Rutashubanyuma
JF-Expert Member
- Sep 24, 2010
- 219,470
- 911,174
Binti aacha shule akidai naye ameoteshwa
Imeandikwa na Na Abby Nkungu, Singida; Tarehe: 15th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 54; Jumla ya maoni: 0
WIMBI la watu wanaojitangaza wakidai wameoteshwa na Mungu kuweza kutoa tiba ya magonjwa sugu, limezidi kukua, safari hii ameibuka binti mwenye umri wa miaka 19 ambaye amelazimika kuacha shule aweze kujikita katika utoaji wa tiba ya kikombe.
Binti huyo, Zubeda Nassoro ni mwanafunzi wa Kidato cha Tatu katika shule ya Sekondari ya Mungumaji iliyopo katika Manispaa ya Singida. Zubeda amekiri kuacha shule, akisisitiza ameoteshwa na Mungu ili kutoa tiba mbadala ya magonjwa sugu yakiwemo Kifua kikuu, kifafa, kansa, kisukari na ukimwi.
Tofauti na watu wengine waliooteshwa kutoa kikombe, akiwamo mwasisi wa tiba hiyo, Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Masapila wa kijiji cha Samunge, Loliondo wilayani Ngorongoro, Zubeda yeye anatoza sh 1,100 kwa tiba ya ukimwi akidai mgonjwa atapona ndani ya siku tatu, huku magonjwa mengine yakichukua saa tano kupona.
Binti huyo, akizungumza nyumbani kwao katika kitongoji cha Irao- Nkuhi kijiji cha Mungumaji nje kidogo ya mji wa Singida alisema kuwa, katika miaka ya nyuma, alikuwa akitibu magonjwa ya kawaida kama malaria, kuhara na mengine mengi.
Alisema kuwa mapema mwezi Machi mwaka huu akiwa usingizini, alioteshwa na Mungu kwamba sasa ataacha kutibu magonjwa ya kawaida na ataanza rasmi kazi ya kutibu magonjwa sugu.
Alisema kuwa katika kuoteshwa huko, alielekezwa kwamba dawa za kutibu magonjwa sugu ni magome ya mti wa mwembe na kwamba malighafi hiyo ataipata kwa wingi mkoani Tabora. Akifafanua zaidi, alisema kila mgonjwa atapaswa kuja na kikombe chake na atalipa gharama
ya dawa sh 1,100/= tu.
Sh 500 ni kwa ajili ya mhudumu wake, Sh 500 atalipwa mtu atakayekuwa analeta magome ya mti wa mwembe kwa maelezo katika ndoto aliambiwa asiwe anafuata magome. Kiasi cha Sh 100 kitakachobaki kitakuwa mali yake.
Baba mzazi wa Zubeda, Nassoro Hamisi (44), alisema katika ukoo wao, wamewahi kuwa na watu wengi tu waliokuwa wakijishughulisha na kutibu kwa kutumia dawa za miti shamba.
Mkuu wa wilaya ya Singida, Pascal Mabiti amekiri kupata taarifa ya binti huyo kuoteshwa kutibu magonjwa sugu matano. Hata hivyo amesema ameshaaagiza wataalamu wa afya kuifanyia uchunguzi dawa hiyo.
Wakati binti huyo akiibuka mkoani Singida, mwandishi Joachim Nyambo anaripoti kutoka Chunya kuwa, mlemavu wa macho asiyeona kabisa, Simon Mahela naye ameibuka na kuanza kutoa tiba ya `kikombe, akidai naye ameoteshwa kutoa tiba itakayofanya kazi na kuponya kabisa magonjwa katika kipindi cha siku 43.
Alianza kutoa tiba hiyo katikati ya wiki iliyopita katika kijiji cha Mbuyuni, wilayani hapa kwa gharama ya Sh 500.
Wakazi hao walise awali mtaalamu huyo alidai kuoteshwa mara kadhaa na babu yake ambaye sasa ni marehemu, lakini alikuwa akidharau hadi ilipofikia siku hiyo alipomuomba kijana mmoja amsindikize katika milima ya Iseche, Tarafa ya Kwimba, wilayani hapa kwa lengo la kuutafuta mti anaodai kuutumia kutibia magonjwa sugu.
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Mbuyuni, Romwad Mwashiuya alithibitisha kuibuka kwa mkazi huyo wa Mbuyuni na kusema kuwa Mahela anaishi kwa msaada wa kuongozwa na watu wa karibu.
