A
Anonymous
Guest
Nina jambo ambalo linaumiza sana aisee, ni kuhusu Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) kwenye Kifurushi cha Toto Afya ambayo kinalipiwa Shilingi 150,000/=.
Mtoto wangu amezaliwa na tatizo la maji mengi kichwani (Hydrocephalus) na akafanyiwa operation Hospitali ya Taifa Muhimbili, anatakiwa kuendelea na clinic pamoja na mazoezi lakini cha ajabu hiki Kifurushi cha Toto Afya hakina uwezo wa kulipia mazoezi, na ukienda kwenye clinic zake za kichwa dawa zote muhimu kwa mfano ya degedege, haipo kwenye bima.
Inachoweza kufanya ni kulipia kuona daktari pamoja na vipimo vya kawaida sana kama damu lakini vile vyote vikubwa na muhimu ni lazima ulipe cash.
Kwahiyo hapa utu kwa watoto upo wapi jamani, wazazi wenye hawa watoto tunateseka sana na bima imekuwa sio msaada kabisa.
Tunaomba JamiiForums mtusaidie kupaza sauti zetu Wazazi tunaumia sana.
Mtoto wangu amezaliwa na tatizo la maji mengi kichwani (Hydrocephalus) na akafanyiwa operation Hospitali ya Taifa Muhimbili, anatakiwa kuendelea na clinic pamoja na mazoezi lakini cha ajabu hiki Kifurushi cha Toto Afya hakina uwezo wa kulipia mazoezi, na ukienda kwenye clinic zake za kichwa dawa zote muhimu kwa mfano ya degedege, haipo kwenye bima.
Inachoweza kufanya ni kulipia kuona daktari pamoja na vipimo vya kawaida sana kama damu lakini vile vyote vikubwa na muhimu ni lazima ulipe cash.
Kwahiyo hapa utu kwa watoto upo wapi jamani, wazazi wenye hawa watoto tunateseka sana na bima imekuwa sio msaada kabisa.
Tunaomba JamiiForums mtusaidie kupaza sauti zetu Wazazi tunaumia sana.