Binti afunguka kuwa mwanaume aliyefungwa miaka 30 jela siye aliyempa ujauzito

Melki the Storyteller

JF-Expert Member
May 3, 2022
5,700
9,778
Hakika wanawake si binadamu, ni viumbe wa ajabu sana kulinganishwa na majini au hata nyoka. TUISHI NAO KWA AKILI

Mwaka 2017 huyu binti alikuwa kidato cha nne. Kwa bahati mbaya alipata ujauzito mwezi wa tatu. Juhudi za kumtafuta mhusika zilimwangukia kijana aliyekuwa anachukua diploma ya unesi katika college X.

Tulimshambulia kwa maneno makali na laana za kutosha kwa dhambi ya kuzikatisha ndoto za binti wa baba wa rafiki yangu ambaye familia yetu na yake zinaheshimiana na zina historia ndefu kidogo huko nyuma.

Kama ilivyo ada, sheria ilifuata mkondo wake. Baada ya mchakato kukamilika, kijana alihukumiwa kifungo cha miaka 30.

Nami kwa mara ya kwanza nilihudhuria hukumu hiyo mahakamani na ndipo kuthibitisha kuwa kumbe kifungo cha kumbebesha ujauzito mwanafunzi huwa kipo, na ndipo nilipoanza kuwaogopa watoto wa kike wanaovaa sketi zenye marinda.

Ujauzito wa binti ulilelewa na familia yake japo baba wa binti alikuwa tayari kashamfukuza binti yake ambaye alitoweka kwa kipindi cha takribani wiki mbili nyumbani, lakini baadae aliamua kupunguza hasira. Binti alifanikisha kujifungua kitoto cha kiume.

Mwaka 2018 mwezi wa tatu/ wa nne, kama sijasahau ilikuwa ni wiki ya pasaka, alijitokeza kijana akatangaza nia ya kumuoa, inavyosemekana walifahamiana wakiwa kanisani anaposali binti! Huyu kijana alifanya kazi ya kuuza matunda.

Familia ya binti iliamua kukubaliana na matokeo ili kupunguza mzigo nyumbani na kuepusha ile hali ya binti kubeba ujauzito wa pili akiwa nyumbani. Basi, ndoa ikapangwa, hatua zikafuatwa, binti akaolewa pasi na mahari.

Mwezi mmoja baadae, familia ya binti ikajipanga, ikachanga pesa kwa ajili ya mtaji ilikusudi binti yao aishi maisha mema akiwa na mmewe huyo. Walifungua biashara ya maana tu. Maisha yakasonga, kukawepo ushemeji, tukasahau tukio kabisa.

Mwezi June mwaka huu (2022) kulitokea sintofahamu katika ndoa ya binti kiasi cha kutengana kabisa, yeye na mumewe, ila ni baada ya kipigo kitakatifu alichoambulia binti.

Mume alitokomea kusikojulikana akiwa na mapato karibu yote ya biashara waliyokuwa wanaendesha na mtaji juu, kilichobaki kwenye duka lao hilo la jumla ni bidhaa tu.

Binti aliamua kurejea nyumbani kwa wazazi wake ili kutuliza akili, lakini tokea kufika kwake nyumbani pale, wazazi wake wamekuwa wakitutaarifu kuwa binti yao akili haitulii, hajatulia kabisa na amekuwa kama mtu aliyeathiriwa kisaikolojia. Muda mwingine huzungumza peke yake, kulia lia tu, kuzubaa. Istoshe hapo alipo ana ujauzito wa miezi miwili.

Katikati ya mwezi huu wa nane, baadhi ya watu muhimu kutoka familia yetu ukiniongeza mimi ambaye sielewi ni kwanini wameona ni vyema kushiriki mipango hiyo tuliitwa kwenye kikao cha dharura cha familia yao, ndipo baba wa binti alivyotueleza kuwa, binti yake amekili kuwa kijana aliyefungwa jela siye mwenye mtoto wa kwanza wa binti.

Bali mwenye mtoto ni huyo mwanaume aliyemuoa binti! Inavyosemekana katika mahusiano yao, walijikuta wakipeana ujauzito kimasihara. Kwa kuwa binti alimpenda sana mhusika, alikubali kusikiliza ushauri wake aliopewa wa kumtafuta mwanaume mwingine na kumbambikizia ujauzito ili kumnusuru mwanaume huyo kwenda jela ili mtoto apate malezi ya baba aliye sahihi.

