Bingu Mutharika afariki rasmi

Hili ni pigo kwa wanampinduzi wote, ni pigo kwa wapinzani wa mabeberu na silaha zao IMF na World Bank. Ni maumivu kw wana-majumui wa Afrika.

Rest In Peace Comrade Bingu Wa Mutharika

Ndugu yangu Ben,

Hapo naomba kutofautiana na wewe ... siyo kwamba nafurahia kifo chake bali unachokisema hapo kwangu naona hakiko sahihi.

Mwana mapinduzi wa zama za sasa hawezi kukandamiza demokrasia ndani ya nchi kwa kutumia mtutu wa Bunduki na kuendeleza utawala wa ki-Sultan. Unajua running mate wa 2004 yuko wapi? Alisakiziwa kesi ya uhaini ambapo ukiwa convicted ni death penalty. Mwaka 2009 akachagua running mate tofauti, mama wa watu alipoona anawekwa pembeni na kwamba mgombea urais wa 2014 ni mdogo wa Bingu, mama akaamua kuanzisha chama chake.

Anapinga ubeberu huku yeye mwenyewe akiwa fisadi mkubwa, analazimisha mkewe alipwe mshahara wa dollar za Marekani zaidi ya 8,000 kwa mwezi kwa kazi ambayo inaweza kufanywa na Wizara ya Jinsia na Watoto.

Mwana mapinduzi anayeendeleza usultan kwa kumpendekeza mdogo wake awe mgombea Urais. Labda kama unaongelea mapinduzi ya zama za akina Castro - Cuba, na Korea ya Kaskazini ambako bado wanarithishana uongozi. So, kama umezaliwa kwenye ukoo/familia ambayo haina connection na ruling class basi imekula kwako.

Mwana mapinduzi wa kweli na mpinga sera za mabeberu, hawezi kuishi akiwa amezingirwa na ufisadi, nepotism, na ubabe ambao ulimfanya awe na maadui kila kona.

Mwezi uliopita walitaka kupeleka mswada wa mabadiliko ya sheria fulani, kikao cha Chama wakamwambia usidhani kwamba una numbers ndani ya Bunge kuna wabunge ni wa chama chako lakini they are not happy with what is going on chini uongozi wako serikalini na kwa kuwa ni kura ya siri, they will vote against na hutaweza kuwatambua ni akina nani. Ingekuwa ni kura ya wazi wangeweza kuogopa.

Kwangu mimi huyu hana tofauti na Mugabe, ni wale wale tu wanadai wanapingana na makaburu huku wao wakiendeleza ufisadi wa kufa mtu.
 
Nabii T.b Joshua akumbukwe.
hilo tayari, kinachofuata ni EL kuapishwa urais Tz

HAKUWAHI KUTABIRI HILO. TAFUTA KWA WEBSITE YA SCOAN AU EMMANUEL TV HUTAONA.
Kwa uhakika zaidi waandikie email kuwauliza. Haya ni mambo ya kizushi kama walivyoanza kumzushia "eti Mugabe ndio ametabiriwa anakufa".
 
"Medical sources said the ex-World Bank economist had been flown out because an energy crisis in the nation of 13 million was so severe the Lilongwe state hospital would have been unable to conduct a proper autopsy or even keep his body refrigerated."..."We know he is dead and unfortunately he died at a local, poor hospital which he never cared about - no drugs, no power," said Chimwemwe Phiri, a Lilongwe businessman waiting in a snaking line of cars for fuel at a petrol station."

HII INASIKITISHA SAANA.
 
TB JOSHUA mshenzi. akifanya mawasiliano na kujua kuna mtu anaumwa ndo anatabiri! Waamini ka misukule nanyi.

