Biashara ya Utumwa:Mfalme wa Udachi aomba radhi.

Webabu

JF-Expert Member
Apr 29, 2010
7,183
10,913
1688276332627.png

Mfalme wa Udachi (Netherlands) ameomba radhi kutokana na nchi hiyo kupata faida kubwa iliyotokana na biashara ya kuuza watu mnamo karne ya 17.
Katika hotuba yake kwa taifa kuadhimisha miaka 160 tangu kupigwa marufuku kwa biashara hiyo, mfalme Willem-Alexander akiambatana na mkewe bi Maxima amesema nchi yake ilisafirisha na kuuza watu duniani kote kabla ya marufuku hiyo
Katika mapitio ya kumbukumbu za biashara hiyo imejulikana kuwa Udachi ilipata jumla ya dola milioni 595 baina ya mwaka 1675 na 1770 kwa kusafirisha waumwa wasiopungua 600,000.
Maelfu ya waafrika walinunuliwa na kusafirishwa kwenda makoloni ya Udachi yaliyokuwa visiwa vya Carribean na Amerika ya kusini, hata hivyo hiyo ilikuwa ni asilimia 5 ya biashara yote ya utumwa..Sehemu kubwa ilikuwa ni biashara ya Uiengereza na Marekani ambapo meli iliyokuwa ikibeba watumwa ya ufalme wa Uiengereza iliyoitwa Jesus ilipewa nishani kwa kuleta faida kubwa iliyotokana na biashara hiyo ya utumwa duniani.
Waiengereza walinunua watumwa wengi kutoka Afrika ya magharibi huku wachache wakiwatoa kutoka Afrika Mashariki.
Biashara ya utumwa Afrika mashariki ilifanyika katika muda wa karibu na kupigwa marufuku kwa biashara hiyo mwaka 1863 wakati wa utawala wa ufalme wa Zanzibar ulioanza mwaka 1832.
.Waiengereza waliamua kusitisha biashara hiyo baada ya uvumbuzi mkubwa wa mitambo iliyofanya kazi zilizofanywa na watumwa kwenye makoloni yao na kupelekea kusafirisha watumwa na kuwatunza kuwa ni ghali zaidi
 
Amefanya vyema.
Pia bado mataifa mengi yanatakiwa kufikia hatua ya kuomba radhi na kufanya reparations.
Spain
Portugal
Middle East Arabs( Hawa walikuwa suppliers kutoka East Africa).
England hawa ndo walikuwa washenzi zaidi
Na miafrika baadhi ilishiriki kuuza wenzao
 
Waafrika tuliishayakanyaga.

Kwa mtazamo wangu, kutumikishana ni pale mmoja anakuwa ana akili na mwingine ni mjinga.

Miaka ile Waingereza waliitawala robo tatu ya dunia mpaka unashangaa mababu wetu walikuwa wajinga kiasi gani! Unakuta mzungu mmoja anawalinda Waafrika kadhaa na hakuna Mwafrika anayefurukuta.

Hata leo hii Waafrika tunaendelea kutumikishana ndani ya nchi zetu na hakuna anayefurukuta.

Wazungu wanatengeneza mazingira ya kuendelea kututawala hata wakiwa wachache. Kwa mfano, sisi Watanzania tunawezaje kuja kuwatumikisha Wazungu au Waarabu ikiwa wanatudai pesa nyingi na tunaendelea kuwaomba misaada?

Je, Waafrika tuna ujasiri wa kukataa kulipa madeni ya nje?








Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
Waafrika tuliishayakanyaga.

Kwa mtazamo wangu, kutumikishana ni pale mmoja anakuwa ana akili na mwingine ni mjinga.

Miaka ile Waingereza waliitawala robo tatu ya dunia mpaka unashangaa mababu wetu walikuwa wajinga kiasi gani! Unakuta mzungu mmoja anawalinda Waafrika kadhaa na hakuna Mwafrika anayefurukuta.

Hata leo hii Waafrika tunaendelea kutumikishana ndani ya nchi zetu na hakuna anayefurukuta.

Wazungu wanatengeneza mazingira ya kuendelea kututawala hata wakiwa wachache. Kwa mfano, sisi Watanzania tunawezaje kuja kuwatumikisha Wazungu au Waarabu ikiwa wanatudai pesa nyingi na tunaendelea kuwaomba misaada?

Je, Waafrika tuna ujasiri wa kukataa kulipa madeni ya nje?








Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Mkuu umeongea vzr sana na kinachonishangaza sisi tume tukia Jana kwamba hatuna Kazi ya kufanya Kila siku kuomba mikopo tu hatuhangaiki kutafuta namna ambavyo tunaweza shindana nao Kama sio kuwa pita tuki kwenye usingizi mzito
 
Amefanya vyema.
Pia bado mataifa mengi yanatakiwa kufikia hatua ya kuomba radhi na kufanya reparations.
Spain
Portugal
Middle East Arabs( Hawa walikuwa suppliers kutoka East Africa).
England hawa ndo walikuwa washenzi zaidi
Na miafrika baadhi ilishiriki kuuza wenzao
Walikuwa wanawachoma moto watumwa utadhani mbuzi ili iwe kama alama ya anaowamiliki.
 
Walitukosea halafu wakaja kutuletea maandiko ya kujifunza kusamehe.

Sometime unashindwa elewa kanchi kadogo kama UK kaliwezaje kutawala dunia ?
Ka Japan kaliwezaje kwa Wachina!?

Baadaye wajukuu watajiuliza Ka U.A. Emirate na Dubai waliwezaje!?
 
Waafrika tuliishayakanyaga.