Kwa kuwa binti alimpenda mwanaume huyo, hakuona tatizo kufuata ushauri huo

Mpaka sasa hakuna mchango wa maana wa mawazo uliotolewa!

Nimekuwa nikijiuliza, hivi kuna uwezekano wowote wa ku cancel kifungo? Kwa kuwa binti kakili kuwa yule kijana si mhusika?

Kila siku huwa nawakumbusha kuwa wanawake sio watu wazuri, mnaniona kuwa ni mtu mwenye chuki binafsi! Mnaona sasa?
 
Mosi, kutembea na mtoto wa shule ni kosa la ubakaji, hata kama hujampa mimba. Hivyo kama jamaa alilala naye kweli itakuwa ni shida. Japo kama hakulala naye na ninyi mkaamua kumsingizia, nadhani kuna shida pahala. Lakini, nabaki kujiuliza, huyo hakimu aliwezaje kufikia maamuzi kiholela-holela tu (Kama hii siyo CHAI, basi hakimu naye ana shida kubwa). Kuna utaratibu maalumu wa kupima ushahidi kwenye kesi za ubakaji.

Miaka ya nyuma kesi kama hii ilitokea sema tofauti kidogo. Jamaa aliletwa mahakamani, lakini binti alichelewa kupimwa hospitalini. Vipimo vya hospitalini vilionesha kwamba binti huyo ameanza michezo hiyo muda mrefu, hata kabla hajaanza mahusiano na huyo jamaa. Tena ikaonyesha alikuwa na wanaume wengine siku za karibuni. Kuzingatia hili jamaa akachomoka vizuri tu.

Kuna mambo mengi ya kuzingatia kabla hujatoa hukumu ya ubakaji, hatusikilizi tu ushahidi wa mhanga (Binti aliyebakwa), kune mengi tunazingatia. Aidha hakimu hakuyazingatia au hii Thread ni CHAI.

Pili, nadhani ifike mahali sheria zetu za uzazi na ndoa zipitiwe upya, maana PATERNITY FRAUD imekuwa kubwa. Wanaume wengi wanabebeshwa mizigo mikubwa ya kulazimishwa kulea watoto wasio wao. Sheria ya Tanzania kama ya Uingereza ina kitu wanaita PRESUMPTION OF PATERNITY, kwamba kama mwanaume umeoa mke au unaishi na mwanamke (Cohabitation), ikitokea kazaa mtoto basi moja kwa moja huyo mtoto ni wako na unatakiwa kumlea bila hata vipimo vya kibaiolojia.

Hii siyo sahihi, kama mwanaume ataamua kulea mtoto asiye wake basi iwe kwa hiari yake mwenyewe, japo nadhani PATERNITY TEST (DNA TESTING), iwe lazima ili kuwalinda watoto wa kiume. Sheria iwekwe kabisa kwamba mtoto akizaliwa ni lazima apimwe. Vipimo vikishapatikana basi sheria ichukue mkondo wake, ambapo kama ni kweli itabidi mwanaume alee na kama siyo kweli mwanamke aliyesababisha FRAUD amlipe huyo mwanaume.
 
Hakika wanawake si binadamu, ni viumbe wa ajabu sana kulinganishwa na majini au hata nyoka. TUISHI NAO KWA AKILI



Kwa kuwa binti alimpenda mwanaume huyo, hakuona tatizo kufuata ushauri huo

Mpaka sasa hakuna mchango wa maana wa mawazo uliotolewa!

Nimekuwa nikijiuliza, hivi kuna uwezekano wowote wa ku cancel kifungo? Kwa kuwa binti kakili kuwa yule kijana si mhusika?

Kila siku huwa nawakumbusha kuwa wanawake sio watu wazuri, mnaniona kuwa ni mtu mwenye chuki binafsi! Mnaona sasa?
Kwa nini kijana asingebisha Ili wapime DNA?
 
Hizi kesi nadhani kuna umuhimu wa kuweka kifungu, kwamba lazima ipimwe DNA baada ya mtoto kuzaliwa ili hukumu iwe halali.... hata kama itabidi mtuhumiwa akae rumande mpaka mtoto azaliwe ni bora kuliko utaratibu wa sasa.

Maan inawezakana kabisa binti akawa na mahusiano na wanaume wengi, na hata asijue aliyempa mimba ni nani, balaa likamwangukia wa karibu.
 
Binadamu sio watu wazuri, sio wanawake tu. Kwani huyo kijana hakujitetea kwenu kuwa hana mahusiano na huyo binti? Unless kama alikuwa na mahusiano naye basi atakuwa amejifunza kuwa hutakiwi kutembea na mwanafunzi hata usipompa mimba.
 
