Biashara ya kuuza mifumo

Biashara ya kuuza mifumo

blind fighter

Member
Joined
May 17, 2021
Posts
85
Reaction score
128
Wakuu habari za wakati. ni muda sasa toka nimemaliza chuo, mwaka huu mwezi wa saba natimiza miaka miwili mtaani.

Chuoni nimesoma Shahada ya Teknolojia ya Habari za Biashara (bachelor in bussiness Infomation Technology). Mwaka jana mwezi wa pili nimepata kazi kwenye kampuni moja hivi ya kufundisha hapa hapa dar es salaam.

Kutokana na ugumu wa maisha punde tu baada ya kutoka chuoni, nilizama kwenye ile kazi hadi leo, bado nafundisha pale. ila ninachofundisha hakiendani na fani, mshahara ni laki 5 take home, japo nimejaribu kuomba kuongezewa mshahara ila bado.

umri unaelekea miaka 30, no any development step nimefanya, japo kuna saving kidogo nimefanya kwenye account, nimeomba kazi mbali mbali ilasjafanikiwa kupata.

Nina uelewea wa IT, i can read and deburg codes, network basics, system administration and intermediate of data analystics (Excel, SQL and poweBI as my favourite visualization tool).

Kwa kuwa umri umeenda, ugumu wa maisha na kutegemewa na familia kijijini, sikupata muda wa kukaa na kutengeneza system yoyote as a project, nimekaa chini nikapata wazo la baishara ya kuuza na kutoa huduma zamifumo ikiwemo

  • Multi Tenant School Management System
  • Online Exam for Coaching / Training Institute (Complete Premium) with Android App
  • Ecommerce Shopping Website (Complete Website) plus Android App
  • Multi-Tenancy eCommerce Platform (Laravel)
  • Food Delivery App with Admin Panel and Delivery Man App
  • Taxi Booking Application (Android & iOS App) with Admin Panel
  • ERP, Stock Management, Point of Sale & Invoicing Application
  • SaaS-Based Invoicing and Billing Platform (PHP Script)
  • Hospital Management System PHP Website with Android App
  • Multi-Hospital Management SaaS Application with Mobile Apps
  • Online Matrimonial Portal (digital platform where people can find life partners)
Hii mifumo sio kwamba nimeitengeneza, nanunua, na ipo tayari. sitoanza na yote, bali nitachagua mmoja au miwili
Sasa nimekuja kwenu kuomba ushauri juu ya haya maamuzi, changamoto ya biashara hii na faida yake.
Pia nipo tayari kwa kazi za ufundishaji au hata za kiofisi kama data analyst.
 
Toka asubuhi nimeuona uzi wako ila sasa kingereza ulichoandikq hapo katikati ndiyo kinanifanya kila muda nichungulie walau nikute kuna waliochqngia na mimi nielewe niweze kuchangia maana sielewi chochote mdogo wangu .

Ila haina shida fanya nadhani itakuwa biashara nzuri sana
 
Vyote hivyo viko poa mkuu,ishu unawafikia vipi wateja?
Yani marketing?
 
ili kuongeza kipato naona ongeanza kufannya freelancing jobs as data analyist online
 
Wakuu habari za wakati. ni muda sasa toka nimemaliza chuo, mwaka huu mwezi wa saba natimiza miaka miwili mtaani.
chuoni nimesoma Shahada ya Teknolojia ya Habari za Biashara (bachelor in bussiness Infomation Technology). Mwaka jana mwezi wa pili nimepata kazi kwenye kampuni moja hivi ya kufundisha hapa hapa dar es salaam. kutokana na ugumu wa maisha punde tu baada ya kutoka chuoni, nilizama kwenye ile kazi hadi leo, bado nafundisha pale. ila ninachofundisha hakiendani na fani, mshahara ni laki 5 take home, japo nimejaribu kuomba kuongezewa mshahara ila bado.

umri unaelekea miaka 30, no any development step nimefanya, japo kuna saving kidogo nimefanya kwenye account, nimeomba kazi mbali mbali ilasjafanikiwa kupata.

Nina uelewea wa IT, i can read and deburg codes, network basics, system administration and intermediate of data analystics (Excel, SQL and poweBI as my favourite visualization tool).

Kwa kuwa umri umeenda, ugumu wa maisha na kutegemewa na familia kijijini, sikupata muda wa kukaa na kutengeneza system yoyote as a project, nimekaa chini nikapata wazo la baishara ya kuuza na kutoa huduma zamifumo ikiwemo

  • Multi Tenant School Management System
  • Online Exam for Coaching / Training Institute (Complete Premium) with Android App
  • Ecommerce Shopping Website (Complete Website) plus Android App
  • Multi-Tenancy eCommerce Platform (Laravel)
  • Food Delivery App with Admin Panel and Delivery Man App
  • Taxi Booking Application (Android & iOS App) with Admin Panel
  • ERP, Stock Management, Point of Sale & Invoicing Application
  • SaaS-Based Invoicing and Billing Platform (PHP Script)
  • Hospital Management System PHP Website with Android App
  • Multi-Hospital Management SaaS Application with Mobile Apps
  • Online Matrimonial Portal (digital platform where people can find life partners)
Hii mifumo sio kwamba nimeitengeneza, nanunua, na ipo tayari. sitoanza na yote, bali nitachagua mmoja au miwili
Sasa nimekuja kwenu kuomba ushauri juu ya haya maamuzi, changamoto ya biashara hii na faida yake.
Pia nipo tayari kwa kazi za ufundishaji au hata za kiofisi kama data analyst.
Oa kwanza, achana na mambo ya mifumo. Miaka 30 sio michache kuanza kuwa na familia...kipato cha laki 5 kinatosha sana kuendesha familia.
 
Nachokushauri mkuu usikate tamaa, Anza kufanya research ya ICT startups companies na mid-size ICT companies zilizopo kwenye jamii unayoishi.

Kwa Dar-es-salaam, Dodoma, Mwanza na Arusha zipo nyingi sana.

Team up na hizo startups ambazo tayari zimeshatengeneza marketing na zina bidhaa sokoni ili mwende Sawa.

Kinachotuangusha waafrika hasa nyie watu wa IT ni kila mmoja kuwa kivyake, huko kwenye partnership utapata watu ambao wapo kwenye soko na wanajua kuwafikia wateja. Pamoja mtafika mbali

Best wishes.
 
Mkuu nimesoma hizo system zako zote, lakini hakuna kipya hapo. Hizo zote zipo tayari na zilishafanyika.
Nakushauri tafta resources mbalimbali na uongeze ubunifu zaidi, piaa tafta watalaam wa software, computer na automation wakuelekeze mbinu tofauti tofauti. Hizo za kwako hapo juu utachelewa sana zipo tayari hta Mimi baadhi nazidevelop vzr tu.
 
Kusoma ni rahisi sana, mtihani waga ni kubadiri kisomo kuwa hela.
Kila la kheri mtoa mada.
 
Katafute asset, achan na utoto.
Jamii yetu bado hatupo huko......save for future use.
 
Back
Top Bottom