Kwa mtazamo wangu, kutumikishana ni pale mmoja anakuwa ana akili na mwingine ni mjinga.

Miaka ile Waingereza waliitawala robo tatu ya dunia mpaka unashangaa mababu wetu walikuwa wajinga kiasi gani! Unakuta mzungu mmoja anawalinda Waafrika kadhaa na hakuna Mwafrika anayefurukuta.

Hata leo hii Waafrika tunaendelea kutumikishana ndani ya nchi zetu na hakuna anayefurukuta.

Wazungu wanatengeneza mazingira ya kuendelea kututawala hata wakiwa wachache. Kwa mfano, sisi Watanzania tunawezaje kuja kuwatumikisha Wazungu au Waarabu ikiwa wanatudai pesa nyingi na tunaendelea kuwaomba misaada?

Je, Waafrika tuna ujasiri wa kukataa kulipa madeni ya nje?








Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Wazungu wanaidharau na wanaipangia Afrika nini cha kufanya, Museveni alisimulia jinsi Marais sita kutoka nchi za Barani Afrika walivyoamrishwa kutokwenda Libya kutafuta usuluhishi na Gaddafi mambo yalipoharibika

 
Afadhali wameomba radhi ila Bado wanatutawala kwa kutumia akili, Kuna kipindi nchi za kiafrika walikutana wadai fidia ila baadhi ya nchi kwa makusudi wakavuruga mkutano kwa kuingiza swala la Palestinia na Israel
 
Naamini ipo siku Wazungu watakuja kutumikishwa na Mwafrika,. FACTOR ni Wazungu wanapoteza ulijali na nguvu kazi sababu ya Homosexuality. Pia uzazi umeshuka Sana. Watakuwa na nguvu za sayansi wakati manpower ina collapse
Waafrika wanaouza bandar
 
Waafrika tuliishayakanyaga.

Kwa mtazamo wangu, kutumikishana ni pale mmoja anakuwa ana akili na mwingine ni mjinga.

Miaka ile Waingereza waliitawala robo tatu ya dunia mpaka unashangaa mababu wetu walikuwa wajinga kiasi gani! Unakuta mzungu mmoja anawalinda Waafrika kadhaa na hakuna Mwafrika anayefurukuta.

Hata leo hii Waafrika tunaendelea kutumikishana ndani ya nchi zetu na hakuna anayefurukuta.

Wazungu wanatengeneza mazingira ya kuendelea kututawala hata wakiwa wachache. Kwa mfano, sisi Watanzania tunawezaje kuja kuwatumikisha Wazungu au Waarabu ikiwa wanatudai pesa nyingi na tunaendelea kuwaomba misaada?

Je, Waafrika tuna ujasiri wa kukataa kulipa madeni ya nje?








Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Mf anachofanya Sa100 makosa ni ya babu zetu km Sa100 anavyouza nch
 
Nasema hivi hata Leo hii biasharaa ya utumwa ikirudi Tena kwa hiari hakuna mwafrika atabakia Afrika hata hizo meli hazitotosha kusomba watu,Kama Leo maelfu ya vijana Kila siku kutwa kuzururusha kwenye ofisi za balozi zao wanapambania viza waende ulaya plus wale waendao kwa njia ya panya huku wengi wakifa baharini utasemaje utumwa umeisha huku ndoto za wengi ni kuzamia Ulaya.
 
View attachment 2675878
Mfalme wa Udachi (Netherlands) ameomba radhi kutokana na nchi hiyo kupata faida kubwa iliyotokana na biashara ya kuuza watu mnamo karne ya 17.
Katika hotuba yake kwa taifa kuadhimisha miaka 160 tangu kupigwa marufuku kwa biashara hiyo, mfalme Willem-Alexander akiambatana na mkewe bi Maxima amesema nchi yake ilisafirisha na kuuza watu duniani kote kabla ya marufuku hiyo
Katika mapitio ya kumbukumbu za biashara hiyo imejulikana kuwa Udachi ilipata jumla ya dola milioni 595 baina ya mwaka 1675 na 1770 kwa kusafirisha waumwa wasiopungua 600,000.
Maelfu ya waafrika walinunuliwa na kusafirishwa kwenda makoloni ya Udachi yaliyokuwa visiwa vya Carribean na Amerika ya kusini, hata hivyo hiyo ilikuwa ni asilimia 5 ya biashara yote ya utumwa..Sehemu kubwa ilikuwa ni biashara ya Uiengereza na Marekani ambapo meli iliyokuwa ikibeba watumwa ya ufalme wa Uiengereza iliyoitwa Jesus ilipewa nishani kwa kuleta faida kubwa iliyotokana na biashara hiyo ya utumwa duniani.
Waiengereza walinunua watumwa wengi kutoka Afrika ya magharibi huku wachache wakiwatoa kutoka Afrika Mashariki.
Biashara ya utumwa Afrika mashariki ilifanyika katika muda wa karibu na kupigwa marufuku kwa biashara hiyo mwaka 1863 wakati wa utawala wa ufalme wa Zanzibar ulioanza mwaka 1832.
.Waiengereza waliamua kusitisha biashara hiyo baada ya uvumbuzi mkubwa wa mitambo iliyofanya kazi zilizofanywa na watumwa kwenye makoloni yao na kupelekea kusafirisha watumwa na kuwatunza kuwa ni ghali zaidi

Meli inaitwa jesus na hapo mataifa yaliyotajwa yote ni ya ulaya ila mitanzania yenye chuki na upumbav itaanza wasema waarabu yaani alituloga waafrica kafa mda mrefu xnaa
 
Back
Top Bottom