Hii sheria ya miaka 30 kisa mimba kwa kweli naiona kama ajenda flani ya siri juu ya wanaume. Ni yakikatili sana. Na angalu ingekuwa inasubili uthibitisho wa DNA.

Nina watoto wa kike ila sidhani kama nitabariki mtoto wa watu afungwe miaka 30 kwa sababu ya nyege za binti yangu vinginevyo ithibitike pasipo shaka kabisa kuwa alibakwa. Na kama kubakwa hapa namaanisha alimlazishwa kwa nguvu.

Nawapa pole sana walio jela kwa hizi kesi zilizosababishwa na watu wakatili kuwahi kuishi katika uso wa dunia.

Nyege ni kwa wote, umamfunga mmoja unamwacha mwingine. Nani sasa atalea huyo mtoto
 
Hizi kesi nadhani kuna umuhimu wa kuweka kifungu, kwamba lazima ipimwe DNA baada ya mtoto kuzaliwa ili hukumu iwe halali.... hata kama itabidi mtuhumiwa akae rumande mpaka mtoto azaliwe ni bora kuliko utaratibu wa sasa.

Maan inawezakana kabisa binti akawa na mahusiano na wanaume wengi, na hata asijue aliyempa mimba ni nani, balaa likamwangukia wa karibu.
Ibaki hivyohivyo maana balaa linamwangukia aliye mwagia ndani hata kama bao lake halikurutubisha.
 
Mi ndo maana nasema ni ajenda flani ya siri sana juu ya wanaume ambayo wanaojiita wanasheria wameicope kichwa kichwa
Hizi kesi nadhani kuna umuhimu wa kuweka kifungu, kwamba lazima ipimwe DNA baada ya mtoto kuzaliwa ili hukumu iwe halali.... hata kama itabidi mtuhumiwa akae rumande mpaka mtoto azaliwe ni bora kuliko utaratibu wa sasa.

Maan inawezakana kabisa binti akawa na mahusiano na wanaume wengi, na hata asijue aliyempa mimba ni nani, balaa likamwangukia wa karibu.
 
Hizi kesi nadhani kuna umuhimu wa kuweka kifungu, kwamba lazima ipimwe DNA baada ya mtoto kuzaliwa ili hukumu iwe halali.... hata kama itabidi mtuhumiwa akae rumande mpaka mtoto azaliwe ni bora kuliko utaratibu wa sasa.

Maan inawezakana kabisa binti akawa na mahusiano na wanaume wengi, na hata asijue aliyempa mimba ni nani, balaa likamwangukia wa karibu.
Ukikamatwa na mwanafunzi hata bila kumpa mimba nadhani gereza linakuhusu. Mimba nadhani ni matokeo na uthibitisho tu kuwa huyu mwanafunzi kuna aliyetembea nae anatakiwa apatikane.

Ni kama ukikutwa unahudumia bangi shambani kwako, hata kama hutaivuta wewe ni tatizo.
 
Hizi kesi nadhani kuna umuhimu wa kuweka kifungu, kwamba lazima ipimwe DNA baada ya mtoto kuzaliwa ili hukumu iwe halali.... hata kama itabidi mtuhumiwa akae rumande mpaka mtoto azaliwe ni bora kuliko utaratibu wa sasa.

Maan inawezakana kabisa binti akawa na mahusiano na wanaume wengi, na hata asijue aliyempa mimba ni nani, balaa likamwangukia wa karibu.
... hoja ya msingi hapa sio kuzaa bali "kutembea" na binti wa shule au under 18; hiyo peke yake (haihitaji kutia mimba au kuzaa) inakupeleka jela miaka 30. Hoja yako ya DNA test ina mashiko kwa kesi za kubambikiwa watoto.
 
Tatizo la hili sheria ni kumfunga baba..
... kwa sababu baba ni mtu mzima (18+) hivyo alijua kwa akili zake timamu anavunja sheria tofauti na binti (under 18) ni mtoto mdogo hana ufahamu kwamba anavunja sheria.
 
Hakika wanawake si binadamu, ni viumbe wa ajabu sana kulinganishwa na majini au hata nyoka. TUISHI NAO KWA AKILI

Mwaka 2017 huyu binti alikuwa kidato cha nne. Kwa bahati mbaya alipata ujauzito mwezi wa tatu. Juhudi za kumtafuta mhusika zilimwangukia kijana aliyekuwa anachukua diploma ya unesi katika college X.

