Binafsi sijaielewa hii picha

Binafsi sijaielewa hii picha

Kuna mamlaka zingine huwezi kukubali kama ni kweli zimetokana na watu,kuhusu vitambulisho yaani ni ukatiri wa hali ya juu kwa wauza mboga hata akijaza tenga hafikishi elfu kumi
 
Kama Mungu amekujalia maisha flani..yaani unajiweza....ukipata uteuzi wa ukuu wa wilaya awamu hii kimbia sana...
Hivi vyeo vya awamu hii ni kuchuma laana tu....
Mtu anakuja na VX yenye injini V8 na waandishi wa habari, polisi..msafara woote eti wanakuja kumkagua muuza mchicha kama ana kitambulisho cha mmachinga
 
Mtaji wa huyo mama muuza mchicha ni Buku moja tu, lakini amelazimishwa kuchujua kitambulisho cha mjasiriamali kwa Buku 20!!
Lakini umesahau kusema na Kodi alizokuwa anatakiwa kulipa kila siku kwenye mamlaka husika kwa kulinganisha na hiyo buku 20! ambayo ni kwa mwaka.
 
Mchicha Fungu mbili wenye thamani isiyozidi shipingi elfu moja, kitambulisho shingoni cha shilingi elfu ishirini.
Wacha porojo wewe, nani anafanya biashara ya kijinga ya kuuza fungu mbili kwa siku?
 
Back
Top Bottom