Imeandikwa na Na Abby Nkungu, Singida; Tarehe: 15th April 2011 @ 23:59 Imesomwa na watu: 54; Jumla ya maoni: 0
WIMBI la watu wanaojitangaza wakidai wameoteshwa na Mungu kuweza kutoa tiba ya magonjwa sugu, limezidi kukua, safari hii ameibuka binti mwenye umri wa miaka 19 ambaye amelazimika kuacha shule aweze kujikita katika utoaji wa tiba ya kikombe.
Binti huyo, Zubeda Nassoro ni mwanafunzi wa Kidato cha Tatu katika shule ya Sekondari ya Mungumaji iliyopo katika Manispaa ya Singida. Zubeda amekiri kuacha shule, akisisitiza ameoteshwa na Mungu ili kutoa tiba mbadala ya magonjwa sugu yakiwemo Kifua kikuu, kifafa, kansa, kisukari na ukimwi.
Tofauti na watu wengine waliooteshwa kutoa kikombe, akiwamo mwasisi wa tiba hiyo, Mchungaji Mstaafu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Ambilikile Masapila wa kijiji cha Samunge, Loliondo wilayani Ngorongoro, Zubeda yeye anatoza sh 1,100 kwa tiba ya ukimwi akidai mgonjwa atapona ndani ya siku tatu, huku magonjwa mengine yakichukua saa tano kupona.
Binti huyo, akizungumza nyumbani kwao katika kitongoji cha Irao- Nkuhi kijiji cha Mungumaji nje kidogo ya mji wa Singida alisema kuwa, katika miaka ya nyuma, alikuwa akitibu magonjwa ya kawaida kama malaria, kuhara na mengine mengi.
Alisema kuwa mapema mwezi Machi mwaka huu akiwa usingizini, alioteshwa na Mungu kwamba sasa ataacha kutibu magonjwa ya kawaida na ataanza rasmi kazi ya kutibu magonjwa sugu.
Alisema kuwa katika kuoteshwa huko, alielekezwa kwamba dawa za kutibu magonjwa sugu ni magome ya mti wa mwembe na kwamba malighafi hiyo ataipata kwa wingi mkoani Tabora. Akifafanua zaidi, alisema kila mgonjwa atapaswa kuja na kikombe chake na atalipa gharama
ya dawa sh 1,100/= tu.
Sh 500 ni kwa ajili ya mhudumu wake, Sh 500 atalipwa mtu atakayekuwa analeta magome ya mti wa mwembe kwa maelezo katika ndoto aliambiwa asiwe anafuata magome. Kiasi cha Sh 100 kitakachobaki kitakuwa mali yake.
Baba mzazi wa Zubeda, Nassoro Hamisi (44), alisema katika ukoo wao, wamewahi kuwa na watu wengi tu waliokuwa wakijishughulisha na kutibu kwa kutumia dawa za miti shamba.
Mkuu wa wilaya ya Singida, Pascal Mabiti amekiri kupata taarifa ya binti huyo kuoteshwa kutibu magonjwa sugu matano. Hata hivyo amesema ameshaaagiza wataalamu wa afya kuifanyia uchunguzi dawa hiyo.
Wakati binti huyo akiibuka mkoani Singida, mwandishi Joachim Nyambo anaripoti kutoka Chunya kuwa, mlemavu wa macho asiyeona kabisa, Simon Mahela naye ameibuka na kuanza kutoa tiba ya `kikombe, akidai naye ameoteshwa kutoa tiba itakayofanya kazi na kuponya kabisa magonjwa katika kipindi cha siku 43.
Alianza kutoa tiba hiyo katikati ya wiki iliyopita katika kijiji cha Mbuyuni, wilayani hapa kwa gharama ya Sh 500.
Wakazi hao walise awali mtaalamu huyo alidai kuoteshwa mara kadhaa na babu yake ambaye sasa ni marehemu, lakini alikuwa akidharau hadi ilipofikia siku hiyo alipomuomba kijana mmoja amsindikize katika milima ya Iseche, Tarafa ya Kwimba, wilayani hapa kwa lengo la kuutafuta mti anaodai kuutumia kutibia magonjwa sugu.
Ofisa Mtendaji wa Kata ya Mbuyuni, Romwad Mwashiuya alithibitisha kuibuka kwa mkazi huyo wa Mbuyuni na kusema kuwa Mahela anaishi kwa msaada wa kuongozwa na watu wa karibu.