Tulimshambulia kwa maneno makali na laana za kutosha kwa dhambi ya kuzikatisha ndoto za binti wa baba wa rafiki yangu ambaye familia yetu na yake zinaheshimiana na zina historia ndefu kidogo huko nyuma.

Kama ilivyo ada, sheria ilifuata mkondo wake. Baada ya mchakato kukamilika, kijana alihukumiwa kifungo cha miaka 30.

Nami kwa mara ya kwanza nilihudhuria hukumu hiyo mahakamani na ndipo kuthibitisha kuwa kumbe kifungo cha kumbebesha ujauzito mwanafunzi huwa kipo, na ndipo nilipoanza kuwaogopa watoto wa kike wanaovaa sketi zenye marinda.

Ujauzito wa binti ulilelewa na familia yake japo baba wa binti alikuwa tayari kashamfukuza binti yake ambaye alitoweka kwa kipindi cha takribani wiki mbili nyumbani, lakini baadae aliamua kupunguza hasira. Binti alifanikisha kujifungua kitoto cha kiume.

Mwaka 2018 mwezi wa tatu/ wa nne, kama sijasahau ilikuwa ni wiki ya pasaka, alijitokeza kijana akatangaza nia ya kumuoa, inavyosemekana walifahamiana wakiwa kanisani anaposali binti! Huyu kijana alifanya kazi ya kuuza matunda.

Familia ya binti iliamua kukubaliana na matokeo ili kupunguza mzigo nyumbani na kuepusha ile hali ya binti kubeba ujauzito wa pili akiwa nyumbani. Basi, ndoa ikapangwa, hatua zikafuatwa, binti akaolewa pasi na mahari.

Mwezi mmoja baadae, familia ya binti ikajipanga, ikachanga pesa kwa ajili ya mtaji ilikusudi binti yao aishi maisha mema akiwa na mmewe huyo. Walifungua biashara ya maana tu. Maisha yakasonga, kukawepo ushemeji, tukasahau tukio kabisa.

Mwezi June mwaka huu (2022) kulitokea sintofahamu katika ndoa ya binti kiasi cha kutengana kabisa, yeye na mumewe, ila ni baada ya kipigo kitakatifu alichoambulia binti.

Mume alitokomea kusikojulikana akiwa na mapato karibu yote ya biashara waliyokuwa wanaendesha na mtaji juu, kilichobaki kwenye duka lao hilo la jumla ni bidhaa tu.

Binti aliamua kurejea nyumbani kwa wazazi wake ili kutuliza akili, lakini tokea kufika kwake nyumbani pale, wazazi wake wamekuwa wakitutaarifu kuwa binti yao akili haitulii, hajatulia kabisa na amekuwa kama mtu aliyeathiriwa kisaikolojia. Muda mwingine huzungumza peke yake, kulia lia tu, kuzubaa. Istoshe hapo alipo ana ujauzito wa miezi miwili.

Katikati ya mwezi huu wa nane, baadhi ya watu muhimu kutoka familia yetu ukiniongeza mimi ambaye sielewi ni kwanini wameona ni vyema kushiriki mipango hiyo tuliitwa kwenye kikao cha dharura cha familia yao, ndipo baba wa binti alivyotueleza kuwa, binti yake amekili kuwa kijana aliyefungwa jela siye mwenye mtoto wa kwanza wa binti.

Bali mwenye mtoto ni huyo mwanaume aliyemuoa binti! Inavyosemekana katika mahusiano yao, walijikuta wakipeana ujauzito kimasihara. Kwa kuwa binti alimpenda sana mhusika, alikubali kusikiliza ushauri wake aliopewa wa kumtafuta mwanaume mwingine na kumbambikizia ujauzito ili kumnusuru mwanaume huyo kwenda jela ili mtoto apate malezi ya baba aliye sahihi.

Kwa kuwa binti alimpenda mwanaume huyo, hakuona tatizo kufuata ushauri huo

Mpaka sasa hakuna mchango wa maana wa mawazo uliotolewa!

Nimekuwa nikijiuliza, hivi kuna uwezekano wowote wa ku cancel kifungo? Kwa kuwa binti kakili kuwa yule kijana si mhusika?

Kila siku huwa nawakumbusha kuwa wanawake sio watu wazuri, mnaniona kuwa ni mtu mwenye chuki binafsi! Mnaona sasa?
Hatari mkuuu Hawa viumbe Hawa viazi sna tu siamini kbsa kma Kuna mapenzi ya dhati

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom