Binadamu & Viumbe hai tuna faida gani Duniani?

Binadamu & Viumbe hai tuna faida gani Duniani?

impongo

JF-Expert Member
Joined
Feb 18, 2015
Posts
8,844
Reaction score
7,904
Mada haihusiani na dini.

1. Viumbe hai tuna msaada gani kwa Dunia Nini faida yetu?

2. Nini thamani ya viumbe hai hapa duniani mchango wetu ni upi?

3. Ikitokea viumbe hai hakuna katika sayari hii, je Dunia itaathirika kwa lolote ni madhara gani yatakayoipata Dunia kutokana kutokuwepo viumbe hai?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Mada haihusiani na dini.

1. Viumbe hai tuna msaada gani kwa Dunia Nini faida yetu?

2. Nini thamani ya viumbe hai hapa duniani mchango wetu ni upi?

3. Ikitokea viumbe hai hakuna katika sayari hii, je Dunia itaathirika kwa lolote ni madhara gani yatakayoipata Dunia kutokana kutokuwepo viumbe hai?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app

Hapo mwanzo mungu aliziumba mbingu na nchi, baadae bustani ya eden na wanyama wote. Akamuumba m2 awatawale na kuitunza eden. Akale majani aina zote na matunda. Mungu akaona mtu mume (adamu) yuko upweke akamfanyia msaidizi, akawaambia wakazaane na kuongezeka.
NIMESHAKUJIBU JIONGEZE UTALIONA JIBU HAPO
 
" 1. Viumbe hai tuna msaada gani kwa Dunia Nini faida yetu?"

Viumbe hai hasa binadamu hawana faida yoyote kwa dunia zaidi ya kuifanyia uharibifu kama ukataji miti hovyo bila kupanda.

"2. Nini thamani ya viumbe hai hapa duniani mchango wetu ni upi?"

Hawana thamani wala mchango wowote.

" 3. Ikitokea viumbe hai hakuna katika sayari hii, je Dunia itaathirika kwa lolote ni madhara gani yatakayoipata Dunia kutokana kutokuwepo viumbe hai?"

Kwa asimilimia 99% hakutakuwa na madhara yoyote kwa dunia, itakuwa kama sayari nyingine isipokuwa yenyewe itakuwa safi yenye ukijani na miti ya kutosha na hewa safi na mandhari nzuri ya kusupport maisha ya viumbe hai.
 
Mada haihusiani na dini.

1. Viumbe hai tuna msaada gani kwa Dunia Nini faida yetu?

2. Nini thamani ya viumbe hai hapa duniani mchango wetu ni upi?

3. Ikitokea viumbe hai hakuna katika sayari hii, je Dunia itaathirika kwa lolote ni madhara gani yatakayoipata Dunia kutokana kutokuwepo viumbe hai?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile gani kea dunia? Au unangoja app
Jiulize, eewe una faida gani kwa dunia? Au u angora use halafu uwe crude oil 🛢?
 
Mkuu naomba unisikilize na unielewe.

Ipo hivi, binadamu ni chakula cha Mungu na Ibilisi. Yaani binadamu unaowaona hapa duniani ni mazao au mifugo iliyofugwa na Mungu ili baadaye iliwe.

Najua huwezi kunielewa, ila ukweli ni kwamba nafsi za binadamu ni chakula muhimu sana cha Mungu na Ibilisi ndiyo maana unaona Mungu na Ibilisi wanaugomvi usioisha. Sababu kubwa ya ugomvi wao ni nafsi yako wewe binadamu.

Ibilisi yupo tayari kufanya lolote ili apate nafsi yako ili aweze kusavaivu na hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu na yeye anatumia njia zake ili apate nafsi yako.

Ndio maana unaona watu wanazaliwa wapya maana yake Mungu amepanda mazao mapya kwa ajili ya chakula cha Mungu au Ibilisi, na watu wengine wanakufa maana yake nafsi imerudi na kuliwa na Mungu au na Ibilisi.

Kwa hiyo ikitokea binadamu wote hatupo duniani maana yake Mungu na Ibilisi watakosa chakula chao na watashindwa kusavaivu hivyo na wao watatoweka.

Ibilisi na Mungu hawana nguvu yoyote ya kusavaivu, kulinga na kujigamba kama dunia itakuwa haina binadamu.

Mungu alitumia akili kubwa sana ya kujitengenezea chakula chake ambacho ni sisi binadamu.

Hivyo viumbe vingine kwa asilimia kubwa vinasapoti maisha ya binadamu ili yaweze kutokea ili Mungu awe na uhakika wa kupata chakula chake.

Wewe ni chakula cha Mungu tu mkuu kwa hiyo lazima uwepo duniani kwa namna yoyote ile na kwa njia yoyote ile.

Huwezi ukaletewa Jua, mvua, mimea,samaki,maji,hewa n.k bure bure tu mkuu. Lazima na wewe uliwe.
 
Hapo mwanzo mungu aliziumba mbingu na nchi, baadae bustani ya eden na wanyama wote. Akamuumba m2 awatawale na kuitunza eden. Akale majani aina zote na matunda. Mungu akaona mtu mume (adamu) yuko upweke akamfanyia msaidizi, akawaambia wakazaane na kuongezeka.
NIMESHAKUJIBU JIONGEZE UTALIONA JIBU HAPO
Hujajibu swali naona porojo tu🤣🤣
Mtoa mada kauliza maswali vizuri tu wewe unaandika vitu vingine kabisa
 
Unaona mwanzo "sio mada ya dini" halafu unaenda kutoa maoni ya miungu... uzembe wa kufikiri na kuvunja maelekezo ni tatizo kubwa sana.

Anyway, kwenye mada viumbe sisi ni wanyonyaji tu. Tunazungusha carbon zetu kwenye uso wa dunia(viumbe vyote vinatokana na kaboni). Sayari na mifumo yake inasaidia kustahimili maisha yetu. Hatuna faida kwa sayari na ulimwengu kiujumla kwa mtazamo huo.

Viumbe mbalimbali vimeibuka na kutoweka kabisa bila dunia kutetereka. Hata leo tukitoweka hapa duniani kwa kuuana/kufa au kuhamia kwenye satellite au sayari ingne, sayari hii itaendelea kuzunguka na kugeuka kama hatukuwahi kutokea kwenye uso wake.

Sikuhizi vilio vya hali ya hewa na mabadiliko ya tabia nchi utasikia wakisema tulinde dunia. Ni kauli mbiu ya kisiasa sana. Watu waambiwe ukweli. Tunavyochezea ardhi, kaboni kuzipeperushia angani, kuchezea vyanzo vya maji n.k... tutakufa wakati dunia itaendelea na mwendo wake tu. Waseme "let's protect ourselves" na sio hizi ngonjera za kitafsida za "save the planet" na nyingne kama hizo.
 
" 1. Viumbe hai tuna msaada gani kwa Dunia Nini faida yetu?"

Viumbe hai hasa binadamu hawana faida yoyote kwa dunia zaidi ya kuifanyia uharibifu kama ukataji miti hovyo bila kupanda.

"2. Nini thamani ya viumbe hai hapa duniani mchango wetu ni upi?"

Hawana thamani wala mchango wowote.

" 3. Ikitokea viumbe hai hakuna katika sayari hii, je Dunia itaathirika kwa lolote ni madhara gani yatakayoipata Dunia kutokana kutokuwepo viumbe hai?"

Kwa asimilimia 99% hakutakuwa na madhara yoyote kwa dunia, itakuwa kama sayari nyingine isipokuwa yenyewe itakuwa safi yenye ukijani na miti ya kutosha na hewa safi na mandhari nzuri ya kusupport maisha ya viumbe hai.
Mkuu...miti na mimea ni sehemu ya viumbe hai.
 
Mada haihusiani na dini.

Kama aihusiani na dini inahusiana na nini???

1. Viumbe hai tuna msaada gani kwa Dunia Nini faida yetu?

Viumbe hai hatuna msaada wowote kwa dunia bali sisi ndio tunafaidika na dunia, mfano mtu awe na gari lake linalomsaidia katika usafiri hapo anayefaidika ni yeye na wala sio gari isipokuwa gari litahitaji matunzo ili liendelee kumsaidia huyo ndugu ni hivyohivyo kwa dunia ambapo inahitaji matunzo kutoka kwa viumbe hai hususan binadamu ambaye ndiye muharibifu mkubwa wa hii dunia.

2. Nini thamani ya viumbe hai hapa duniani mchango wetu ni upi?

Mchango wa viumbe hai kwa dunia hakuna kwani viumbe hai kiasili wametokana na dunia yenyewe kwahiyo viumbe hai ni sehemu ya dunia, mazingira ya dunia kamwe hayawezi kukosa viumbe hai, dunia ikikosa viumbe hai basi itakuwa sawa na a non life supporting planet(mfano wa sayari zingine) ambapo kwa hali ya dunia ilivyo jambo hilo haliwezi kutokea.

3. Ikitokea viumbe hai hakuna katika sayari hii, je Dunia itaathirika kwa lolote ni madhara gani yatakayoipata Dunia kutokana kutokuwepo viumbe hai?

Maana yake miti haitakuwepo duniani!!!!, Dunia itakuwa jangwa na joto kuongezeka mvua kubwa zitanyesha, barafu za north pole zitayeyuka na vina vya bahari vitaongezeka baadhi ya visiwa vitamwezwa na bahari, mafuriko kutokana na mvua kubwa zitaosha ardhi ya uso wa dunia na ardhi hiyo kujaa baharini hatimaye sehemu kubwa ya nchi kavu ya dunia itamezwa na maji ya bahari na sehemu kavu ya dunia itabakia ni miamba tupu.
 
Mada haihusiani na dini.

1. Viumbe hai tuna msaada gani kwa Dunia Nini faida yetu?

2. Nini thamani ya viumbe hai hapa duniani mchango wetu ni upi?

3. Ikitokea viumbe hai hakuna katika sayari hii, je Dunia itaathirika kwa lolote ni madhara gani yatakayoipata Dunia kutokana kutokuwepo viumbe hai?

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Atakuja yule mpuuzi wa "thibitisha" nami huwa namjibu sawasawa na upumbavu wake "METHALI 26:5" kuwa athibitishe uwepo wa hewa kimwonekano au kimguso/kushikika ikiwa anaamini uwepo wake basi hana lolote [emoji23]
 
" 1. Viumbe hai tuna msaada gani kwa Dunia Nini faida yetu?"

Viumbe hai hasa binadamu hawana faida yoyote kwa dunia zaidi ya kuifanyia uharibifu kama ukataji miti hovyo bila kupanda.

"2. Nini thamani ya viumbe hai hapa duniani mchango wetu ni upi?"

Hawana thamani wala mchango wowote.

" 3. Ikitokea viumbe hai hakuna katika sayari hii, je Dunia itaathirika kwa lolote ni madhara gani yatakayoipata Dunia kutokana kutokuwepo viumbe hai?"

Kwa asimilimia 99% hakutakuwa na madhara yoyote kwa dunia, itakuwa kama sayari nyingine isipokuwa yenyewe itakuwa safi yenye ukijani na miti ya kutosha na hewa safi na mandhari nzuri ya kusupport maisha ya viumbe hai.
"hakutakuwa na madhara yoyote kwa dunia, itakuwa kama sayari nyingine isipokuwa yenyewe itakuwa safi yenye ukijani na miti ya kutosha na hewa safi na mandhari nzuri ya "kusupport maisha ya viumbe hai."

[emoji3516][emoji3516]
"Kusapoti viumbe hai" hapa ndipo umerudi kwenye madhara yatotokea maana ulishasema hakutakuwa na madhara yoyote ikiwa dunia haitakuwa na viumbe hai.
 
"hakutakuwa na madhara yoyote kwa dunia, itakuwa kama sayari nyingine isipokuwa yenyewe itakuwa safi yenye ukijani na miti ya kutosha na hewa safi na mandhari nzuri ya "kusupport maisha ya viumbe hai."

[emoji3516][emoji3516]
"Kusapoti viumbe hai" hapa ndipo umerudi kwenye madhara yatotokea maana ulishasema hakutakuwa na madhara yoyote ikiwa dunia haitakuwa na viumbe hai.
Ndio mkuu, sababu uwepo wa viumbe hai duniani sasa hivi ni mazingira safi ya dunia yenye uwezo wa kusupport maisha.
Ila hapa tulikuwa tunaongelea kama theory tu yaani "what if" lakini technically sayari yoyote yenye mazingira safi kama ya dunia lazima kutatokea viumbe hai.
 
"hakutakuwa na madhara yoyote kwa dunia, itakuwa kama sayari nyingine isipokuwa yenyewe itakuwa safi yenye ukijani na miti ya kutosha na hewa safi na mandhari nzuri ya "kusupport maisha ya viumbe hai."

[emoji3516][emoji3516]
"Kusapoti viumbe hai" hapa ndipo umerudi kwenye madhara yatotokea maana ulishasema hakutakuwa na madhara yoyote ikiwa dunia haitakuwa na viumbe hai.
Ukisema ukijani tu umeharibu maana ukijani huo unatokana na viumbe hai ambavyo ni Mimea.

Yaani keakifupi Dunia mzima inakua empty Kama jangwa kote bila chochote.
 
Mkuu naomba unisikilize na unielewe.

Ipo hivi, binadamu ni chakula cha Mungu na Ibilisi. Yaani binadamu unaowaona hapa duniani ni mazao au mifugo iliyofugwa na Mungu ili baadaye iliwe.

Najua huwezi kunielewa, ila ukweli ni kwamba nafsi za binadamu ni chakula muhimu sana cha Mungu na Ibilisi ndiyo maana unaona Mungu na Ibilisi wanaugomvi usioisha. Sababu kubwa ya ugomvi wao ni nafsi yako wewe binadamu.

Ibilisi yupo tayari kufanya lolote ili apate nafsi yako ili aweze kusavaivu na hivyo ndivyo ilivyo kwa Mungu na yeye anatumia njia zake ili apate nafsi yako.

Ndio maana unaona watu wanazaliwa wapya maana yake Mungu amepanda mazao mapya kwa ajili ya chakula cha Mungu au Ibilisi, na watu wengine wanakufa maana yake nafsi imerudi na kuliwa na Mungu au na Ibilisi.

Kwa hiyo ikitokea binadamu wote hatupo duniani maana yake Mungu na Ibilisi watakosa chakula chao na watashindwa kusavaivu hivyo na wao watatoweka.

Ibilisi na Mungu hawana nguvu yoyote ya kusavaivu, kulinga na kujigamba kama dunia itakuwa haina binadamu.

Mungu alitumia akili kubwa sana ya kujitengenezea chakula chake ambacho ni sisi binadamu.

Hivyo viumbe vingine kwa asilimia kubwa vinasapoti maisha ya binadamu ili yaweze kutokea ili Mungu awe na uhakika wa kupata chakula chake.

Wewe ni chakula cha Mungu tu mkuu kwa hiyo lazima uwepo duniani kwa namna yoyote ile na kwa njia yoyote ile.

Huwezi ukaletewa Jua, mvua, mimea,samaki,maji,hewa n.k bure bure tu mkuu. Lazima na wewe uliwe.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Unaona mwanzo "sio mada ya dini" halafu unaenda kutoa maoni ya miungu... uzembe wa kufikiri na kuvunja maelekezo ni tatizo kubwa sana.

Anyway, kwenye mada viumbe sisi ni wanyonyaji tu. Tunazungusha carbon zetu kwenye uso wa dunia(viumbe vyote vinatokana na kaboni). Sayari na mifumo yake inasaidia kustahimili maisha yetu. Hatuna faida kwa sayari na ulimwengu kiujumla kwa mtazamo huo.

Viumbe mbalimbali vimeibuka na kutoweka kabisa bila dunia kutetereka. Hata leo tukitoweka hapa duniani kwa kuuana/kufa au kuhamia kwenye satellite au sayari ingne, sayari hii itaendelea kuzunguka na kugeuka kama hatukuwahi kutokea kwenye uso wake.

Sikuhizi vilio vya hali ya hewa na mabadiliko ya tabia nchi utasikia wakisema tulinde dunia. Ni kauli mbiu ya kisiasa sana. Watu waambiwe ukweli. Tunavyochezea ardhi, kaboni kuzipeperushia angani, kuchezea vyanzo vya maji n.k... tutakufa wakati dunia itaendelea na mwendo wake tu. Waseme "let's protect ourselves" na sio hizi ngonjera za kitafsida za "save the planet" na nyingne kama hizo.
Nimekuelewa vizuri sana mkuu.
 
Back
Top Bottom