Bwana Paul Kijoka,

Hapo naomba nimtetee TB Joshua (haimaanishi kwamba nina amini unabii wake, maana sijui anatumia nini). Kama Mugabe ndo angekufa, then ningeweza kusema unabii wa TB Joshua una walakini. Maana siyo siri tena kwamba Bob Mugabe anaumwa saratani na alishaambiwa na madaktarri wake kwamba anaweza kuishi kwa miaka 5 (hii ni according to ule mtandao wa kutoa siri za cables WIKI).

Mutharika kama wiki 2 au 3 zilizopita alitamka kwenye vyombo vya habari kwamba utabiri wa TB Joshua haumlengi yeye, maana yeye ni mzima wa afya, hana matatizo ya afya. Ni rahisi kutoa prognosis ya mgonjwa wa cancer kuliko magonjwa mengine kama ya moyo ambayo hutokea ghafla bila kubisha hodi. Mfano mzuri ni juzi jinsi mchezaji Muamba alivyozimia ghafla na "kufa kwa muda wa dakika 78", before that he was very fine na alikuwa uwanjani akisakata kabumbu. Kwa hiyo hata kama TB Joshua angekuwa na detailed info za ugonjwa wa moyo wa Mutharika, bado asingeweza kutabiri maana wapo wagonjwa wengi sana wa moyo ambao huishi miaka mingi sana na wengine huwa wana magonjwa ya moyo lakini hawajui kama wanaumwa.

TB Joshua alisema Rais huyo anatokea Kusini na ni ambaye umri umeenda. Wengi walielekeza macho kwa Mugabe maana ndo mzee sana kuliko wenzake Angola, Zambia na Malawi (hawa wote walikuwa kwenye late 70s). Baada ya huo unabii (utabiri?) wananchi wa Zimbabwe walishakaa mkao wa kusubiri breaking news, bahati mbaya imekula kwao, breaking news imeenda Malawi, Mwisho, TB Joshua alisema kwamba Rais atakayekufa, atafariki kwa ugonjwa na kifo chake kitakuwa cha ghafla.

Kwa hiyo sina hakika kama anaweza kufanya mawasiliano na kujua details zote hizo. Hapa cha kujiuliza ni kwamba je ni maono kutoka kwa Mungu au anatumia nguvu za kiza?

Hayo ni maoni yangu tu, wafuasi na waumini wa TB Joshua naomba msinitoe macho.
 
RIP Wa Muthalika

Ukweli ni kwamba alikufa masaa mawili tu tangu kupatwa na hiyo attack na walimsafirisha Afrika Kusini kwa kuuhifadhi mwili usiharibike hadi mazishi yaani 'embalming". Magazeti binafsi ya malawi yameripoti kufukuzwa waandishi wote uwanja wa ndege usiku mwili wa kiongozi huyo ulipokuwa ukisafirishwa na wauguzi waliomhudumia waliripoti mkuu huyo kufariki ingawa hawakutaka kutajwa majina yao.
 
Bwana Paul Kijoka,

Hapo naomba nimtetee TB Joshua (haimaanishi kwamba nina amini unabii wake, maana sijui anatumia nini). Kama Mugabe ndo angekufa, then ningeweza kusema unabii wa TB Joshua una walakini. Maana siyo siri tena kwamba Bob Mugabe anaumwa saratani na alishaambiwa na madaktarri wake kwamba anaweza kuishi kwa miaka 5 (hii ni according to ule mtandao wa kutoa siri za cables WIKI).

Mutharika kama wiki 2 au 3 zilizopita alitamka kwenye vyombo vya habari kwamba utabiri wa TB Joshua haumlengi yeye, maana yeye ni mzima wa afya, hana matatizo ya afya. Ni rahisi kutoa prognosis ya mgonjwa wa cancer kuliko magonjwa mengine kama ya moyo ambayo hutokea ghafla bila kubisha hodi. Mfano mzuri ni juzi jinsi mchezaji Muamba alivyozimia ghafla na "kufa kwa muda wa dakika 78", before that he was very fine na alikuwa uwanjani akisakata kabumbu. Kwa hiyo hata kama TB Joshua angekuwa na detailed info za ugonjwa wa moyo wa Mutharika, bado asingeweza kutabiri maana wapo wagonjwa wengi sana wa moyo ambao huishi miaka mingi sana na wengine huwa wana magonjwa ya moyo lakini hawajui kama wanaumwa.

