oba
JF-Expert Member
- Oct 31, 2010
- 310
- 65
Leo nilipoenda mhimbili hospitali kumwona ngugu yangu mgonjwa nilikutana na bibi mmoja akitokwa machozi na mama mmoja alipotaka kujua kulikoni alionesha cheti cha msamaha wa matibabu na kulalamika kuwa pamoja na cheti hicho hajapata matibabu ya dawa alizoandikiwa na daktari eti kwa kuwa hazipatikani katika pharmacy ya hapo hospitali ya taifa. Nilipomtazama kwa makini nikamfananisha na bibi mmoja aliyekuwa akishangilia hotuba ya JK juzi akifurahia na kumshangilia Raisi kwa kuwafanya madaktari kusitisha mgomo bila kujali kama madai yao ya kuboreshwa mazingira ya kazi na uwepo wa vifaa tiba yametekelezwa au la.
My take.
Tusifurahi madaktari kusitisha mgomo ila twapaswa kufurahi kuwa madai yao yametekelezwa vinginevyo sisi wananchi ndio tutakaoumia!!
My take.
Tusifurahi madaktari kusitisha mgomo ila twapaswa kufurahi kuwa madai yao yametekelezwa vinginevyo sisi wananchi ndio tutakaoumia!!