Biden atashinda, Trump is done

Biden atashinda, Trump is done

In life, good attitude will always take you far. Ulimi ni kiungo kidogo lakini chaweza kukuangamiza vibaya

Mtu kutwa kutoa kauli chafu. Anadiriki kumuita Dr. Fauci disaster, Kamala Harris monster....list ni ndefu

Trump anaenda kuponzwa na ulimi wake

Wacha ale jeuri yake
Keshapigwa
 
Nitakuwa muongo nikisema uchakachuzi upo upande mmoja tu.

Wanasiasa, kwa sababu moja au nyingine, huwa ni wa laghai laghai. Watafanya kila wawezalo ili wajinufaishe wao.

Kuhusu wapi Trump kachakachua, ni vigumu kusema kwa sababu hakuna sehemu ambayo mpinzani wake ameiangazia.

Hiyo inaweza ikawa ni sababu kwamba kwa sasa anaongoza. Angekuwa yuko nyuma, naamini angepata maeneo ya kuyalalamikia.

Hillary aliposhindwa unakumbuka alimlalamikia nani? Putin....siyo?

Al Gore je? Yeye alimlalamikia Jeb Bush, ambaye ndo alikuwa Gavana wa FL mwaka huo wa 2000.

Biden nahisi Fulton County, ambayo ni majority Democratic county, na ni county ambayo ina corruption ya hali ya juu, mimi naitilia mashaka sana. Kuna mambo yaliendelea ambayo yanatia shaka.

Philadelphia Pia, ambao ni mji wenye Democrats wengi, kuna nyakati waangalizi wa GOP walifungiwa nje mpaka ikabidi waende mahakamani.

Sasa hebu jiulize, katika huo muda ambao hawakuwemo kwenye vyumba vya kuhesabia, ni nini kilichokuwa kinaendelea?

Kuna incidents nyingi tu kama hizo na zimetokea kwenye ‘battleground’ states.

Kwa nini? Kwa nini hazijatokea Oregon au Washington?

Mimi si mshabiki kabisa wa hizi habari sijui advance voting, mail in voting, na upuuzi mwingine kama huo kwa sababu njia hizo zinatoa mianya mingi sana ya uchakachuzi.

Mimi napendelea watu wanapiga kura siku moja. Muda wa kupiga kura ukiisha, masanduku yanafunguliwa, kura zinahesabiwa hadharani mbele ya mashuhuda wote, zinajumlishwa, mshindi anatajwa.

Hizi habari za kuendelea kuhesabu kura siku 3, 4, au 5 baadaye ni chanzo cha uchakachuzi na zinashusha imani ya watu katika mfumo mzima uliopo.

Hivi kuhesabu na kujumlisha kura kwa nini kuchukue masiku yote hayo? Nini kilicho kigumu?

Hili suala hata huku kwetu ndilo linalopelekea watu kutokuwa na imani na chaguzi zetu.

Pamoja na yote hayo, mimi katika maisha yangu sijawahi kuathirika kwa namna yoyote ile kutokana na rais aliyepo madarakani.

Boksi lipo palepale na nisipobeba, watoto hawatokula.

Mzee Biden hawezi kuja kunilipia bili ya umeme, Trump hawezi kuja kunilipia bili ya maji, na Magufuli hawezi kunilipia ada za watoto.

Na hata nikifukuzwa kazi, wote hao hawawezi kuja kunipa kazi. Itabidi ninyanyuke mwenyewe nikachakarike mtaani kutafuta kibarua kingine.
IMG-20201106-WA0366.jpg
 
Hongera sana kwa correct prediction...

It's true that, it's almost done..

Pennsylvania State yenye Electoral College votes 20 inaenda mikononi mwa Joe Biden (D)..

Georgia yenye Electoral College votes 16 hata kama kwa sasa kunafanyika "vote recounting", obviously itakwenda kwa Joe Biden (D)..

Kuna possibility Joe Biden (D) akaweka rekodi ya kushinda kwa zaidi ya Electoral College votes 300..!!

This is shameful results for USA incumbent president...

Hii inaonesha kuwa, Rais aliye madarakani na anayetoka sasa hukufanya kazi yake vizuri kiasi cha kuwaudhi wananchi wengi..
IMG-20201107-WA0309.jpg
 
Hivi ile Ban tuliyopigwa na Trump ya kuingia USA Biden ataiondoa? Inaonesha Makonda alifunga na kuomba sana😀😀😀
 
Hivi ile Ban tuliyopigwa na Trump ya kuingia USA Biden ataiondoa? Inaonesha Makonda alifunga na kuomba sana😀😀😀
Mlipigwa ban? Wewe na nani?

Umenikumbusha kuna mfanyakazi mmoja wa uhamiaji nilikutana naye uwanja wa ndege Dar mwaka 2016 akanambia eti endapo Trump angeshinda, basi wabongo wote waliopo Marekani wangerudishwa.

🤣🤣🤣🤣🤣

Analysis za baadhi ya wabongo, hususan kuhusu siasa za Marekani huwa zinanichekesha sana.

Kuna mwingine, tena mtu wangu karibu kabisa, ile 2008 baada ya Obama kushinda eti akadai Marekani kutatokea vita kwa sababu Obama atawapendelea watu weusi na hivyo Wazungu watachukia.

Uelewa finyu sana wa mambo.
 
Imebaki wiki tatu lakini naamini Biden keshashinda na Trump keshashindwa.

Nimeangalia factors tofauti

1. Pesa -- siku zote mgombea anaeweza changisha hela nyingi anashinda. Biden kamzidi Trump kwa mbali

2. Swing states -- Ohio na Florida kote Biden ana-lead.

3. Pandemic -- Hili mradi ni main news Trump hawezi shinda.

Naona Biden atakuwa new President. Trump is done!
Nimesema mara kadhaa hapa kwamba suala la COVID-19 ndio moja ya sababu kuu ya kushindwa Trump, watu hawaelewi.
 
Nimesema mara kadhaa hapa kwamba suala la COVID-19 ndio moja ya sababu kuu ya kushindwa Trump, watu hawaelewi.

Actually covid haijaleta impact kama ilivyotarajiwa..
Idadi ya kura alizopata Trump imeongezeka sana kuzidi mwaka 2016..
Na idadi ikubwa hawajamlaumu kuhusu covid..

Racial inequality wamesema ndo angalau
Ambao wamempigia Biden ndo no 1 factor
 
Trump keshaanza kutembeza Clearance form hapo White house au Bado!??
 
Jaman si mtabiri kuhusu Tz pia na iwe kweli
 
Mlipigwa ban? Wewe na nani?

Umenikumbusha kuna mfanyakazi mmoja wa uhamiaji nilikutana naye uwanja wa ndege Dar mwaka 2016 akanambia eti endapo Trump angeshinda, basi wabongo wote waliopo Marekani wangerudishwa.

🤣🤣🤣🤣🤣

Analysis za baadhi ya wabongo, hususan kuhusu siasa za Marekani huwa zinanichekesha sana.

Kuna mwingine, tena mtu wangu karibu kabisa, ile 2008 baada ya Obama kushinda eti akadai Marekani kutatokea vita kwa sababu Obama atawapendelea watu weusi na hivyo Wazungu watachukia.

Uelewa finyu sana wa mambo.
Mkuu Umesahau Tanzania ilipigwa ban ya kutokuingia USA? Pamoja na Nigeria, na nchi zingine tano..

Pamoja na makonda na familia yake wakapigwa life ban ..juzi kati tu hapa.
 
Actually covid haijaleta impact kama ilivyotarajiwa..
Idadi ya kura alizopata Trump imeongezeka sana kuzidi mwaka 2016..
Na idadi ikubwa hawajamlaumu kuhusu covid..

Racial inequality wamesema ndo angalau
Ambao wamempigia Biden ndo no 1 factor
Kweye COVID-19 Trump mara nyingi amewadharau wataalam wa afya na ushauri wao.

Dr Fauci na wengine wamepata taabu sana kufanya kazi na Trump.

Biden ameahidi kufanya kazi na wataalam na pia kuwahimiza wamarekani kuvaa barakoa.

Pia ameahidi kutoa dawa ya chanjo bure kwa kila mmarekani.

Ukizungumza hivi vitu mbele ya wapiga kura hukosi kitu.
 
Nimesema mara kadhaa hapa kwamba suala la COVID-19 ndio moja ya sababu kuu ya kushindwa Trump, watu hawaelewi.
Mimi nadhani ni character.

C-19 ni kama imekuja tu kuongeza ladha mwishoni mwishoni hapa.

Kwa sababu, kama sababu kuu ingekuwa ni C-19, basi ungeona huo ushindi umepenyeza hadi kwenye bunge [Reps na Senate], State legislatures, na kwenye ugavana wa majimbo.

Hilo halijatokea.

Matter of fact, GOP wameongeza viti kwenye House of Representatives. More than likely the house will be split 50-50 or thereabouts. Hivyo, siku za Nancy Pelosi kuwa spika zinahesabika.

Kwenye senate more than likely GOP wata maintain majority, albeit a slim one. But a majority nonetheless.

Kwenye state legislatures, GOP wameweza ku flip state legislatures 3, na hivyo kuongeza idadi ya majority ya legislatures zinazoongozwa na GOP.

Na hilo suala ni muhimu sana kwa redistricting ambayo yaweza ku determine house majority for the foreseeable future.

Kwenye ugavana pia, GOP wana viti vingi kuliko Dems. Asilimia 52 hivi, kama sijakosea.

Hivyo, hakukuwa na blue wave kama ambavyo polls zilikuwa zinadai.

Kilichokuwepo ni rejection tu ya Donald Trump, hususan kutokana na tabia yake.

Kama ingekuwa ni rejection ya GOP policies, ni lazima ingekuwa reflected kwenye nafasi zingine.

Mfano, ni majuzi tu hapa senate GOP wamem confirm Justice Amy Coney Barret kwenda kwenye Supreme Court. Lakini hilo halijawa cost kwenye sanduku la kura.

Na kuna GOP wengi saana ambao hawakumpigia kura Trump, bali walipiga kura dhidi yake kwa kumpigia kura Biden.

Hilo kundi halitokuwepo tena 2024. Litarudi nyumbani.

The 2020 US election was a referendum on Donald Trump mainly because of his character.
 
Back
Top Bottom