TB Joshua alisema Rais huyo anatokea Kusini na ni ambaye umri umeenda. Wengi walielekeza macho kwa Mugabe maana ndo mzee sana kuliko wenzake Angola, Zambia na Malawi (hawa wote walikuwa kwenye late 70s). Baada ya huo unabii (utabiri?) wananchi wa Zimbabwe walishakaa mkao wa kusubiri breaking news, bahati mbaya imekula kwao, breaking news imeenda Malawi, Mwisho, TB Joshua alisema kwamba Rais atakayekufa, atafariki kwa ugonjwa na kifo chake kitakuwa cha ghafla.

Kwa hiyo sina hakika kama anaweza kufanya mawasiliano na kujua details zote hizo. Hapa cha kujiuliza ni kwamba je ni maono kutoka kwa Mungu au anatumia nguvu za kiza?

Hayo ni maoni yangu tu, wafuasi na waumini wa TB Joshua naomba msinitoe macho.
Sasa ndiyo unataka tumwamini? Utabiri si lolote wala chochote na wala haudokezi ucha Mungu wa mtu. Huyu anaweza kuwa tapeli kama wengine tuliowazoea ambao hujitajirisha wakitumia Biblia na Jina la Yesu ambao hata hapa wamejaa lukuki. Yesu alishatuonya juu ya hilo.
Isitoshe kama ni utabiri wa vifo hata Sheikh Yahya alikuwa anatabiri mara nyingine kwa usahihi kabisa, ndiyo tuseme alikuwa nabii?
 
Marehemu Raisi Bingu wa Mutharika ana historia ndefu ktk nchi ya Malawi lakini zuri ambalo anaweza kukumbukwa nalo ni jinsi alivyowasaidia Wakulima wa Malawi kupata pembejeo kwa urahisi kwa kutoa Ruzuku kwa utaratibu mzuri ambao ulikuwa unaeleweka kwa kila mtu,mengi mabaya pia ameyafanya hasa kwa kutumia Dola kukandamiza Demokrasia,ikumbukwe kuwa Raisi huyu aliingia madarakani kwa nguvu ya aliekuwa Raisi wa wakati huo Dr Bakili Muluzi,aliempigia kampeni Nchi nzima ili atambulike,ilichukuwa muda mchache tu alitofautiana na Dr Muluzi hadi ikampelekea yeye kuanzisha Chama chake cha DPP ,kwa namna moja ama nyingine amepelekea anguko kubwa la uchumi wa nchi yake hautaamini hivi sasa thamani ya Kwacha imeshuka kwa kiwango kikubwa mno,maisha ya Wamalawi ni ya dhiki mno mafuta ya Dizeli ni shida mno kuyapata katika vituo vya kuuzia mafuta hayo baya zaidi hakuwa tayari kumsikiliza mtu yoyote lile alitakalo yeye basi ni lazima litekelezwe!
 
Sasa ndiyo unataka tumwamini? Utabiri si lolote wala chochote na wala haudokezi ucha Mungu wa mtu. Huyu anaweza kuwa tapeli kama wengine tuliowazoea ambao hujitajirisha wakitumia Biblia na Jina la Yesu ambao hata hapa wamejaa lukuki. Yesu alishatuonya juu ya hilo.
Isitoshe kama ni utabiri wa vifo hata Sheikh Yahya alikuwa anatabiri mara nyingine kwa usahihi kabisa, ndiyo tuseme alikuwa nabii?

Luhala hujalazimishwa kumuamini kiongozi kato yale yalio semwa sio lazima wewe kumuamini na hujalazimiswa kuamini
 
Back
Top Bottom