Binti aua mwanaye kwa kumtumbukiza kwenye ndoo ya maji

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Dec 11, 2012
5,897
10,358
Siku moja tangu Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 19 aitwae Johari Twaha, Mkazi wa mtaa wa Kigamboni Mkoani Iringa akamatwe na Polisi kwa tuhuma za kumtumbukiza kwenye ndoo ya maji ya lita ishirini na kumuua Mtoto wake mwenye umri wa miezi saba, Polisi wamesema Johari aliua Mtoto ili aende Dar es salaam kutafuta maisha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Allan Bukumbi amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo ambapo amesema Johari alimuua Mtoto kwasababu alikuwa anataka kwenda Dar es salaam kwa Baba yake kwa ajili ya kutafuta maisha.

"Huyu Binti alimuua Mtoto kwasababu Baba yake huyu Binti (Babu wa Mtoto) yupo Dar es salaam kwahiyo aliitwa na Baba yake kwenda Dar es salaam kwa ajili ya kuhangaika na maisha yeye anasema Iringa maisha ni magumu yamemshinda kwahiyo Baba yake alimpa masharti kuwa aende Dar es salaam bila Mtoto”

Johari alitekeleza mauaji hayo November 19,2023 saa tano katika eneo la Mawelewele Mkoani Iringa kwa kumtumbukiza mwanaye kwenye ndoo iliyopo chooni kichwa chini miguu juu na kusababisha kifo chake.
 
Siku moja tangu Mwanamke mmoja mwenye umri wa miaka 19 aitwae Johari Twaha, Mkazi wa mtaa wa Kigamboni Mkoani Iringa akamatwe na Polisi kwa tuhuma za kumtumbukiza kwenye ndoo ya maji ya lita ishirini na kumuua Mtoto wake mwenye umri wa miezi saba, Polisi wamesema Johari aliua Mtoto ili aende Dar es salaam kutafuta maisha.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Allan Bukumbi amethibitisha kutokea kwa mauaji hayo ambapo amesema Johari alimuua Mtoto kwasababu alikuwa anataka kwenda Dar es salaam kwa Baba yake kwa ajili ya kutafuta maisha.

"Huyu Binti alimuua Mtoto kwasababu Baba yake huyu Binti (Babu wa Mtoto) yupo Dar es salaam kwahiyo aliitwa na Baba yake kwenda Dar es salaam kwa ajili ya kuhangaika na maisha yeye anasema Iringa maisha ni magumu yamemshinda kwahiyo Baba yake alimpa masharti kuwa aende Dar es salaam bila Mtoto”

Johari alitekeleza mauaji hayo November 19,2023 saa tano katika eneo la Mawelewele Mkoani Iringa kwa kumtumbukiza mwanaye kwenye ndoo iliyopo chooni kichwa chini miguu juu na kusababisha kifo chake.
Polisi wamesema Johari aliua Mtoto ili aende Dar es salaam kutafuta maisha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom