ugomvi kila siku juu ya wivu. Rafiki yake mmoja wa mbezi , akijua umbo la Tyner lingempa bata zaidi, anamkaribisha kwake haraka sana.

Mabwana wanakuwa wengi kuliko nywele zake, wa kila rika, rangi tofauti. Kajui kumkataa mtu mwenye kipaji na nyota ya pesa. Yeye anakuwa mmoja ya waasisi wa neno la mjini ''kudanga''. Anadanga mpaka shetani mwenyewe anaogopa na kumkana waziwazi.

Kiwanja chochote cha bata huwezi kumkosa Tyner.. Anakunywa PII TUU kila siku kama karogwa. Mtoto mzuri, mbichi, laini anahusudu wala hajui kitu kinaitwa Zana. yaani ganda la ndizi pyuu mpaka makaaa. Ndo maisha yake ya miaka sasa.

Rafiki yake wa mbezi wanazinguana anasepa. Sasa hivi kambi popote. Anaishi kwenye nyumba za wageni kama sabuni ya 'Vera'.

Kila siku anaamka giza likiingia na kuanza kukusanya hesabu kam bodaboda, mwanga ukichomoza asubuhi yeye anaingia kulala. Tyner anaishi kwa ratiba ya Marekani akiwa Jiji hili hili la Chalamila.

Utu umemtoka moyoni, nyumbani hapakumbuki, punda hawakumbuki, jiji limemkolea, anakula baa anashida baa hana hata ujuzi wa kuchemsha chai, Siyo 'Waifu matirio' tena bali ni ' waifu masali'. Maisha yake yameaharibika.

Mzazi mkoani usiruhusu mtoto wako asiyekuwa na mbele wala nyuma kielimu akaja Dslama mjini. Asilimia kubwa ya mabinti zetu wanageuka kuwa watumwa wa biashara haramu ya ngono. Wanatumikishwa kama taksi za mtandaoni, Watu 'wanarikwesti' tu inauma sana.


ITAENDELEEEAA.......
Temeke Mtoto mzuri 2k tu dar Miaka ijayo Watsjiuza kwa 1k , Samani yao imeshuka.
 
Ndefu kidogo....

Leo acha niseme kidogo kuhusu dada zetu tuseme Betina aka Tyner.

Picha linaanza akifika Dar, ngozi halisi inaanza kuonekana. Kumbe hakuwa mweusi tii bali ni rangi ya chokoleti. Maji ya chumvi, vipodozi, misosi flani, sabuni na mafuta anayoanza kupaka. Kombinesheni yote hii inazalisha kiumbe tofauti na kile kilichokua Itigi bondeni kule. Alikua na haki ya kujiita Tyner badala ya Betina.

Kutokana na hilo unaweza kuamini hili, kwamba hata majina yetu wazazi walitupatia kutokana na mazingira ya eneo husika. Mazingira tunayoaishi baadaye yanaanza kutulazimisha tujibatize upya majina na kuyatupa ya awali. ,abinti wanaongoza kwenye jambo hili. Betina ni mmoja wapo.

Akishafika dar hawezi kurudi Singida, akafanye nini?? wakati mwili wake ushakuwa na thamani ya shoo kadhaa za Konde Boy. Sura yake inawalazimu panya road waokoke papohapo bila kusubiri neno la Mwakasege na Kimaro wa Kijitonyama. Ashakua mzuri mpaka uzuri wenyewe unaona wivu juu ya uzuri wake. Kawa kisu kweli kweli sio tena yule Betina wa kuchunga punda Itigi.

Anarudije Manyoni? Akafanye nini na punda za Itigi? Amwachie nani viwanja vya bata hapa mjini Daslama. Ndio kwanza ameanza kuonja laadha ya utamu wa jiji hili, Rafiki yake anayeishi Sinza, aliyeanza kujitegemea baada ya kupitia njia anazopitia sasa Tyner, ndie aliyempokea, amamhifadhi, wakaishi.

Gheto lenye kila kitu ndani kinachotakiwa kwa mtoto wa kike wa mjini. Maana kuna mtoto wa kike na mtoto wa kike wa mjini. Kinavutia kuliko sura nashepu za mastaa wengi wa Bongo Movie. Kuna vyumba vya watoto wa kike vina urembo kulik warembo wenyewe.. pale mjini TikTok mnaviona. Ndo hiki alichopokelewa Tyner.

Ndo yale magheto ya watoto wa kike, ambayo mwanaume unajikuta bwege tu. Utampa nini sasa labda figo. Na Hiyo figo uwe nayo sasa, figo za masela wengi zimechakaa kama ardhi ya pale Jangwani wakati wa masika. Imechakazwa kwa sumu zote unazojua wewe hapa duniani.

Haya yote yanakuja baada ya Tyner kufukuzwa nyumbani kwa dada yake, (siyo tumbo moja ila wanatoka sehemu moja pale Itigi Singda). Ambaye alimleta Daslama kumsaidia shughuli zake za saluni. Haukupita mwaka kabla ya kuanza kuraruana kwa sababu za kipuuzi, 'Mabwana'.

Aliingia Daslama kama msichana wa kawaida sana. Mitoko na pamba alizoiga kutoka kwa wateja wa saluni ya dada, ghafla akawa kiumbe pendwa tyner. Wateja wa saluni wakageuka kuwa mawakala wa mwili wake, anauzwa kama mwanasoka na huduma yake inakuwa sio ya nchi hii. Kila pedeshee anataka kummiliki walau aonje ladha adimu kwa wasio na pesa.

Anaanza kutishia himaya ya mwenyeji wake (dada), hajioni tena kama mfanyakazi wa saluni. Kwani usiku mmoja anaingiza pesa nyingi kuliko mtaji wa saluni na faidaa zake. Itakuwa rahisi Konde Boy kurudi WCB kuliko Tyner kuendelea kuishi kwa dada. Ndipo akatimuliwa usiku usiku.

Anaempokea Sinza ni miongoni mwa wateja wa saluni, ambaye alishiriki kumnadi Tyner kwa wanaume. Mrembo ni rahisi kumjua mrembo mwenzake. Anampokea kwa bashasha la kike akijua sasa atavuna pesa za ukuwadi kwa uhuru zaidi. Wanangu wa Telegram mnaelewa.

Ungewatembelea mchana muda wote wamelala, sure zimekunjamana kwa ukosefu wa usingizi, Nyakati za jioni wakijipara, ukiwaona utashangaa na matajiri wote hapa mjini wanakosaje kuolewa? Okay sawa na waoaji hawapo na mabrazameni wanaozalisha akina Tanasha hawawaoni kina Tyner?

Mwka mmoja baada ya Tyner kulainika zaidi ngozi kuongezavifurushi vya bando kwenye umbile. Sasa anakuwa Tyner hasa, mashosti wanamchukia kwa wivu. Hajali, kwani ana marafiki wengi wa kiume kuliko wa kike na hao ndio anawahitaji. Humwambii kitu..

Anazidi kuvutia zaidi, Sinza nako hawezi kudumu kwani ugomvi kila siku juu ya wivu. Rafiki yake mmoja wa mbezi , akijua umbo la Tyner lingempa bata zaidi, anamkaribisha kwake haraka sana.

Mabwana wanakuwa wengi kuliko nywele zake, wa kila rika, rangi tofauti. Kajui kumkataa mtu mwenye kipaji na nyota ya pesa. Yeye anakuwa mmoja ya waasisi wa neno la mjini ''kudanga''. Anadanga mpaka shetani mwenyewe anaogopa na kumkana waziwazi.

Kiwanja chochote cha bata huwezi kumkosa Tyner.. Anakunywa PII TUU kila siku kama karogwa. Mtoto mzuri, mbichi, laini anahusudu wala hajui kitu kinaitwa Zana. yaani ganda la ndizi pyuu mpaka makaaa. Ndo maisha yake ya miaka sasa.

Rafiki yake wa mbezi wanazinguana anasepa. Sasa hivi kambi popote. Anaishi kwenye nyumba za wageni kama sabuni ya 'Vera'.

Kila siku anaamka giza likiingia na kuanza kukusanya hesabu kam bodaboda, mwanga ukichomoza asubuhi yeye anaingia kulala. Tyner anaishi kwa ratiba ya Marekani akiwa Jiji hili hili la Chalamila.

Utu umemtoka moyoni, nyumbani hapakumbuki, punda hawakumbuki, jiji limemkolea, anakula baa anashida baa hana hata ujuzi wa kuchemsha chai, Siyo 'Waifu matirio' tena bali ni ' waifu masali'. Maisha yake yameaharibika.

Mzazi mkoani usiruhusu mtoto wako asiyekuwa na mbele wala nyuma kielimu akaja Dslama mjini. Asilimia kubwa ya mabinti zetu wanageuka kuwa watumwa wa biashara haramu ya ngono. Wanatumikishwa kama taksi za mtandaoni, Watu 'wanarikwesti' tu inauma sana.


ITAENDELEEEAA.......


Elimu, sio, kabisa kigezo cha kuishi Dar.
 
Wanawake wote unaowaona dsm Ni kama bots ,ukiwa na Hela unarequest tu ...pisi hiyoo hapo ,unakula mpaka morning
 
Back
Top Bottom