Mzee Mwanakijiji
Platinum Member
- Mar 10, 2006
- 33,378
- 39,319
Yep! Hicho ndicho kichwa cha habari kwenye ippmedia.com cha habari ifuatayo:
Binti apachikwa mimba na mwenziye
2007-10-11 16:36:12
Na Janeth Kiure, Kibaha
Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Lupondo, Paulina Ciaga amefukuzwa shule baada ya kubainika kuwa amepewa ujauzito na mwanafunzi mwenzie wa kidato cha kwanza.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani Henry Salewi amesema mwanafunzi huyo alitimliwa shule jana mishale ya saa 7:00 mchana alipobainika kuwa na ujauzito a miezi sita.
Amesema Kamanda Salewi kuwa binti huyo alipohojiwa kuhusiana na mtu aliyempa ujauzito, akamtaja kijana Bakari Busoji ambaye pia ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule yao kuwa ndIye aliyempa ujauzito huo.
Kamanda Salewi akasema Polisi ilipomfuatilia mtuhumiwa huyo ailikuta ameshatoroka na kwenda kusiko julikana na hivyo anaendelea kusakwa na Jashi hilo.
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi mkoani Pwani linaashikilia Mbaraka Omary, 14, Jasta Antony, 27 na Thabit Khalfan, 27 kwa tuhuma za kukutwa wakiwa na gramu 15 za bangi.
Kamanda Salewi amesema watu hao walikamatwa jana mishale ya saa 2:30 katika uwanja wa mpira wa Nyundo wakati Polisi walipofanya msako katika eneo hilo.
Kamanda Salewi amesema Jeshi lake pia linamshikilia Benedict John aliyekamatwa akiawa na lita 10 za pombe haramu ya gongo.
Akasema mtuhumiwa huyo alikamatwa jana mishale ya saa 4:00 asubuhi huko Kimanzichana wilayani Mkuranga akiwa na kiasi hicho cha gongo.
Pia Kamanda Salewi amesema mtuhumiwa mwingine RamadhaniNyawimba pia alikamatwa jana mishale ya 2:30 katika kijiji cha Tangisini akiwa na lita 60 za pombe haramu ya gongo.
Akasema watuhumiwa wote ni watumiaji na wauzaji wa pombe hiyo, jambo ambalo ni kinyume na sheria za nchi.
Kamanda Salewi amesema watuhumiwa wote wataburuzwa mahakamani wakati wowote baada ya Polisi kukamilisha upelelezi wao.
SOURCE: Alasiri
Binti apachikwa mimba na mwenziye
2007-10-11 16:36:12
Na Janeth Kiure, Kibaha
Mwanafunzi wa kidato cha pili katika Shule ya Sekondari Lupondo, Paulina Ciaga amefukuzwa shule baada ya kubainika kuwa amepewa ujauzito na mwanafunzi mwenzie wa kidato cha kwanza.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Pwani Henry Salewi amesema mwanafunzi huyo alitimliwa shule jana mishale ya saa 7:00 mchana alipobainika kuwa na ujauzito a miezi sita.
Amesema Kamanda Salewi kuwa binti huyo alipohojiwa kuhusiana na mtu aliyempa ujauzito, akamtaja kijana Bakari Busoji ambaye pia ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika shule yao kuwa ndIye aliyempa ujauzito huo.
Kamanda Salewi akasema Polisi ilipomfuatilia mtuhumiwa huyo ailikuta ameshatoroka na kwenda kusiko julikana na hivyo anaendelea kusakwa na Jashi hilo.
Wakati huo huo, Jeshi la Polisi mkoani Pwani linaashikilia Mbaraka Omary, 14, Jasta Antony, 27 na Thabit Khalfan, 27 kwa tuhuma za kukutwa wakiwa na gramu 15 za bangi.
Kamanda Salewi amesema watu hao walikamatwa jana mishale ya saa 2:30 katika uwanja wa mpira wa Nyundo wakati Polisi walipofanya msako katika eneo hilo.
Kamanda Salewi amesema Jeshi lake pia linamshikilia Benedict John aliyekamatwa akiawa na lita 10 za pombe haramu ya gongo.
Akasema mtuhumiwa huyo alikamatwa jana mishale ya saa 4:00 asubuhi huko Kimanzichana wilayani Mkuranga akiwa na kiasi hicho cha gongo.
Pia Kamanda Salewi amesema mtuhumiwa mwingine RamadhaniNyawimba pia alikamatwa jana mishale ya 2:30 katika kijiji cha Tangisini akiwa na lita 60 za pombe haramu ya gongo.
Akasema watuhumiwa wote ni watumiaji na wauzaji wa pombe hiyo, jambo ambalo ni kinyume na sheria za nchi.
Kamanda Salewi amesema watuhumiwa wote wataburuzwa mahakamani wakati wowote baada ya Polisi kukamilisha upelelezi wao.
SOURCE: Alasiri