Makwarukwaru
Member
- Mar 10, 2012
- 66
- 25
Kwa mtazamo wa kawaida, madawa ya kulevya ni kitu kinachopigwa vita sana. lakini kiuhalisia haiko hivyo. Kwani watu wanauza madawa haya peupe bila woga wala wasiwasi. Nani yuko nyuma ya biashara hii?ananguvu kiasi gani mpaka imekua halali kiasi hiki?Ukitembelea maeneo ya kawe ukwamani vijana wanatumia madawa 24/7 bila kificho wala wasiwasi,nani yuko nyuma yao anaewapa kichwa kiasi hiki? Sijataka kusema maeneo mengine ila hali ni mbaya,kama serikali kila mara inapiga kelele kuhusu madawa hawa mbona hawakamatwi? Mwisho, bangi ikikamatwa huwa inaharibiwa tunaona, ule unga unaokamatwa huwa unapelekwa wapi au unafanywa nini?