MAMA POROJO
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 4,974
- 785
Mkuu Majimoto
Mimi maranyingi sana usiku huwa nahisi kama vile nimevamiwa na mwili huwa mzito sana huwa nahisi kabisa kuna wachawi wananichezea na huwa siwezi hata kutikisika na sometimes huhisi kukabwa ila cha ajabu nikiwa kwenye hali hii huwa najikuta nakemea bila kujijua kwa kutumia jina la Yesu na nikiona mpambano umekuwa mkali huomba msaada wa damu ya YESU na moto wa roho mtakatifu hapo hata kama walikuwa wengi kiasi gani na wakali kiasi gani lazima watoke nduki na nikishtuka naona kabisa mwili wangu upo tofauti na najihisi tofauti ninachoshangaa ni kuwa huwa nipo usingizini akili ya kukemea huwa naitoa wapi? huwa inakuja automatic? na kwanini? Na cha kushangaza mimi sijasimama sana katika imani japokuwa naamini Mungu ndo kila kitu na sina kinga zozote za kiganga!!!!! na hii huwa inatokea sana siku nikijisahau kulala bila kusali
Maelezo tafadhali
Wachawi huchezea na kuumiza watu wengi sana usiku. Wanapoingia chumbani kwako hupulizia dawa za usingizi za kichawi unalala usingizi mzito kama wa mgonjwa anayefanyiwa upasuaji hospitalini, wakishapuliza mchawi mmoja hukaa juu ya kifua chako kama vile anaendesha pikipiki na mchawi mwingine hukaa juu ya miguu yako kama vile anaendesha pikipiki halafu wachawi wanaangaliana. Machawi aliyekaa juu ya kifua chako karibu ya shingo huruka juu na kutua juu ya kifua chako kwa mata.ko kwa nguvu, akitua chini, mchawi aliyekalia miguu yako naye huruka juu na kutua juu ya miguu yako, mchezo huo huendelea hadi wanahakikisha kuwa kipigo hicho kimekuigia vizuri.
Wakati mwingine wachawi huwa wanachukua watu wazima wazima usiku na kuondoka nao kwenda kuwanga. Wanachofanya huingiza mzimu wa uchawi ndani yako ukiwa umelala, mzimu ukishaingia unainuka kitandani na unaondoka nao kwenda kuwanga, aidha kama siku hiyo ni siku ya kucheza ngoma za kichawi nawe utashiriki, kama siku hiyo ni siku ya kwenda makaburi kufukua maiti utashiriki na kula nyama za maiti, kama siku hiyo ni siku ya kuingia ndani ya nyumba za watu na kukalia watu nawe utakuwa ndio namba moja.
Ndiyo maana, utakuta watu wengi wanapoamka asubuhi, wanakuwa wachovu kwelikweli, shingo zikiuma na miguu ikiwaka moto. Kama umeamka asubuhi na kuanza kunyosha mikono kila upande na kupiga miayo mingi, ndugu ujue ulikaliwa usiku huo.
Kwa kawaida mtu akiwa na njaa huwa mlegevu na kupiga miayo, akipewa chakula njaa hutulia na anapata nguvu mpya, mtu pia akiwa na kiu akipata maji ya kunywa kiu huisha na kupata nguvu hasa kwa wale wanaofanya kazi ngumu juani.
Mtu akiwa amechoka huhitaji mapumziko, mapunziko mazuri ni kuulaza mwili kitandani au juu ya mkeka na unapoamka mwili unakuwa mchangamfu na mwenye nguvu. Tatizo kubwa hutokea unapolala usiku, kwa nini unapoamka mwili uwe mchovu, wakati dawa ya uchovu ni usingizi?. Ndugu hiyo ndiyo kazi za wachawi kuchezea watu usiku kama vile chapati inavyogeuzwa ikiwa ndani ya kikaango ndivyo hivyo hivyo wanakugeuza na kukukalia kwa nguvu usiku.